Happy Anniversary (au ukipenda, happy birthday) kwa mahusiano ya Kenya-Tanzania

Happy Anniversary (au ukipenda, happy birthday) kwa mahusiano ya Kenya-Tanzania

pingli-nywee

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
11,923
Reaction score
13,350
Siamini kwamba mwaka mmoja umepita, bila ya hasira, visasi, mivutano, malumbano, majibizano na 'makasiriko', kati ya nchi mbili hizi za Kenya na Tanzania. Sio baada ya yote tuliyoyashuhudia, kwa karibia miaka sita.

Yaani tangia mwezi wa nne hivi mwaka uliopita mambo yaligeuka ghafla, yakawa shwari zaidi ya kale kaupepo ka ufukweni. Sasa hivi hata mgogoro wa mwisho, wa Machi mwaka jana, kuhusu mahindi na sumu kuvu tumeusahau kabisaaa.

Hata kile kitendo cha kustaajabisha. Kilichotutonesha vidonda na kupelekea vifaranga visivyo na hatia, vionje ghadhabu kali ya binadamu, tumekizika kwenye kaburi la sahau.

Sijui kitakachofata au hapo mbeleni hali itakuwaje. Ila 'stage' kama hii ndio ile ambayo huwa unawapata wapendanao wakitazama mara kwa mara na kupeana tabasamu za bure. Vicheko navyo huwa vimeshamiri, tena vya kushirikisha meno yote 32, bila ubaguzi. Alafu utasikia, 'baby unajua leo ndio mwaka mmoja umefika tangu tupatane na tupendane?'

Happy Anniversary guys! 🇰🇪🇹🇿🇰🇪🇹🇿
 
Watz walikua wamepigwa na kitu kizito kwenye miaka hiyo sita, nenda majukwaa yao ya siasa uone nyuzi za kuponda huo utawala zinavyochachamaa, kwanza ripoti ya CAG ndio imefunika kabisa.....

Huyu mama Samia tumuombee tuendelee vizuri, ila upande wetu Kenya tuwe makini tusije tukamchagua kichaa wa kuturudisha nyuma.

Hata wale buku saba kama wametoweka, wamebaki wachache kama mayatima waliochanganyikiwa na upepo unavyovuma.
 
Siamini kwamba mwaka mmoja umepita, bila ya hasira, visasi, mivutano, malumbano, majibizano na 'makasiriko', kati ya nchi mbili hizi za Kenya na Tanzania. Sio baada ya yote tuliyoyashuhudia, kwa karibia miaka sita.

Yaani tangia mwezi wa nne hivi mwaka uliopita mambo yaligeuka ghafla, yakawa shwari zaidi ya kale kaupepo ka ufukweni. Sasa hivi hata mgogoro wa mwisho, wa Machi mwaka jana, kuhusu mahindi na sumu kuvu tumeusahau kabisaaa.

Hata kile kitendo cha kustaajabisha. Kilichotutonesha vidonda na kupelekea vifaranga visivyo na hatia, vionje ghadhabu kali ya binadamu, tumekizika kwenye kaburi la sahau.

Sijui kitakachofata au hapo mbeleni hali itakuwaje. Ila 'stage' kama hii ndio ile ambayo huwa unawapata wapendanao wakitazama mara kwa mara na kupeana tabasamu za bure. Vicheko navyo huwa vimeshamiri, tena vya kushirikisha meno yote 32, bila ubaguzi. Alafu utasikia, 'baby unajua leo ndio mwaka mmoja umefika tangu tupatane na tupendane?'

Happy Anniversary guys! 🇰🇪🇹🇿🇰🇪🇹🇿
Yule jamaa alikuwa mshamba sana. Alikuwa anaogopa kupanda ndege. Kiingereza chake kilikuwa kinatia watu aibu. Chuki yake dhidi ya Kenya ilikuwa nyingi ungedhani tulimuibia mke wake. Very useless guy.
 
