Hapa mkuu Lifecode alikuwa anamaanisha nini?

Twende taratibu huenda tukaelewana vizuri!

1. Kiumbe ni nini? Unamaanisha kiumbe hai au kisicho hai?

2. Je, mimea ni sehemu ya viumbe? Hakuna mimea imetengenezwa maabara leo? Namaanisha mimea kama michungwa, papai, mbegu za mahindi nk. Hapa tuwaulize watu wa maabara ya SUA huenda wakatusaidia

3. Huwa nasikia watu wanasema kuna wanyama na jamii ya ndege wa kisasa! Mfano, nasikia kuna kuku wa kisasa ambao ni tofauti kabisa na kuku wa kule kijijini kwetu! Hali kadhalika naskia kuna ng'ombe wa kisasa, mbuzi na wanyama wengine! Hawa wametokea wapi? Maana naskia sikia chanzo chake ni maabara za kisayansi! Watu wa SUA watusaidie tena hapa

4. Watu wa Taasisi ya Afya Ifakara pia watusaidie hapa, hivi mbu ni kiumbe au sio kiumbe!? Na kama ni kiumbe, hivi haijawahi kutokea wataalamu wa maabara kuzalisha mbu kwa lengo la kutokomeza hawa mbu aina ya "anofrensi" wanaotuletea malaria? Au ni habari za uzushi hizi maana mwenzetu unatwambia hakuna mwenye uwezo wa kutengeneza kiumbe

Labda nimemezeshwa taarifa za vijiweni, hebu nitoe tongotongo kwa haya nayoyasikia sikia ili niongeze ufahamu na Mimi

Na jambo jingine ni hili nalotaka Msaada wa ufahamu toka kwako:-

1. Kwa kuwa hakuna aliyebuni namba kwa maana zilikuwepo, yaani binadamu wamezipa majina tu, Je, hakuna uwezekano binadamu hao waliozipa majina namba kuzitumia namba hizo hizo kwa namna watakavyo wao kwa lengo la kuwasiliana wao kwa wao na kuficha taarifa hizo kwa watu wengine!?

2. Pili, umesema hakuna aliyeanzisha elimu bali wapo walioweka kanuni zao kwenye hiyo elimu.

Swali ni Je, hakuna uwezekano katika kanuni hizo unazodai wameweka ndio code zenyewe za walichokilenga!? Yaani walificha taarifa fulani kwa kundi fulani katika kanuni hizo?

Hapa najaribu kwenda na wewe taratibu huenda nikakuelewa au wewe ukaelewa wanachojadili wadau humu



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo maana iko wapi? Naomba unisaidie kuquote mkuu kama hutojali

Asante kwa masahihisho ya kiuandishi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nachojua mmea au Mnyama wa kisasa ni Copy iliyotokana na mnyama halisi so kwa upande wangu kusema kuwa kuna maabara zinazotengeneza mimea au wanyama sio sahihi labda ungesema kuna maabara zinazofanya mabadiliko ya hivyo vitu ingemake sense zaidi unless kama kuna mmea au Mnyama unayemjua ambapo hapo awali hakikuwepo unaweza ukawa na rights za kusema hicho kimetengenezwa maabara.
 
Nashukuru sana kwa masahihisho haya, nadhani mantiki iko pale pale kwamba kuna kitu kinafanana na kuku wa asili wanasayansi walikizalisha kwa kutengeneza mafomula na kuchanganya makemikali wanayoyajua wao maabara na Sasa kinatumika kama kitoweo mtaani!

Sidhani kama bado nimekosea, ni matumizi ya lugha tu! Turudi kwenye mada sasa inayobishaniwa na mdau hapo juu! Ikiwa wanasayansi wameweza ku "copy" hao viumbe, je bado haiwezekani kwao kuzalisha viumbe wanaofanana na virus? (au tuseme ku copy virus) kwa matumizi wanayoyakusudia wao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hujajibu swali langu la msingi! Unaamini kuna watu wanaweza kutumia mapembe, michoro, namba au alama fulani kufikisha taarifa fulani kwa kutaka kundi la watu wengine wasielewe wanachokusudia?
Hili ni swali jipya si miongoni mwa maswali ambayo umeuliza. Swali hili linakinzana na swali lako ulilo uliza, kwanza linaonyesha umekiri ya kuwa mapembe na hizo namba wamezikuta. Lakini swali hili limejibiwa katika maelezo yangu huko nyuma kama ulikuwa makini,nilisema ya kuwa watu wanacho fanya wao ni kutoa majina na kuweka maana zao kisha wanaziita ni siri, wakati kiuhalisia ni kinyume chake. Kwani kujua kwake au kutokujua kwake hizo maana ni sawa, na hakuna athari yoyote. Kwani hakuna uhusiano kati ya hizo maana na mapembe au mfano wake kwa lolote.

