Hapa lazima ukimbie

Daviie

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2016
Posts
1,294
Reaction score
1,480
Nilikutana na mshikaji wangu Tandika stendi ya Mbagala, akanishtua kwa nyuma akisema "Malogymathematic ndio wewe!? upo kaka?" Nikamjibu nipo kiongozi tunasindikiza wenye maisha yao akacheka sana,

Mara akaanza kuzungumzia matatizo ya familia yake, nikamwambia tuyaachehayo mimi mwenzako nimepitia makubwa,
aling'ang'nia kuzungumzia kero za familia yake,

Nikamzuia nikamwambia " Unadhanifamilia yako ina matatizo?" Basi sikiliza kisachangu hiki…."Miaka kadhaa iliyopita nilikutana namwanamke mjane aliyekua na binti mkubwa tu,mimi na huyo mjane tukaamua kuoana.

Baadayebaba yangu ambae alikuwa mkiwa baada yakufiwa na mama kitambo tu akaamua kumuoabinti yangu wa kambo (yaani binti wa huyu mke wangu niliyemwoa akiwa mjane), hivyo huyo binti yangu wa kambo akawa mama yangu wa kambona Baba yangu akawa mtoto wangu wa kambo wakiume ambapo mke wangu akawa mama mkwe wake

Baadaye binti ya mke wangu yaani binti yangu wakambo (ambaye kwa sasa ndiye mke wa babayangu na hivyo kuwapia mama yangu wa kambo)alipata mtoto wa kiume.

Mtoto huyo wa kiumeakawa mdogo wangu kwa sababu tulichangia baba mmoja, lakini kwa vile pia alikua ni mtoto
wa binti wa mke wangu papo hapo akawa mjukuu wa mke wangu na mimi nikawa babu yake huyomdogo wangu.

Lakini hayo yote yalikua si kitu mpaka mimi na mke wangu tulipopata mtoto wa kiume. Sasamsichana (yaani binti ya mke wangu ambaye piani mke wa baba yangu) ambaye ni ndugu wamtoto wangu huyo wa kiume kwa kuchangiamama yao mmoja, akawa pia bibi yake namwanangu (mwee!!).

Hali hiyo ilimfanya pia babayangu kuwa shemeji wa mtoto wangu (achiliakuwa babu yake!!) ambaye ndugu yake wa kike kwa upande wa mama yao ndie mke wake baba yangu. Kwa hiyo mimi ni shemeji yake mamayangu wa kambo ambapo mke wangu ni mamamdogo (anti) wa binti yake mwenyewe .

Mtoto wangu wa kiume ni mpwa wa baba yangu ambapo mimi nikawa babu yangu mwenyewe.Kabla sijammalizia jamaa akaondoka Mimi sio mtu wa mchezomchezo

*Sipendagi Ujinga*
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mmmmh!Mkuu unaposema mtumishi halali maana yake kuna haramu.Nijuavyo Mungu haonekani kwa macho wala kusikika kwa masikio labda kwenye vitabu vinavyo dhaniwa narudia vinavyo dhaniwa kuwa ni vyake sasa,ithibati ya huyu halali na huyu haramu anatoa nani?na kwa vigezo vipi?Tusaidie mkuu tujifunze
yap ameokoka na sasa ni mtumishi halali wa Mungu
 
Hapa apply ule usemi unaosema " wengi wape" . Kama ambavyo watu wengi hasa watanzania wanaamini kuna Mungu, lakini ukiangalia aliyoyafanya Nabii Tito ikaonekana amepotoka tofauti na mtazamo wa wengi basi alihesabika kama mtumishi haramu. Baada ya kudai ameokoka na anasali katika makanisa ambayo wamezoea wengi basi inaonekana huko ndo kwa Mungu halali. Japo kwa watu wenye free minds kama wewe ndo mtasema hakuna halali wala haramu but kidunia ipo hivyo sie kuna namna tunaona sawa na si sawa kwa mazoea na mitazamo yetu
 
Hapo nimekusoma mkuu.Kumbe tunataka Mungu tuliyemuumba kwa mawazo yetu wenyewe yale yaliyo kinyume na uelewa wetu tukayaita haramu.Nimekuelewa sana mkuu
 
Nimewaza huo mlolongo wa ukoo hadi kichwa kinauma[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tatizo ni pale kijana wako akioa hebu fafanua mkewe atamwitaje mdogo wako?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…