Hasara ya kula vyakula Feki Junk food take a way

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
MATATIZO YA KIAFYA YANAYOSABABISHWA NA KULA VYAKULA VYENYE “HYDROGENATED VEGETABLE OILS.” MFANO WA VYAKULA VYENYE HAYA MAFUTA NA MAGONJWA YALIYO ASHIRIWA KUSABABISHWA NA HAYA MAFUTA.






Well, since background yangu kielimu na kikazi ni juu ya afya ya jamii, leo niliona hebu ngoja nipitie huu uwanja wa AFYA kiundani. Kwa maana ijapokuwa ninajidhania nimekubuu vizuri katika hii fani ya AFYA bado naelewa kwamba kuna mambo mengi kuhusu AFYA ambayo ninaweza kujifua kiundani zaidi.

Hivyo basi, nimeona kwanini nijifunze mwenyewe wakati ninaweza kujifunza na darasa kubwa ikiwa ni wewe msomaji.
Leo katika pita pita zangu niliona nisome kiundani zaidi kuhusu hivi vyakula tunavyokula kila siku. Ikiwa ni pamoja na vyakula vya mabox, vyakula vya migahawani (fast foods) na hata vitu kama mafuta tunayotumia wakati wa kutayarisha chakula (kupika).

Kwa kuanza basi, kama inavyoeleweka hapa Marekani unaweza kupata vyakula vya kila aina iwe unapendelea "ORGANIC" ama "NON ORGANIC," "KUPIKA MWENYEWE NYUMBANI" ama "KULA FAST FOODS." Uwezo ni? Wako.
Well, either way kuhusu mambo ya vyakula hapo juu, binafsi I have a hard time kuamini kwamba nikienda "WHOLE

FOODS" kila chakula ni "ORGANIC" as they claim it. Nadhani as long as naishi Marekani, mivyakula yote ni processed nikimaanisha kwamba somehow wakati wa production some kind of "madawa yalitiwa ndani eidha kuongeza utamu wa

chakula ama kumkuza kuku na ng'ombe haraka haraka." Well, nadhani hii ni moja wapo ya malipo ya kuishi marekani na sio Afrika. Kitu kingine, unless nimekipanda chakula na kukichuma mwenyewe shambani kwangu basi sinamatumaini makubwa juu ya vyakula ninavyo nunua madukani.
Anyways, nirudi kwenye topic.

Tafiti zime na zinaonyesha kwamba; kuna uhusiano mkubwa kati ya vyakula vilivyotengenezwa na mfuta ya kuigizwa "hydrogenated oils" na ukubwa wa matokeo ya namba ya ugonjwa wa CANCER (vifo na wagonjwa kiujumla).


Vyakula vingi hapa marekani vinapokuwa vikitengenezwa hutumia mafutafeki yanayoitwa "HYDROGENATED OILS" haya mafuta yanapotumiwa yanavuruga na kupoteza umuhimu wa mafuta yanayopatikana kupitia wanyama waliokuwa na

kulishwa lishe bora na pia mimea inavyotoa mafuta. Maranyingi haya mafuta feki, yanapotumiwa husaidia kufanya chakula kitesti vizuri mdomoni na kuongeza ladha na pia husaidia kuongeza mda wachakula kukaa katika shelf dukani bila ya kuharibika.

Haya mafuta feki hutengenezwa kwa kuchukuwa "mafuta ya kawaida na kuyapitisha katika presha ya Hydrogen gas (250-400 digree farenheight) kwa muda wa masaa huku kukiwa na kichocheo (catalyst) kama nickel au platinum." Hii process ya kisayansi wanasema ni nzito kiasi cha kwamba kuna compounds zinakuwa zinajitengeneza wakati wa hii

process ambazo hazijawahi kuonekana before wakimaanisha kwamba, wanasayansi walianza kuona ama kuzijua hizo compound baada ya viwanda kuanza kutengeneza haya "MAFUTA FEKI." Part ya hizo compounds zinaitwa "trans" fatty acids. Kama wote tunavyojua "fatty acids" ndo chanzo cha kutengenezwa kwa "fats/Mafuta" na nyinginezo

compounds nyingi tuu ambazo sio nzuri katika mwili wa binadamu whatsoever. Haya ni mafuta yasiyo funjika tunaweza kusema.
NI MATATIZO GANI YANAYOSABABISHWA NA HAYA MAFUTA YASIYO VUNJIKA "TRANS FAT” KATIKA MWILI WA BINADAMU?




Kwanza kabisa, binadamu anapokula vyakula vilivyotengenezwa na haya mafuta (in this case vyakula vingi vya hapa marekani vinavyouzwa madukani), matatizo ya kiafya hutokea mfano kama; magonjwa ya moyo, cansa, kisukari, upungufu wa mwili kutengeneza kinga wenyewe, magonjwa ya kizazi na obesity (fetma kwa Kiswahili).