Sasa jitahidi kusoma vizuri ninacho kiandika ili uepushe kupoteza muda kuulizwa maswali ambayo nimeshayajibu tayari.
Katika sehemu zote ulizojaribu kuni qoute kwa kutaka kujibu nilichokuuliza naona unaruka ruka tu! Sijui, labda wengine watanisaidia kama wanakuelewa!
Poa.
 
Tunakubaliana kwamba hawawezi kuyaumba, Yes! Swali ni Je, hawawezi kuyatumia kuficha siri zao kwa watu wengine!? Yaani kutoweza kuyaumba kunawazuia wao kuyatumia kufikishiana taarifa kwa namna wanavyotaka wao!?

Sent using Jamii Forums mobile app

Tatizo sio kuficha siri, tatizi ni kufungamanisha siri hizi na jambo husika, hii ni aina ya shirki,ndio maana ukiangalia kwa undani Sayansi hii inayoelezwa na huyu ni aina au inapelekea katika USHIRIKINA.
 
1. Kiumbe ni nini? Unamaanisha kiumbe hai au kisicho hai?

Kiumbe ni kile ambacho hakijatengenezwa na kiumbe. Sijui kama kuna ambacho sio, hai kama kipo nithibitishie, na uniambie imunajuaje kiumbe kisicho kuwa na uhai.
2. Je, mimea ni sehemu ya viumbe? Hakuna mimea imetengenezwa maabara leo? Namaanisha mimea kama michungwa, papai, mbegu za mahindi nk. Hapa tuwaulize watu wa maabara ya SUA huenda wakatusaidia

Mimea ni viumbe.

Wewe waulize walitumia nini na mpaka ikawa hiyo mimea, sababu haikuwepo hapo kabla.

Sasa usipende kusikia na story, lazima uhoji. Hii kazi utaifanya kwa muda wako. Kisha uwaulize uhai wa huo viumbe wamepata, na kisha kwanini kinapo kufa wanashindwa kurudisha uhai hali ya kuwa waliweza kukiumba (Hii kama unavyosikia).

Huu ni muendelezo wa kusikia, sasa usipende kusikia bali, uwe una hoji. Walitumia malighafi gani kuwazalisha au kuwatengeneza. Maana kilugha kisicho hai ndio hutengenezwa.
Labda nimemezeshwa taarifa za vijiweni, hebu nitoe tongotongo kwa haya nayoyasikia sikia ili niongeze ufahamu na Mimi

Nimekusaidia kwa kukupa maswali ya msingi juu ya nukta zako 4 hapo juu, kisha kwa muda wako watafute watu wa mimea wakujibu.

Naendelea ...
 

1. Swali hili umerudia kuliuliza, na hii inaonyesha kwanini hauko makini,ila kwa kukusaidia nalijibu tena, niliposema watu wanazipa maana ujue kabisa najua hilo, ila nachokataa mii ni kufungamanisha maana hizo na namba hizo na si vingenevyo. Nakupa mfano, katika Falsafa za Pythagoras yeye alitumia namba kuwasilisha mawazo yake na kuelezea maana ya maisha, akasema namba kumi ni "Ukamilifu" swali nji upi uhusiano kati ya ukamilifu na namba kumi? Je bila namba kumi ukamilifu haupo ? Kama jibu nji kinyume chake hakuna maana ya kusema namba 10 ni ukamilifu. Kwahiyo haya yanabaki kuwa ni mawazo yao katika kuwasilisha mitazamo yqo ila hakuna uhusiano wowote kati ya viwili hivyo na hii iko hivyo mpaka katika hayo mengine.

2. Swali hili rahisi sana, kama ungekuwa unafikiri mambo kwa kina usingeuliza. Nakuoa mfano wa kanuni fulani katika Elimu ya Sheria kisha namalizia kanuni ya Fizikia katika "Newton's Law of Universal Gravitation".

Katika Sheria kuna kanuni inasema hivi "Hakika juu ya jambo fulani huwa haiondolewi na shaka juu ya jambo hilo". Kwa kanuni kipi kinaweza kufichwa hali ya kuwa marejeo yapo na uhalisia upo ?

"Newton's law of universal gravitation is usually stated that every particle attracts every other particle in the universe with a force which is directly proportional to the product of their masses and inversely proportional to the square of the distance between their centers."

Katika kanuni hiyo kuna code gani zitakaa, juu ya jambo ambalo halina ushahidi wa Kisayansi zaidi ya kanuni za kimahesabu jambo ambalo halina ithibati nje ya makaratasi ? Utapataje kivuli kilicho nyooka katika mti ulio pinda ?

