Hamuwezi amini leo nimekojoa jiwe

Hamuwezi amini leo nimekojoa jiwe

mtanzania asiye jielewa

Senior Member
Joined
Nov 13, 2016
Posts
179
Reaction score
98
Ndugu zangu nilikuwa nasumbuliwa na tatizo la mkojo kutoka kidogo kidogo yaani kila nikienda chooni mkojo hauishi. Nikaenda hospitali ya rufaa nikapimwa wakanikuta nina UTI sugu, nikaandikiwa sindano saba lakini tatizo halijaaisha kila dakika ni kwenda chooni mkojo unatoka kidogo unakata mpaka imefikia hatua nimekata tamaa.

Sasa leo nikiwa nimechoka huku maumivu yakizidi pale unapoanzia uume ikabidi nijishike kwa kupangandamiza ndipo nilisikia kitu kimenikata kwa ndani nikashtuka sana hapo hapo mkojo ukanibana nikakimbia kwenda chooni sijui kipi kimenituma nikojoe nje ya sink la chooni. Wakati mkojo unatoka kwa kasi na mimi nikijikamua NILISIKIA KITU KIMETOKA KWENYE UUME WANGU ndipo nikainama nikalisafisha na kuliokota kuangalia kwa makini ni mawe kama matatu yameeungana ndipo nikalipeleka hospitalini (maabara) mtu wa maabara alishangaa sana akaenda kuliangalia aliporudi aliniiuliza je hukutoka damu? Nikamjibu hapana wakaniomba nipeleke mkojo.

Kwa hiyo kesho ndo nitaenda kuchukua mjibu kamili.

Swali langu kwenu wataalamu, ni kwanini hali hii imenipata?

NAOMBENI MAJIBU NDUGU ZANGU
 
Urinary track infection
Ni mawe yanayotoka kwenye kibofu
Ambapo ulikuwa hujatibiwa kwa muda mrefu, mwisho huwa yanafuata mkojo
Huwa watu wanakojoa mawe na kupona kwa tatizo la kuumia na kuto toka mkojo kawaida
 
Urinary track infection
Ni mawe yanayotoka kwenye kibofu
Ambapo ulikuwa hujatibiwa kwa muda mrefu, mwisho huwa yanafuata mkojo
Huwa watu wanakojoa mawe na kupona kwa tatizo la kuumia na kuto toka mkojo kawaida
track???? are you sure
 
Professionally
Hiyo hali huwatokea wale wasiokunywa maji na hukaa na mkojo bila kuukojoa, hivo madini yapatikanayo ndani ya mkojo husababisha mkojo huo kuganda(yaani kutengeneza mawe)
 
Back
Top Bottom