Hasheem Thabit, kumbuka nyumbani ule mema ya nchi

Nelson Masaduki

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2017
Posts
346
Reaction score
380
Hasheem Thabeet ni Mtanzania aliyezaliwa tarehe 16 February 1987. Ni mchezaji wa mpira wa kikapu ambaye ni hazina kwa Taifa letu. Licha ya muda wake mwingi kuutumia nchini Marekani katika timu ya Memphis Grizzlies, endapo Thabeet ataamua kuendeleza kipaji chake kwa kuwainua vijana wa Tanzania, anaweza kutengeneza timu nzuri ya mpira wa kikapu hapa nchini. Kama ilivyo kwa wenzake waliopewa viwanja, naamini Hasheem Thabeet anaweza pia kupata ardhi nzuri mkoani Dodoma na kuangusha mjengo wa maana. Mtaa wa Wanamichezo ukajijenga mkoani Dodoma.

Nelson,
SUA-Morogoro
 
Hv hii post ya muda gan maan ni kitambo sana jamaa hayupo nba yupo kwny developing system huko japan aicee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu umejuaje kama Hana ardhi Dom ? Hashim dodoma ni mwenyeji hivyo kuna uwezekano ardhi anayo tayari , au mbaka iwe ya kupewa
 
Kaa hukohuko ule unavyokula ukirudi huku utangoja miaka 40 kutambuliwa mchango wako na kupata zawadi ambayo wakati huo itakuwa haina thamani. Tino angezawadiwa kiasi hicho wakati wake angetajirika. Juzi amepewa sawa na mshahara wa wiki mbili wa mtoaji.
 
Huyo mtu wenu alishafeli,kachezea shilingi chooni.
Niliwahi kumsikiliza alirudi likizo,alikuwa anaongea Kiswahili cha Marekani ,nilishangaa sana,nilimuona ana majivuno,limbukeni,...Kitaalamu tunasema Hajitambui(sijui sasa) Ingekuwa ni maajabu makubwa kama angeendelea kutamba kwenye kile kilichomuinua,kwa kiwango kile cha ushamba!
 
Unamzungumzia huyu aliyemaliza Jitegemee? Aliyekwenda US ukubwani na sasa akija anaigiza kusahau kiswahili? Hapo kichwani kuna tatizo! Miaka yote hiyo hujawahi kugundua kwamba mtu huyu hajitambui? Linganisha na Dikembe Mutombo wa DRC.
 
Kama demotion ni mafanikio basi huyu dogo kafanikiwa..🙂
 
Jamaa hawezi nyanyuka tena alishafika kwenye peak ilitakiwa amantain peak ila yeye alidrop.
 
Yeye mwenyewe sasa hivi anahitaji kuiñuliwa kipaji chake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…