Shujaa Mwendazake
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 4,016
- 6,759
Leo wakati wa hotuba yake baada ya kuapisha mabalozi Mh Rais alijaribu kuhusiana na kupanda kwa bei ya mbolea nchini , jambo ambalo linaonekana wazi kuwa litaleta athari sana katika suala letu la chakula hapo mwakani. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa kupanda kwa bei ya mbolea nchini kumetokana na uzalishaji mdogo wa bidhaa hiyo katika viwanda vya nje ya nchi kufuatia kufungwa na kupunguza uzalishaji baada ya ugonjwa wa Corona.
Lakini hapo nyuma tuliona jinsi aliyekuwa Mbunge wa Mbozi Pascal Haonga akituambia kuwa Serikali imepandisha Kodi ya Mbolea na kupelekea Malalamiko kadhaa zikiwemo threads zilizoshushwa humu Jamvini.
Mheshimiwa Haonga alisema:
"Serikali ya C.C.M itaua kilimo,imepandisha kodi ya pembejeo za kilimo ili kukomoa wakulima mbolea ya kupandia mazao aina ya DAP imeongezeka bei kutoka 52,000= hadi 92,000/=.Mbolea za kukuzia Mf.UREA kutoka 48,000/=na sasa ni 80,000/= na CAN kutoka 40,000-60,000/=."
Kama hilo si sahihi Mh.Haonga alipaswa akanushe hilo na aombe radhi kwa upotoshaji huu unaoweza kuleta chuki kwa wananchi hususan wakulima kwa serikali yao. Hili inaonekana alizusha mno na kwa nafasi yake kama mtunga Sheria aliyepita alikuwa na uwezo wa kureserch na kuthibitisha hiyo taarifa yake kwanza kabla ya kuisambaza. Haonga alikwenda mbali zaidi na kuweka hili neno "ILI KUKOMOA WAKULIMA"
www.jamiiforums.com
www.jamiiforums.com
www.2eyezmedia.com
Lakini hapo nyuma tuliona jinsi aliyekuwa Mbunge wa Mbozi Pascal Haonga akituambia kuwa Serikali imepandisha Kodi ya Mbolea na kupelekea Malalamiko kadhaa zikiwemo threads zilizoshushwa humu Jamvini.
Mheshimiwa Haonga alisema:
"Serikali ya C.C.M itaua kilimo,imepandisha kodi ya pembejeo za kilimo ili kukomoa wakulima mbolea ya kupandia mazao aina ya DAP imeongezeka bei kutoka 52,000= hadi 92,000/=.Mbolea za kukuzia Mf.UREA kutoka 48,000/=na sasa ni 80,000/= na CAN kutoka 40,000-60,000/=."
Kama hilo si sahihi Mh.Haonga alipaswa akanushe hilo na aombe radhi kwa upotoshaji huu unaoweza kuleta chuki kwa wananchi hususan wakulima kwa serikali yao. Hili inaonekana alizusha mno na kwa nafasi yake kama mtunga Sheria aliyepita alikuwa na uwezo wa kureserch na kuthibitisha hiyo taarifa yake kwanza kabla ya kuisambaza. Haonga alikwenda mbali zaidi na kuweka hili neno "ILI KUKOMOA WAKULIMA"
Rais Samia kweli umedhamiria kukusanya Kodi za dhuluma hadi kwenye mbolea?
Haya yote yanayoendelea nadhani tunayaona na hii itoshe kusema CCM hawana nia tena na kuongoza nchi. Mmeongeza Kodi sawa, ndio iwe mara mbili? Ongezeko la 100% tena kwa kipindi hiki? HAPANA Mama hii ni Kodi ya dhulma, haikubaliki. Watanzania wengi wamejiajiri kwenye kilimo lakini napo umeamua...
Baada ya makato ya simu sasa ni bei ya Mbolea
Wakati wananchi wakipaza sauti kulalamikia tozo za miamala ya simu ambayo imeonekana kua mzigo na maumivu kwa wananchi sasa bei ya mbolea imeenda kupaa isivyo kawaida hivyo kuketa taharuki wa wakulima. Kilimo ndo uti wa Mgongo wa taifa ambapo zaidi ya 70% ya wananchi wanajishughulisha na...
Waziri Mkenda: kuongezeka kwa bei ya mbolea hakuhusishi tozo za serikali kwa kuwa mbolea haitozwi kodi - 2 Eyez Media
Waziri wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda amesema kuwa kuongezeka kwa bei ya mbolea nchini hakuhusishi tozo za serikali kwakuwa mbolea haitozwi kodi. Ameyasema hayo jana alipofanya ziara bandarini kuangalia kasi ya ushushwaji wa mbolea, ambapo amesema serikali inafuatilia kwa ukaribu bei yake...
www.2eyezmedia.com