Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 144
salim said salim, zanzibar
NI kawaida katika nchi nyingi kusikia taasisi za ndani na nje zinafanya utafiti wa masuala ya siasa, uchumi, utamaduni, michezo na burdani na kutoa matokeo.
Zanzibar imeshuhudia taasisi za nje ya visiwa hivi hasa ya REDET iliyopo Dar es Salaam zikitoa matokeo ya tafiti zao ambazo watu huzishitukia tu.
Lini tafiti hizo zilifanywa, nani alizifanya, wapi utafiti ulifanyika na vigezo viliotumika huwa hayawekwi wazi.
Vile vile, REDET huleta Zanzibar wale inaowaita wataalamu wa masuala ya demokrasia ambao hutoa elimu ya demokrasia wakati hawaelewi undani wa siasa za Zanzibar, zilizogubikwa na uongo, unafiki, uzandiki, chuki na ubaguzi.
Karibu taarifa zote za REDET, hasa uchaguzi mkuu unapokaribia, huonyesha CCM ni nambari wani na kuwa na muelekeo wa kupata ushindi. Hata wakati mmoja Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) haijawahi kulalamikia ripoti za REDET, labda kwa sababu ripoti zake zote huzipigia debe.
Ninakumbuka wakati wa kuelekea uchaguzi mdogo kisiwani Pemba mwaka 2001, taasisi moja ilisema mchuano ungekuwa mkali. SMZ haikulalamika kwamba utafiti ule ulikuwa si wa kitaalamu na haukuonyesha hali halisi iliokuwepo wakati ule.
Uchaguzi ulifanyika na CCM ilipata chini ya asilimia 12 katika majimbo yote isipokuwa Mkanyageni. Sijui wataalamu wale wa utafiti waliotoa kauli ya kutegemea ushindani mkali katika uchaguzi ule walipata wapi dalili za kuwepo hali ile.
Hivi karibuni taasisi moja ijuliknayo kama Steadman ilisema utafiti wake juu ya mbio za urais wa Zanzibar mwaka 2010 unaonyesha katika orodha ya wanaotajwa kutaka kugombea anayeongoza ni Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye alitajwa kuwapiku wale wa CCM.
Sijui vipi Steadman ilifikia hitimisho hili wala sielewi njia ilizotumia kuendesha huo utafiti au lengo la kufanya hivyo. Sikua na taarifa ya kufanyika utafiti huo, licha ya udogo wa Zanzibar, kama REDET walipofanya (kama walifanya) utafiti wa aina hii siku za nyuma.
Kinachonishangaza ni kuwa SMZ haikulalamikia matokeo ya tafiti za REDET kwa vile yaliisafishia njia kwa CCM. Wapinzani walidai REDET ilikuwa inajenga mazingira ya kuhalalisha wizi wa kura katika chaguzi ziliopita. Ukweli au uongo wa madai hayani suala linalohitaji utafiti usiokuwa na utashi wa kisiasa.
Tunaambiwa kitendo cha Steadman si cha kiungwana kwa vile kibali ilichopewa na SMZ si cha kushughulikia mambo ya siasa. Waziri wa Nchi katika Afisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, alieleza kuwa kilichofanywa na Steadman ni utapeli.
Hapa pamejitokeza hisia kuwa ni taasisi za kiungwana kama za REDET tu ndiyo zenye haki ya kufanya tafiti juu ya chaguzi za Zanzibar kwa vile ni safi na watafiti wake ni waungwana. Wengine huwa hawana nia njema na Zanzibar.
Waziri Hamza alisema hata Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Juma Duni Haji, huenda angetaka kuwa mgombea, lakini Steadman haikumjumuisha katika orodha ya wanaosemekana wanataka kugombea Urais. Labda hapa waziri angelisema haelewi kwa nini na yeye hajaingizwa katika orodha hiyo kama alivyotaka aingizwe Duni.
Lakini la kujiuliza hapa ni je kwa waziri Hamza kumsemea Duni juu ya mbio za kuelekea urais wa Zanzibar na kumfikilia anataka kugombea wakati mwenyewe hajawahi kusema hivyo ni uungwana? Au uungwana hutarajia kitoka upane mmoja tu?