Pia unaposikia mtu ana high cholesterol, hii husababishwa na haya mafuta ambayo mara nyingi huwezi kuyaepuka kwamaana yapo katika kila chakula kilichopo mdukani hapa marekani (kwasababu these foods are processed foods). Hivyo cholesterol yako kuwa juu ama chini inategeana na chakula unachokula na jinsi ulivyo physically active in your daily life.

Tafiti zilizofanywa na Maryland University na U.S. Foods and Drug Administration zilionyesha kwamba uhusiano wa magonjwa kama KANSA katika wagonjwa viliambatana sana na wagonjwa hawa kuwa at some point katika maisha yao walikuwa wakila vyakula vingi vilivyokuwa vinahaya mafuta feki (hydrogenated oils). Kwa uhakiki zaidi: { trans fatty

acids induce adverse alterations in the activities of the important enzyme system that metabolizes chemical carcinogens and drugs (medications), i.e., the mixed-function oxidase cytochromes P-448/450.} Kiswahili lugha "tata" sikuweza kutranslate hii kitu.

Hata hivyo, “trans fatty acids” husababisha kupungua kwa chembe chembe za damu hivyo hata wanye diabetes (fetma) hupata matatizo zaidi katika kutengeneza insulin.
Well, kama unapata shida kuelewa processed foods ni vyakula vya aina gani, well hauko peke yako list hii hapa;
Vyakula vya makopo




Vyakula vilivyokuwa frozen kwenye mifuko au mabox na vyote vyenye lebo zisizoeleweka LOL. Just stay away!!!
Tunaelewa maisha yetu huku marekani ni ya haraka haraka mda wote. Na vyakula vya mabox na makopo ndo vilivyojaa madukani. Cha msingi ni kuwa makini wakati unapoenda dukani kununua chakula. Kama unaweza kununua

vyakula fresh meaning staying mostly in the "fresh produce" area ndo vizuri. Kupika chakula chako nyumbani ni mwendo mmoja wapo wa kupunguza kula vyakula vilivyokuwa processed. Pia badala yakwenda maduka makubwa makubwa kununua chakula, jaribu kutembelea "local foods grown" stores ni njia moja wapo pia ya kurudisha wema katika community. Kula mboga za majani zaidi na matunda
 
pole zenu wamarekani kwani huku bongo ukiingia pale kinondoni mahakamani utapata mchicha bomba tu na vitu vingine vya kula magengeni..

ila kuhusu hot dogs na sausage duu itakuwa ngumu kidogo..
 
njoo huku zenjiberi ule raha,unanunua pweza ngisi,kamba koche (king lobster) wakiwa hai,chicha ,samvu,tembele bado linanuka vumbi,unanunua nazi ikiwa mtini("nikuangulie nazi ngapi? na juice nikuangulie(dafu)?"-muuza/mkwezi akiwa juu ya mnazi anamuuliza mteja wake).
Pata embe ,chungwa ,nanasi durian,shelisheli fresh! njoo muzizi utie raha mwilini!
 
Ahsante sana kwa ushauri mzuri Mzizimkavu, mimi ni mdau wa italian foods haswa macaron,.sasa sijui na hivyo vya kupika pia vina madhara sana au mpaka vile unavyonunua tu na kula ndo vina shida,. hapo sijaelewa vizuri, sorry
 
Welcome to TUKUYU y'll.
Chakula huku Mungu ame2bless. Shambani madizi kibao, shamba la chini kumenjta majimbi na mihogo. La katumba kuna mahindi kibao. Dukani mafuta ya alizeti ndo mpango mzima. Kuku sasa wa huku kwa kupenda cfa, manake wanataga kama mashndano, huyu kafya2a 4, hujakaa vizuri kishingo kanya yai 3. Hujaokota mara mwingine kadondosha 5. Unaamua kususa unaachana nao. Ukitoka nje maparachichi yameletwa na mtoto wa jirani. Unayapokea unaenda zako bandani kukamua maziwa.

Kimbieni mijini.
 
Ndio maana mie namshangaa mtu anaetusukumizia alie vera wakati ziko bustanini kwetu!
 
Topic nzuri saana inabidi tukimbie junk foods na kula vyakula fresh but mbona most of the people wanasema junk foods ndo zinanenepesha??? I'm confused hapo...

Regards,
Jonathan.
 
Topic nzuri saana inabidi tukimbie junk foods na kula vyakula fresh but mbona most of the people wanasema junk foods ndo zinanenepesha??? I'm confused hapo...

Regards,
Jonathan.
Mkuu kunenepa sio ndo kuwa na afya.
 
Wow whta nice article!
Dah yani haya mavyakula basi tu mtu unasema Mungu saidia,maana sio kwamba unapenda na sio kula sikuzote.
Sometimes muda na system ya maisha ndo vinaku-tune uwe kwenye mkumbo.
Kupika unapika ila huwezi kuwa unapika kila siku..sometime viporo unapasha.
Na vinachosha. So mtu ukitoka kazini umechoka unapiga simu kinakuja unakula unalala,habari za kuanza kupika aisee ni muhimu ila hadi huo muda uwepo akili itulie upike unachotaka.
Ila kama ndo hivi uwiii...nehi no more🙂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…