Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
HARRY BELEFONTE MIAKA 96
Miaka ya mwanzoni 1970s nilikuwa napita nje ya ofisi ya British Airways.
Mbele yangu nikawaona Harry Belafonte na Sidney Poitier wanatoka katika ofisi hiyo.
Itaendelea...
Nikawasogelea karibu nikawasalimia na kuomba autograph zao.
Nilikuwa sina karatasi nikatoa kitambulisho changu cha East African Cargo Handling Services wakaweka saini zao nyuma ya kitambulisho changu.
Nakumbuka nyimbo yangu ya kwanza kuisikia ya Harry Belafonte ilikuwa, "Round the Bay of Mexico," ikipigwa katika radio.
Ilikuwa mwaka wa 1957 nakaa Mtaa wa Kiungani Gerezani kwa mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha bint Mohamed.
Jirani yetu kwenye kona ya Mtaa wa Kiungani na Mtaa wa Sikukuu ilikuwa nyumba ya Mashado Plantan.
Hii ilikuwa ndiyo nyumba nzuri kupita zote pale mtaani ikiwa na kila kitu maji, umeme nk.
Namkumbuka mwanae Rita mama yake Mjerumani.
Rita alikuwa mkubwa kwangu kwa umri.
Mashado Plantan alikuwa na mke wa Kijerumani.
Lakini Harry Belafonte alikuwa akipendwa na Bibi yangu Zena bint Farijala.
Bibi kila ilipotokea nafasi ya kuhadithia senema ataeleza movie ya Harry Belafonte "Island in the Sun," aliyoiona na babu yangu Salum Abdallah miaka mingi iliyopita katika ujana wao.
Kipande alichopenda kuhadithia ni Harry Belafonte kupendwa na bint wa Kizungu.
Basi nami nikawa namjua Harry Belafonte na kupenda muziki wake toka utoto wangu.
Katika nyimbo nilizozipenda ilikuwa, "Coconut Woman."
Baadae Harry Belafonte alipokutana na Miriam Makeba wakawa wanaimba pamoja nikapenda sana nyimbo yao, "Train Song."
Hii nyimbo wameimba kwa Kizulu na waliimba nyimbo nyingi kwa Kizulu na Ki-Khosa na kwa hakika utazipenda.
Mwanangu aliniletea biography ya Harry Belafonte "My Song."
Ananambia kwenye duka la vitabu muuzaji alimuuliza kama hicho kitabu atasoma yeye.
"Hiki nampelekea baba yangu yeye anampenda Harry Belafonte."
Belafonte kuna sehemu katika kitabu ilinihuzunisha kidogo kwani hakumsema vizuri Miriam Makeba juu ya hisani kubwa iliyopitika kati yao wakati wa ujana wao wakishirikiana katika muziki.
Makeba anasema hakuna jambo lililokuwa likimpa raha na starehe kama kuwafundisha Wamarekani kuimba nyimbo za Kizulu.
Miaka ikapita nikajikuta niko New York najibanza Manhattan pembeni ya Hudson River.
Wenyeji katika mazungumzo wakanifahamisha kuwa nikivuka mto tu nitafika nyumbani kwa Belafonte.
Bahati mbaya hakuna aliyekuwa anafahamiananae anipeleke kwake.
Harry Belafonte na Sidney Poitier wamefika Tanzania mara mbili na Hamza Aziz alipata kuwaalika nyumbani kwake kwa chakula cha jioni.
Picha hiyo hapo chini Hamza Aziz kulia akiwafahamisha Harry Belafonte na Sidney Poitier kwa Ally Sykes.
Miaka ya mwanzoni 1970s nilikuwa napita nje ya ofisi ya British Airways.
Mbele yangu nikawaona Harry Belafonte na Sidney Poitier wanatoka katika ofisi hiyo.
Itaendelea...
Nikawasogelea karibu nikawasalimia na kuomba autograph zao.
Nilikuwa sina karatasi nikatoa kitambulisho changu cha East African Cargo Handling Services wakaweka saini zao nyuma ya kitambulisho changu.
Nakumbuka nyimbo yangu ya kwanza kuisikia ya Harry Belafonte ilikuwa, "Round the Bay of Mexico," ikipigwa katika radio.
Ilikuwa mwaka wa 1957 nakaa Mtaa wa Kiungani Gerezani kwa mama yangu mkubwa Bi. Mwanaisha bint Mohamed.
Jirani yetu kwenye kona ya Mtaa wa Kiungani na Mtaa wa Sikukuu ilikuwa nyumba ya Mashado Plantan.
Hii ilikuwa ndiyo nyumba nzuri kupita zote pale mtaani ikiwa na kila kitu maji, umeme nk.
Namkumbuka mwanae Rita mama yake Mjerumani.
Rita alikuwa mkubwa kwangu kwa umri.
Mashado Plantan alikuwa na mke wa Kijerumani.
Lakini Harry Belafonte alikuwa akipendwa na Bibi yangu Zena bint Farijala.
Bibi kila ilipotokea nafasi ya kuhadithia senema ataeleza movie ya Harry Belafonte "Island in the Sun," aliyoiona na babu yangu Salum Abdallah miaka mingi iliyopita katika ujana wao.
Kipande alichopenda kuhadithia ni Harry Belafonte kupendwa na bint wa Kizungu.
Basi nami nikawa namjua Harry Belafonte na kupenda muziki wake toka utoto wangu.
Katika nyimbo nilizozipenda ilikuwa, "Coconut Woman."
Baadae Harry Belafonte alipokutana na Miriam Makeba wakawa wanaimba pamoja nikapenda sana nyimbo yao, "Train Song."
Hii nyimbo wameimba kwa Kizulu na waliimba nyimbo nyingi kwa Kizulu na Ki-Khosa na kwa hakika utazipenda.
Mwanangu aliniletea biography ya Harry Belafonte "My Song."
Ananambia kwenye duka la vitabu muuzaji alimuuliza kama hicho kitabu atasoma yeye.
"Hiki nampelekea baba yangu yeye anampenda Harry Belafonte."
Belafonte kuna sehemu katika kitabu ilinihuzunisha kidogo kwani hakumsema vizuri Miriam Makeba juu ya hisani kubwa iliyopitika kati yao wakati wa ujana wao wakishirikiana katika muziki.
Makeba anasema hakuna jambo lililokuwa likimpa raha na starehe kama kuwafundisha Wamarekani kuimba nyimbo za Kizulu.
Miaka ikapita nikajikuta niko New York najibanza Manhattan pembeni ya Hudson River.
Wenyeji katika mazungumzo wakanifahamisha kuwa nikivuka mto tu nitafika nyumbani kwa Belafonte.
Bahati mbaya hakuna aliyekuwa anafahamiananae anipeleke kwake.
Harry Belafonte na Sidney Poitier wamefika Tanzania mara mbili na Hamza Aziz alipata kuwaalika nyumbani kwake kwa chakula cha jioni.
Picha hiyo hapo chini Hamza Aziz kulia akiwafahamisha Harry Belafonte na Sidney Poitier kwa Ally Sykes.