Ni vizuri kwa viongozi wa SMZ kuwa na uvumilivu na si kutaka kila taasisi itoe matokeo yatakayowafurahisha. Hii ndiyo dunia ya leo huyu anasema hili na yule anasema lile. SMZ pia haikupaswa kulalamikia kauli ya nchi za Umoja wa Ulaya (EU) na nchi nyingine za Ulaya na Marekani, juu ya kutofurahishwa na namna zoezi la uandikishaji wapiga kura linavyoendeshwa kisiwani Pemba.
Kwanza tukumbuke kuwa ni nchi hizi ndio zinazotusaidia kufanya huo uchaguzi na kwa hivyo zina haki ya kutaka kuuona ni huru na wa haki na sio fedha zao kutumika kukandamiza demokrasia.
Kama kweli Tanzania, na hasa Zanzibar, inahisi hakuna anayeweza kuinyooshea kidole basi Tanzania nayo isingelinyooshea kidole nchi nyingine wala kupeleka majeshi yake Comoro, Darfur, Sudan na nchi nyingine. Au tunataka tuamini kuwa nchi hizi ni sehemu ya Tanzanika na kwa hivyo tulikuwa hatuingilii mambo ya nchi nyingine?
Vile vile tujiulize kwa nini waliofanya mauaji ya haliki Rwanda wanashitakiwa Arusha? Je, kwa mtazamo wa kila mtu ashughulikie nchi yake si kuingilia mamo ya ndani ya Wanyarwanda?
Ni vizuri tukaanza kuyaangalia mambo kwa sura moja au mbili, lakini zaidi ya hizo. Wakati tukifurahia wanaotupigia debe na kutusifu tusinune wanapotokea wale wanaofanya kinyume na hayo. Tuwe wavumilivu, iwe tunapokosolewa au hata kuwekwa hadharani mambo ambayo hatupendi yawe wazi.
Vile vile tusiwe mahodari kuwaita wachochezi wale wanaotaka watu wajiandikishe kupiga na kuwasifia kama malaika, masheha wanaowanyima watu haki hio au watu wanaopiga watu mapanga na nondo kwenye vituo vya uchaguzi. Tusisahau kuwa pakiwa na wanaokupenda pia wapo wanaokuchukia, iwe kwa sababu za msingi au kwa chuki zao binafsi. Dunia ya sasa si rahisi kuibadili ili ikuridhie unavyotaka wewe kila wakati na kwa kila jambo.
SOURCE: TANZANIA DAIMA.
NI kawaida katika nchi nyingi kusikia taasisi za ndani na nje zinafanya utafiti wa masuala ya siasa, uchumi, utamaduni, michezo na burdani na kutoa matokeo.
Zanzibar imeshuhudia taasisi za nje ya visiwa hivi hasa ya REDET iliyopo Dar es Salaam zikitoa matokeo ya tafiti zao ambazo watu huzishitukia tu.
Lini tafiti hizo zilifanywa, nani alizifanya, wapi utafiti ulifanyika na vigezo viliotumika huwa hayawekwi wazi.
Vile vile, REDET huleta Zanzibar wale inaowaita wataalamu wa masuala ya demokrasia ambao hutoa elimu ya demokrasia wakati hawaelewi undani wa siasa za Zanzibar, zilizogubikwa na uongo, unafiki, uzandiki, chuki na ubaguzi.
Karibu taarifa zote za REDET, hasa uchaguzi mkuu unapokaribia, huonyesha CCM ni nambari wani na kuwa na muelekeo wa kupata ushindi. Hata wakati mmoja Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) haijawahi kulalamikia ripoti za REDET, labda kwa sababu ripoti zake zote huzipigia debe.
Ninakumbuka wakati wa kuelekea uchaguzi mdogo kisiwani Pemba mwaka 2001, taasisi moja ilisema mchuano ungekuwa mkali. SMZ haikulalamika kwamba utafiti ule ulikuwa si wa kitaalamu na haukuonyesha hali halisi iliokuwepo wakati ule.
Uchaguzi ulifanyika na CCM ilipata chini ya asilimia 12 katika majimbo yote isipokuwa Mkanyageni. Sijui wataalamu wale wa utafiti waliotoa kauli ya kutegemea ushindani mkali katika uchaguzi ule walipata wapi dalili za kuwepo hali ile.
Hivi karibuni taasisi moja ijuliknayo kama Steadman ilisema utafiti wake juu ya mbio za urais wa Zanzibar mwaka 2010 unaonyesha katika orodha ya wanaotajwa kutaka kugombea anayeongoza ni Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye alitajwa kuwapiku wale wa CCM.