Sasa walitakiwa wajue ukweli wa nadharia kisha wajue ya kuwa hakuna nadharia inayoweza kuonyesha ukweli wa nadharia nyingine, kwani kila nadharia huweza kuwa vinginevyo.

Ahsante.
 
Zurri:mpaka hapa sijaona ulicho tuongezea,zaidi ya kubaki na sifa hizi.1.unauliza swali kwa swali na unapata majibu ya swali Kwenye swali uliloulizwa.2,ukichanganya mambo ya kisanyasi na uumbaji wa mungu lazima mtofautiane.3,hakuna ambae hajui kwamba wakwanza kuumba ni mungu na anaye kuja kusema amegundua kitu frani walio ktk tasnia ya sayansi atapewa sifa kwani imegundulika njia rahisi ya kurahisisha kazi frani,ila aliye ktk imani hawezi kumuelewa huyo mgunduzi.hivyo hizi njia ata ukitaka kumvuruga mtu yoyote utamvuruga tu.Embu tuache tuendelee mzee baba,habari za mtu anakusalimia shikamoo una muhoji unajua maana ya shikamoo au aliye anzisha hatuata fika plz

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwa maelezo yako ya awali, ulionekana umebase kwenye sayans zaid ndio maana hata dark energy unataka kupata scientific prove ila nashangaa tena unakuja na swala la roho kwamba swala la kuumba ni beyond ya mwanadamu Kwan hawez kuumba roho. Kisayansi Kuna roho? Je kisayansi wanyama Wana roho? Naomba uthibitisho
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo sio kuficha siri, tatizi ni kufungamanisha siri hizi na jambo husika, hii ni aina ya shirki,ndio maana ukiangalia kwa undani Sayansi hii inayoelezwa na huyu ni aina au inapelekea katika USHIRIKINA.
Lengo langu limetimia, sina haja ya kuendelea na wewe tena! Nilitaka ujifunue wazi kwamba mlengo wako ni upi!

Hadi hapa umeshajiweka wazi tayari kwa kuhusianisha sayansi na ushirikina! Kwa mtu anayekusoma kwa umakini hapati taabu tena kukufahamu wewe ni mtu wa aina gani

Nikushauri tu kwamba, ukikuta watu wanajadili jambo usikimbilie kuweka misimamo yako kwa kisingizio cha kuhoji! Kuna tofauti kubwa sana ya kuhoji na kuweka misimamo binafsi!

Unapokuta watu wanajadili jambo, kuwa tayari kujifunza with open mind hata kama hilo jambo unalifahamu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Mpaka sasa bado sijatoka katika hoja za Kisayansi, kwani Sayansi haina majibu ya kila kitu.

Mathalani kwa Wanasayansi wanasema uhai (Roho) unashikiliwa na hiyo Energy, hii ni dhana tu wala hawana ushahidi juu ya hilo.

Lakini sababu tunajua Sayansi ina ukomo na akili ya binadamu kadhalika, sasa mbele ya ukomo huo kuna majibu sahihi. Sasa hatuwezi kuacha majibu sahihi kwayo tunajua Sayansi haina uwezo wa kuyapata.
 

Hapa nimecheka sana.

Kazi yangu nimemaliza.

Penye ukweli uongo hujitenga mzee, na kwenye Sayansi kuna ushirikina na kuna ngano na visasili vya Sayansi.

Namaliza kwa kusema hivi "Hakuna nadharia ambayo inaweza kuthibhitisha ukweli wa nadharia nyingine". Na haya ya aliye nukuliwa na mtoa mada, hakuna anae weza kuthibhitisha ukweli wake mpaka mnakufa zaidi kuishia kwenye makaratasi na kuhadhiana kama story. Watu wanapenda story kuliko kuhoji na kutafuta ukweli.

Ahsante.
 
Nimesoma hiyo post na nilicho kiona ni kwamba wewe umeniwekea def. Ambazo huafikiani nazo.

Naomba unisaidie definition ya dark energy ambayo wewe una afikianan nayo mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio kweli nimeweka taarifu ambazo zinaelezea ukweli kuhusu Dark Energy, ndio maana nampinga aliyenukuliwa kwa maana hizo za Dark Energy. Sasa unatakiwa uelewe kwanza kisha ujenge hoja.

Hizo zote naafikiana nazo ndio maana nazijengea hoja na kushangaa mtu anapo toka na kutaka au kuaminisha watu jambo la nadharia za watu au imani potofu kuwa ndio ukweli na watu waamini hilo.

Ukitaka kujua uongo wa watu wakwambie au ujue maana ya maneno wanayo yatumia.

Ahsante.
 
Ushirikina ni nini? Nani alianzisha ushirikina? Kwa manufaa gani aliuanzisha? Unaweza kuthibitisha ushirikina ukoje kwa kuutenganisha na nadharia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…