Hamu mpya ya kumfahamu Abdul Sykes na historia ya TANU

Hamu mpya ya kumfahamu Abdul Sykes na historia ya TANU

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
HAMU MPYA YA KUMFAHAMU ABDUL SYKES NA HISTORIA YA TANU

Kumekuwa na mwamko mpya wa kushangaza kuhusu historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Juma lililopita tukielekea Nyerere Day nimekuwa nikihojiwa na televisheni takriban kila baada ya siku na wakati mwingine siku zikifukuzana mfululizo.

Ajabu ya Rahman hawa vijana wameshikwa sana na historia ya mchango wa Abdul Sykes katika kuasisi chama cha TANU.

Nimewauliza kama hawachoki kuwaonyesha watazamaji wao historia hii kwani kila ajae kwangu hatakosa maswali kuhusu Abdul Sykes na TANU.

''Mzee Mohamed sisi tunasikiliza hotuba za Baba wa Taifa kila siku usiku sasa miongo miwili baada ya kufa kwake na Mwalimu Nyerere anahutubia taifa na hatujachoka kumsikiliza.

Historia ya Abdul Sykes hatukupata kusomeshwa hata vyuoni sasa tuna kiu nayo.

Kwani wewe unaona tabu kuihadithia?''

Screenshot_20211002-220909_Facebook.jpg
 
HAMU MPYA YA KUMFAHAMU ABDUL SYKES NA HISTORIA YA TANU

Kumekuwa na mwamko mpya wa kushangaza kuhusu historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Juma lililopita tukielekea Nyerere Day nimekuwa nikihojiwa na televisheni takriban kila baada ya siku na wakati mwingine siku zikifukuzana mfululizo.

Ajabu ya Rahman hawa vijana wameshikwa sana na historia ya mchango wa Abdul Sykes katika kuasisi chama cha TANU.

Nimewauliza kama hawachoki kuwaonyesha watazamaji wao historia hii kwani kila ajae kwangu hatakosa maswali kuhusu Abdul Sykes na TANU.

''Mzee Mohamed sisi tunasikiliza hotuba za Baba wa Taifa kila siku usiku sasa miongo miwili baada ya kufa kwake na Mwalimu Nyerere anahutubia taifa na hatujachoka kumsikiliza.

Historia ya Abdul Sykes hatukupata kusomeshwa hata vyuoni sasa tuna kiu nayo.

Kwani wewe unaona tabu kuihadithia?''

View attachment 1960744
Dini yako imekataza kutukuza na kuwamwagia sifa binadamu na wanaume wenziyo kwa namna unavyofanya wewe.
 
Dini yako imekataza kutukuza na kuwamwagia sifa binadamu na wanaume wenziyo kwa namna unavyofanya wewe.
Schmidt,
Mwalimu wangu Sheikh Haruna Allah amrehemu alinifundisha mlango wa mnakasha yaani majadiliano.

Akiniambia, "Ukiona mtu anatukana katika mjadala jua hana la kusema kaishiwa.
Mwenye hoja tusi halipenyi katika fikra zake.

Akifikia hapo jitoe katika mjadala hadi atakapotulia.
Usijibu matusi.

Ukienda kinyume na haya nikufundishayo utanitukanisha mie mwalimu wako kwani watu watauliza umesoma wapi?"

Sasa umekuja kwa adabu basi na tufanye mjadala wa heshima.
Huko kwenye Uislam wala usiguse.

Hao unaowaita "wanaume wenzangu," mimi ni baba zangu.
Kwao mimi ni mtoto.

Nimeishi nao utotoni hadi nimekuwa mzee sasa na baadhi yao nimewazika na kuwaandikia taazia.

Wala sijaandika lile ambalo wazee wangu hawa hawakufanya.

Yote niliyoandika kwenye kitabu cha Abdul Sykes na ninayoandika hapa waliofanyiwa na walioshuhudia yakifanywa katika kupigania uhuru wa Tanganyika wako hai.

Aliye na shaka ana nafasi bado ya kuwauliza.
 
Schmidt,
Mwalimu wangu Sheikh Haruna Allah amrehemu alinifundisha mlango wa mnakasha yaani majadiliano.

Akiniambia, "Ukiona mtu anatukana katika mjadala jua hana la kusema kaishiwa.

Mwenye hoja tusi halipenyi katika fikra zake.

Akifikia hapo jitoe katika mjadala hadi atakapotulia.

Usijibu matusi.

Ukienda kinyume na haya nikufundishayo utanitukanisha mie mwalimu wako kwani watu watauliza umesoma wapi?"

Sasa umekuja kwa adabu basi na tufanye mjadala wa heshima.

Huko kwenye Uislam wala usiguse.

Hao unaiwaita "wanaume wenzangu," mimi ni baba zangu.

Kwao mimi ni mtoto.

Nimeishi nao utotoni hadi nimekuwa mzee sasa na baadhi yao nimewazika na kuwaandikia taazia.

Wala sijaandika lile ambalo wazee wangu hawa hawakufanya.

Yote niliyoandika kwenye kitabu cha Abdul Sykes na ninayoandika hapa waliofanyiwa na walioshuhudia yakifanywa katika kupigania uhuru wa Tanganyika wako hai.

Aliye na shaka ana nafasi bado ya kuwauliza.
Unakufuru kil siku Mzee, mtukuze Mtume wako siyo Sykes. Wewe ahera hutaiona kwa matendo yako. Allah anahesabau mara ngapi umelitaja jina la Mtume wake, na mara ngapi umerudia jina la Sykes.
 
Unakufuru kil siku Mzee, mtukuze Mtume wako siyo Sykes. Wewe ahera hutaiona kwa matendo yako. Allah anahesabau mara ngapi umelitaja jina la Mtume wake, na mara ngapi umerudia jina la Sykes.
Schmidt,
Nilifahamu muda mrefu kuwa hutofika mbali na mimi.
 
Back
Top Bottom