Sijui vipi Steadman ilifikia hitimisho hili wala sielewi njia ilizotumia kuendesha huo utafiti au lengo la kufanya hivyo. Sikua na taarifa ya kufanyika utafiti huo, licha ya udogo wa Zanzibar, kama REDET walipofanya (kama walifanya) utafiti wa aina hii siku za nyuma.
Kinachonishangaza ni kuwa SMZ haikulalamikia matokeo ya tafiti za REDET kwa vile yaliisafishia njia kwa CCM. Wapinzani walidai REDET ilikuwa inajenga mazingira ya kuhalalisha wizi wa kura katika chaguzi ziliopita. Ukweli au uongo wa madai hayani suala linalohitaji utafiti usiokuwa na utashi wa kisiasa.
Tunaambiwa kitendo cha Steadman si cha kiungwana kwa vile kibali ilichopewa na SMZ si cha kushughulikia mambo ya siasa. Waziri wa Nchi katika Afisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, alieleza kuwa kilichofanywa na Steadman ni utapeli.
Hapa pamejitokeza hisia kuwa ni taasisi za kiungwana kama za REDET tu ndiyo zenye haki ya kufanya tafiti juu ya chaguzi za Zanzibar kwa vile ni safi na watafiti wake ni waungwana. Wengine huwa hawana nia njema na Zanzibar.
Waziri Hamza alisema hata Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Juma Duni Haji, huenda angetaka kuwa mgombea, lakini Steadman haikumjumuisha katika orodha ya wanaosemekana wanataka kugombea Urais. Labda hapa waziri angelisema haelewi kwa nini na yeye hajaingizwa katika orodha hiyo kama alivyotaka aingizwe Duni.
Lakini la kujiuliza hapa ni je kwa waziri Hamza kumsemea Duni juu ya mbio za kuelekea urais wa Zanzibar na kumfikilia anataka kugombea wakati mwenyewe hajawahi kusema hivyo ni uungwana? Au uungwana hutarajia kitoka upane mmoja tu?
Ni vizuri kwa viongozi wa SMZ kuwa na uvumilivu na si kutaka kila taasisi itoe matokeo yatakayowafurahisha. Hii ndiyo dunia ya leo huyu anasema hili na yule anasema lile. SMZ pia haikupaswa kulalamikia kauli ya nchi za Umoja wa Ulaya (EU) na nchi nyingine za Ulaya na Marekani, juu ya kutofurahishwa na namna zoezi la uandikishaji wapiga kura linavyoendeshwa kisiwani Pemba.
Kwanza tukumbuke kuwa ni nchi hizi ndio zinazotusaidia kufanya huo uchaguzi na kwa hivyo zina haki ya kutaka kuuona ni huru na wa haki na sio fedha zao kutumika kukandamiza demokrasia.
Kama kweli Tanzania, na hasa Zanzibar, inahisi hakuna anayeweza kuinyooshea kidole basi Tanzania nayo isingelinyooshea kidole nchi nyingine wala kupeleka majeshi yake Comoro, Darfur, Sudan na nchi nyingine. Au tunataka tuamini kuwa nchi hizi ni sehemu ya Tanzanika na kwa hivyo tulikuwa hatuingilii mambo ya nchi nyingine?
Vile vile tujiulize kwa nini waliofanya mauaji ya haliki Rwanda wanashitakiwa Arusha? Je, kwa mtazamo wa kila mtu ashughulikie nchi yake si kuingilia mamo ya ndani ya Wanyarwanda?
Ni vizuri tukaanza kuyaangalia mambo kwa sura moja au mbili, lakini zaidi ya hizo. Wakati tukifurahia wanaotupigia debe na kutusifu tusinune wanapotokea wale wanaofanya kinyume na hayo. Tuwe wavumilivu, iwe tunapokosolewa au hata kuwekwa hadharani mambo ambayo hatupendi yawe wazi.
Vile vile tusiwe mahodari kuwaita wachochezi wale wanaotaka watu wajiandikishe kupiga na kuwasifia kama malaika, masheha wanaowanyima watu haki hio au watu wanaopiga watu mapanga na nondo kwenye vituo vya uchaguzi. Tusisahau kuwa pakiwa na wanaokupenda pia wapo wanaokuchukia, iwe kwa sababu za msingi au kwa chuki zao binafsi. Dunia ya sasa si rahisi kuibadili ili ikuridhie unavyotaka wewe kila wakati na kwa kila jambo.
SOURCE: TANZANIA DAIMA.
Last edited: