HASHEEM Thabeet ampiga mtama TID!

Fareed

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2010
Posts
328
Reaction score
135
STREET FIGHT: HASHEEM THABEET VS. TID :mad2:

ILIKUWA muda wa kama saa nane na nusu usiku. Siku ni Ijumaa tarehe Mei 7, 2010. Nilikuwa nimesimama nje kwenye parking karibu na mlango wa kuingilia Club Billicanas jijini Dar es Salaam nikitafakari nifanye makeke gani usiku huo. Nikiwa nimesimama kwa pembeni, nilimuona msanii wa Bongoflava maarufu kama TID akiingia club huku akiwa ameambatana na kimwana. TID alikuwa amevaa suruali jeans imepauka huku akining'iniza kitambaa (handkerchief) kwenye mfuko wa suruali wa nyuma. Alionekana akiwa high ready to have a good time in the club. Dakika kama 20 baada ya TID kuingia, nikaona Range Rover Sport nyeusi inaingia kwenye parking ya club. Kama sikosei number plates zake ni TSSS 101. Nikiwa nimevutiwa kuliangalia hili gari, nikaona vioo vimeshushwa na mchezaji wa basketball kule mtoni kwenye ligi ya NBA, Hasheem Thabeet, ndiyo anaendesha hiyo Rover. Akiwa amevaa kapero (cap) huku akiambatana na wapambe kama watatu, Hasheem alisalimiana na bouncers na washkaji wengine mlangoni na kuingia club.

Nikiwa naendelea kucheki vimwana wakali wakiingia club, mara naona TID anatoka kwa mwendo haraka kutoka ndani ya club. Nyuma yake namuona Hasheem anamfuata TID huku akiwa anaonekana mwenye hasira.

Mara Hasheem akampiga mtama TID akadondoka kwenye pavement karibu kabisa na mlango wa kuingilia club na kujipiga kisogo sakafuni. Wapambe na bouncers wakajaribu kumvuta Hasheem pembeni lakini Hasheem akaonekana mwenye hasira na kutaka kuendelea kumchapa TID.

Mpambe mmoja wa Hasheem akamwambia, "People are just looking at you cos you are the super star, achana na huyo **** (TID)."

Hasheem akamwambia TID "Mimi ni mtoto wa Sinza, usicheze na mimi ****mayo."

Wapambe wa Hasheem wakafanikiwa kumchukua Hasheem na kwenda naye kuelekea Ben Mkapa Towers, nadhani Savannah club.

Huku chini, TID akaanza kulia kwa sauti. He was kicking and screaming on the ground, obviously trying to create a scene aonekane kama kaumizwa sana na Hasheem. Msichana aliyekuwa na TID alibaki amesimama pembeni, looking sooo embarrassed huku TID akipiga mayowe.

Then TID got up and started running after Hasheem, demu wake alijaribu kumzuia akamsukuma kwa nguvu.

TID aliishia mpaka mbele kidogo ya eneo la kuingilia bar ya Break Point iliyo karibu na Billicanas na kukutana na askari polisi waliokuwa kwenye patrol.

Baada ya kuona Hasheem katoweka, TID alitimka zake kwenye eneo hilo na kuondoka mjini.

CHANZO CHA UGOMVI: Sifahamu nini haswa kilisababisha celebrities hawa wetu wakwaruzane. Watu waliokuwa ndani ya club wanasema TID hakupenda Hasheem alivyomuangalia baada ya kusalimiana wakiwa ndani ya club. Wengine wanasema msichana aliyekuwa na TID alimuomba Hasheem autograph, au ili bainika kuwa binti huyo alikuwa anajuana na Hasheem hivyo TID akanuna na kuamua watoke nje wazichape.

MASWALI YA KUJIULIZA: Je, kama wangeachiwa wazichape the giant Hasheem na the short, slim TID, matokeo yake yangekuaje? Huyu Hasheem hajui kuwa status yake ni kubwa sana na amepata rare opportunity kuwa balozi wa Tanzania kwenye NBA? Hizi beef za celebrities si mambo ya upumbavu tu? Hawa celebrities watakuwa lini? Ni hayo tu.
 
His lanky ass should stay away from bad publicity....
 
Hii noma duu, hasheem angeua Top band, Wasanii wa kibongo nao wamezidi mashauz.... hata dozi hiyo aliyompa ndogo sana. TID asije akanyea debe mara nyingine.... awe makini.
 
hao ndo celebrities wa kibongo bana.................!!!!
 
Hii noma duu, hasheem angeua Top band, Wasanii wa kibongo nao wamezidi mashauz.... hata dozi hiyo aliyompa ndogo sana. TID asije akanyea debe mara nyingine.... awe makini.

samahani ndugu, hiyo username yako ina maana gani?
samahani kama nimekukwaza, imezua maswali mengi kichwani mwangu.
 
ni kweli bro...hakuna kitu hapo

Hasheem namwona hapa IFM shule na VOGUE lake anafungulia muziki mkubwa milango yote wazi na wapambe wake kisa anatafuta attention kwa wasichana.....????????? kama mtu anabisha leo mida ya saa 11 na nusu pitia pale IFM chuo utajionea mwenyewe.
 
TID azichapa na Thabeet....
Thabeet na TID wazipiga kavukavu etc
What a headline kwa Shigo!
 
HIVI ASHEEM MZIMA KWELI, MAmBO YA UPUUZI KABISA HAYO KAAZI KWELIKWELI
 
Hasheem namwona hapa IFM shule na VOGUE lake anafungulia muziki mkubwa milango yote wazi na wapambe wake kisa anatafuta attention kwa wasichana.....????????? kama mtu anabisha leo mida ya saa 11 na nusu pitia pale IFM chuo utajionea mwenyewe.

hili lijamaa kibaiolojia tunaliitaga mutation heheehhe limekuwaga refu beyond DNA limiti.
 
Hasheem namwona hapa IFM shule na VOGUE lake anafungulia muziki mkubwa milango yote wazi na wapambe wake kisa anatafuta attention kwa wasichana.....????????? kama mtu anabisha leo mida ya saa 11 na nusu pitia pale IFM chuo utajionea mwenyewe.

Huyu dogo naona anachezea career yake sasa maana watu wa NBA wana personal conduct policy na haijalishi uko wapi. Wao wanataka wawakilishwe vyema na wawakilishi (wachezaji na watu wengine walo affiliated nao) wao. Huyu dogo na ujinga wake atakuja kutoswa huyu. Mchezo wenyewe hauwezi vizuri halafu bado ana act kijinga jinga. Ngoja David Stern asikie hizi habari na kama ni za kweli tutaona kitakachoendelea
 
Hasheem Thabeet analipwa $10 million a year na timu yake huko Marekani. Hizi ni pesa nyingi sana kwa kijana yoyote na haswa kwake yeye kwa vile alikuwa na maisha magumu kabla ya kufanikiwa kwenda NBA. Ni dhahiri kuwa asipokuwa makini, utajiri huu mkubwa na wa ghafla alioupata utamchanganya.

Ndiyo maana Hasheem alikuwa demoted from NBA. Asipoangalia ataharibikiwa maisha yake na kutimuliwa Marekani. Anahitaji guidance na role model wa kumuonyesha njia so he keeps his feet on the ground. TUMSAIDIE HUYU KIJANA WETU ALIYEIPA SIFA TANZANIA KWENYE NBA ASIPOTEE NJIA.

http://webcache.googleusercontent.com/search?q=cache:WJHoiSsMWa0J:sportsbusinessdigest.com/comparing-nbanfl-rookie-contracts/+hasheem+thabeet+%2410m&cd=1&hl=en&ct=clnk
 
Hasheem has got to be careful! Huyo TID inaelekea pombe haziwezi. Si hata wakati ule alienda jela baada ya kumpiga mtu akiwa amelewa?!
 
Hasheem namwona hapa IFM shule na VOGUE lake anafungulia muziki mkubwa milango yote wazi na wapambe wake kisa anatafuta attention kwa wasichana.....????????? kama mtu anabisha leo mida ya saa 11 na nusu pitia pale IFM chuo utajionea mwenyewe.

kashelewa huto tumafanikio kiganjani mwake tu............
sasa anataka kila mtu amfahamu tena kwa ubaya basi

bora ukose mali upate akili kwa kweli aghrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr!!!
 
Du ! kupigana kumepitwa na wakati.
 
And wait a minute...how big is TID? Hashimu should pick somebody his own size if he thinks he's a bad ass....
 
Hasheem namwona hapa IFM shule na VOGUE lake anafungulia muziki mkubwa milango yote wazi na wapambe wake kisa anatafuta attention kwa wasichana.....????????? kama mtu anabisha leo mida ya saa 11 na nusu pitia pale IFM chuo utajionea mwenyewe.
hawa ndio masupastaa wa kibongo hawa?badala ya kuwaza mambo ya maana akili zimejaa ugoro tu na masifa kwa mademu,yaani watu wengine sijui wameumbwaje jamaa ustaa wote alioupata bado akili kama ya mtoto wa kiswazi manzese au tandale kabisa,T.I.D kafanya makusudi kumchokoza kwani yeye tid hana atakachopoteza,ila jamaa yangu mrefu kavu kweli,mi nilijua sasa hivi kuteremka na hilo vogue makusudi awakomoe waswahili walipomsema alipokuwa kashushwa daraja.sasa sijui anamkomoa nani,bwa mdogo kua hivi visenti vya msimu vitakimbia utabaki kusema mimi ndiyo yuuule hashimu wa N.B.A.shauri yako,wamechoka kina mike tyson,wesley snipes itakuwa huyo hashim,mi yangu macho tu.
 
kwa tabia hii hakuna haja ya gari yake kupewa namba maalumu 'TSS...' bora iwe T...AEK kama za sisi walalahoi tu. alitakiwa awe anamake difference.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…