Watz walikua wamepigwa na kitu kizito kwenye miaka hiyo sita, nenda majukwaa yao ya siasa uone nyuzi za kuponda huo utawala zinavyochachamaa, kwanza ripoti ya CAG ndio imefunika kabisa.....

Huyu mama Samia tumuombee tuendelee vizuri, ila upande wetu Kenya tuwe makini tusije tukamchagua kichaa wa kuturudisha nyuma.

Hata wale buku saba kama wametoweka, wamebaki wachache kama mayatima waliochanganyikiwa na upepo unavyovuma
Tukishampata rais ajaye, uhusiano kati ya Kenya na Tanzania ndio utaharibika kabisa. Mark my words. Hakuna afueni, sio kwa Ruto wala kwa Raila. Yaani wote hao ni manyang'au kweli kweli, tena ile ambayo sio ya mzaha. 😄
 
Wakenya ni wanafiki waliokubuu,
Mmetengeneza tukio la kuchafua utalii Tanzania kupitia lile tapeli la Naija Warere hotel ili kuharibu uzinduzi wa Royal Tour Film.
Baada ya kufeli vibaya mnakuja na unafiki wa ujirani na undugu.
Siku TZ tukipata Raisi mwingine kichwa kibovu, asiishie tu kuchoma moto kuku bali hata nyie awachome moto.
 
Kwanini watanzania hawaonyeshi "excitement" Kama ninyi wakenya?, Hii inaonyesha jinsi gani Tanzania ilivyo muhimu kwa Kenya [emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Tukishampata rais ajaye, uhusiano kati ya Kenya na Tanzania ndio utaharibika kabisa. Mark my words. Hakuna afueni, sio kwa Ruto wala kwa Raila. Yaani wote hao ni manyang'au kweli kweli, tena ile ambayo sio ya mzaha. [emoji1]
Ushirikiano ukiharibika ndio furaha kwa watanzania wengi, hatutaki urafiki na Kenya.

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Wakenya ni wanafiki waliokubuu,
Mmetengeneza tukio la kuchafua utalii Tanzania kupitia lile tapeli la Naija Warere hotel ili kuharibu uzinduzi wa Royal Tour Film.
Baada ya kufeli vibaya mnakuja na unafiki wa ujirani na undugu.
Siku TZ tukipata Raisi mwingine kichwa kibovu, asiishie tu kuchoma moto kuku bali hata nyie awachome moto.

Mlikua pabaya....

20220409142523-jpg.2193860
 
Tukishampata rais ajaye, uhusiano kati ya Kenya na Tanzania ndio utaharibika kabisa. Mark my words. Hakuna afueni, sio kwa Ruto wala kwa Raila. Yaani wote hao ni manyang'au kweli kweli, tena ile ambayo sio ya mzaha. 😄
Raila ana busara anaheshimu Tanzania , imemsaidia na anakiri bila kificho
 
Mlikua pabaya....

20220409142523-jpg.2193860
Kumbe mnaona TZ ipo kwenye healing process halafu nyie mnatusagia kunguni?
Kama ndio utamaduni mpya sisi tutaomba na nyie kwenye ROUND HII mtwangane kweli kweli.
Kwanzia August hapo Kenya biashara ya mapanga itashamiri sana.
Nchi ambayo raia wake hawaogopi kuuana wenyewe kwa wenyewe kamwe hawawezi kuishi ma majirani kwa kuheshimiana.
Hamna adabu nyie.
 
Kumbe mnaona TZ ipo kwenye healing process halafu nyie mnatusagia kunguni?
Kama ndio utamaduni mpya sisi tutaomba na nyie kwenye ROUND HII mtwangane kweli kweli.
Kwanzia August hapo Kenya biashara ya mapanga itashamiri sana.
Nchi ambayo raia wake hawaogopi kuuana wenyewe kwa wenyewe kamwe hawawezi kuishi ma majirani kwa kuheshimiana.
Hamna adabu nyie.

Halafu naona mnaomba kuweka sanamu kabisa Ni wakati sasa wa kujenga sanamu la Magufuli. Tukubaliane kama nchi tulijenge wapi?
 
Back
Top Bottom