Hapiness Magese avishwa pete ya $76,000

Hayo ndo matumizi ya pesa,kama ipo tumia kama huna jutia nampa thumbup bro kwa kumfisha Happy hiyo pete nawaombea sana harus iwe ya kifahari hadi uwekwe kwenye kumbukumbu ya TZ.Hamjasikia Pdidy kamzawadia mtoto wake gari lenye dhamani ya ajabu kwenye b/day tu.
 

Ni jambo la kawaida sana bro kwani waweza ukanunua chochote kile ila kazi ndiyo msingi wa maendeleo itakayo kukukopesha.

Watalii unao waona karibu asilimia 80 huwa wanakopa na kutalii, atahusisha budget yake kupitia pension au mshara wake atakaokuwa akiupata na kulipa deni. Kwa hiyo yawezekana jamaa ana kazi ya nguvu kachukua deni kununua pete pengine hata haijalipiwa cash.

Kuna kitu kinaitwa 'Laybay' ni kulipia kitu kiodgokidogo kikiwa bado kipo kimehifadhiwa dukani.

hata mtu anayeendesha gari ya milioni 100 ughaibuni isikutishe wote humu wamekopa magari, hata nyumba unakopa unailipa kwa mafungu.
 
Hongera kw kupata mshikaji, lakini ndugu zako kule kijijini wanakufa kwa njaa,wanalima kwa jembe la mkono.
 


Alivishwa kama hii? Lazima vibaka waibebe lasivyo atakiona cha moto.
 

na inawezekana ikawa fake diamond!!!!!!
 
Hongera kw kupata mshikaji, lakini ndugu zako kule kijijini wanakufa kwa njaa,wanalima kwa jembe la mkono.


Ungekuwa wewe umevalishwa pete hiyo, ungekumbuka maneno hayo???

Mwacheni kijana wa watu ale jasho lake!!
 
 
Ilaumu serikali wewe sio mtu kabeba Box kapata mshiko wake then unampangia matumizi? Umaskini wetu unaletwa na sera mbovu na zisizo tekelezeka....!!


Umesema kweli mkuu,mbona magari ya mamilioni yako barabarani yanaangizwa twayaona hakuna anaesema,wacha watu watumie pesa zao bana.
 

Wewe umesahau kwamba umasikini wa Watanzania ni mtaji wa kisiasa wa CCM? Umasikini wao ndio unaofanya wapige kura kwa kupewa khanga, vitenge, kofia, chupi, pilau, nyama, halafu wanjanja wa wajanja kidogo ndio wanaambulia Shs 10,000/=. Wanapiga kura, jamaa wanarudi mijini kwa miaka mingine mitano!
 
Hongera Happy Magese... nakutakia maisha mema na mwisho uolewe na uishi maisha mazuri na yenye baraka toka kwa muumba... Be a good girl and thankful to your blessings as you are always lucky
 

Samahani wadau, inawezekana mimi sielewi madini ya diamond gharama zake! hiv kumbe mtu anaweza kuvaa kiasi kikubwa namna hiyo cha pesa kwenye kidole tu? maana kwa makadirio ya haraka ni sawa na Tshs 99,000,000!
Duuh!
 
ubatili mtupu, na kujilisha upepo
Yes you said it rightly. Mfalme Suleman alishayaona haya siku nyingi!! Ndoa za namna hii kwa kawaida zina tabia ya kutodumu muda mrefu. Wanatakiwa kuwa waangalifu sana.

Leka
 
Samahani wadau, inawezekana mimi sielewi madini ya diamond gharama zake! hiv kumbe mtu anaweza kuvaa kiasi kikubwa namna hiyo cha pesa kwenye kidole tu? maana kwa makadirio ya haraka ni sawa na Tshs 99,000,000!
Duuh!

we wa wapi?unashangaa 99m??
 
hiyo pete amenunulia vibaka wataichukua muda si mrefu. huwezi kuvaa kitu ccha mamililioni dar halafu watu wakuangalie hivi hivi labda akaishi geniva
 
Kwani akivishwa expensive pete ndo mapenzi yatakuwa ya milele?takwimu zinaonesha kuwa ndoa nyingi za gharama kubwa huvunjka mapema sana...
 
Kama kweli waache wajinafasi kwa raha zao!..Tumia hela ikuzoee):
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…