Harambee Stars(Kenya) wapo Ufaransa , The Cranes(Uganda) wapo Abu Dhabi, Les Léopards(DRC) wapo Hispania. Je, Taifa Stars(Tanzania) wapo wapi?

Hapo ndo nilishangaa,eti records hawana. Hivyo wakaamini records ambazo ziliwekwa na Kagera wenyewe. Stand united wametolewa kafara.
 
Ubovu wa ligi kuliko miaka yote upo wapi...yanga wasipochukua ubingwa basi ligi inageuka kuwa mbovu...haya mbona hamkuyasema kipindi mnachukua ubingwa mara tatu mfululizo...nyie tulieni dawa iwaingie vizuri hakuna namna
Ushabiki wa design yako ndio unaua soka,Ulishaona wapi na lini FA inakosea kutangaza team zilizoshuka au Siku ya kukabidhi kombe mpira umeisha ndio unaambiwa hawalitoi kombe siku hiyo au mnatangaza mechi za mwisho za Ligi zitaanza muda mmoja kuepuka upangaji matokeo then mechi zingine zinaanza saa 9 jioni na zingine saa 10.
Umeshaona wapi ligi bado mechi 6 kuisha ila kuna team hazijawahi kucheza mechi zote 2 (Yaani 2 kati ya hizo 6 ni za mechi za raundi ya kwanza na pili)refer Yanga na Azam na Simba vs Mtibwa na Biashara
 
Maendeleo hayana itikadi, kabila wala chama lakini ni ngumu kuniaminisha kuwa chama cha soka ambacho upeo wao hauwezi hata kujua ni timu gani inapanda au inashuka, naamini kabisa hawawezi kuipeleka Stars popote!
Kibaya zaidi ni tabia za Watanzania maana hawa TFF wametutia aibu Afcon under 18 na hakuna hata mmoja aliyewajibika na tunawachekea tu!
 
Ila leo wameingia kambini kufuatia Patel kutoa hotel yake kama kambi pia na huduma ya chakula
 
Nadhani hawa TFF kama wana shida ya kifedha ni bora waseme mapema kuliko kwenda kutiana aibu kule Cairo
 
Wapo white sand bibie, halafu tunategemea tufanye maajabu afcon
 
Hao tifua tifua wako bize kuzindua sijui jezi za stars, yani tff ndo wachawi wa mpira wa bongo, wenzetu wameanza maandalizi sisi kimya, halafu tunasubiri maajabu
 
Ubovu wa ligi kuliko miaka yote upo wapi...yanga wasipochukua ubingwa basi ligi inageuka kuwa mbovu...haya mbona hamkuyasema kipindi mnachukua ubingwa mara tatu mfululizo...nyie tulieni dawa iwaingie vizuri hakuna namna
Ubovu upo hapa, ligi haina mzamini, timu ina viporo 12 akati wengine wamebakiza mechi 2, tff na bord ya ligi hawajui timu gani inayositahili kushuka, hawa wana msimamo huu, na wengine huu, marefa kufata maelekezo, mfano mechi ya kmc na simba, n.k
 
Hapo ndo nilishangaa,eti records hawana. Hivyo wakaamini records ambazo ziliwekwa na Kagera wenyewe. Stand united wametolewa kafara.
Bord ya ligi walikuwa na record zao, tff nao wanazao, ndo yale ya mwaka jana, mcheza ana kadi ya njano wengine 3, wengine 2, yani full mapicha picha
 
Ndo mana nakwambia kwanini sikuzote hujawahi toa haya malalamiko ila baada ya timu yako kukosa ubingwa ndo umeanza kutoa kasoro....hizi changamoto kwa soka la africa ni kitu cha kawaida...jana kuna timu tena fainali ya kombe la africa Waydad inafunga goli zuri tu refa anakataa wachezaji wanamwambia refa akacheki marudio kwenye VAR wanaenda kucheki VAR hazifanyi kazi...wamesubiri lisaa limoja haziwaki wachezaji wa waydad wakagoma kurudi uwanjani refa akaamua kumaliza mpira ESP wakapewa ubingwa wa mezani...sasa ingekuwa ni yanga kafanyiwa hivyo mbona humu pasingekalika...mtu kama analalamika mechi ya mwisho ya Mtigwa na Simba kuanza saa 9 wakati wengine wameanza saa 10 mtu kama huyo sijui tumweke kundi gani....hajui kuwa mechi za mwisho huwa zinachezwa muda mmoja kuepusha kupanga matokeo....matokeo ya mtigwa na simba ya aina yoyote yalikuwa hayana athari kwa timu nyingine na ile ilikuwa ni kuwahi kwa sababu kulikuwa na sherehe za kukabidhi kombe...tatizo mnadanganywa sana na Zahera...sasa shangaa ya mechi za mwisho ligi kuu tanzania simba kucheza saa 9 wakati timu nyingine zinaanza kucheza saa kumi na kuna watu mnalalamika...Zahera kule kwao Congo ligi imeisha na timu karibia zote zimemaliza michezo but kuna timu bado zina mechi tatu mkononi wakati nyingine zimemaliza mechi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…