Jospina
JF-Expert Member
- Apr 19, 2013
- 2,421
- 1,395
-Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya klabu ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe ameachiwa kwa dhamana ya Sh. Milioni 15 baada ya kusomewa mashitaka mawili katika Mahakama ya Kisutu mjini Dar es Salaam leo akiunganishwa kwenye kesi inayowakabili rais wa klabu hiyo Evans Aveva na Godfrey Nyange 'Kaburu'. Kaburu na Aveva wataendelea kusota rumande kwa sababu makosa yao hayana dhamana.