Mpap Ndabhit
JF-Expert Member
- Jan 15, 2014
- 331
- 416
Mbeya shida ya maji ni kubwa kuliko wanasiasa wanavyojua. Labda Kipindupindu ndiyo kitawaumbua. Pamoja na miradi mikubwa Mbunge Tulia ameileta Mbeya ukweli mradi wa maji umechelewa. Watu watakuwa wamekufa na Kipindupindu.
Suala la Kipindupindu Mbeya halihitaji utafiti. Jibu liko wazi Mbeya wanakunywa na kutumia maji ya vyooni. Ni kawaida maji kutotoka kwenye mabomba zaidi hata ya mwezi. Maji yanayotumika ni maji ya visima katika nyumba zilizosongamana.
Hayo ndiyo wananchi wanakunywa, kuoshea vyombo, nk. Jiji Zima la Mbeya. Mtu alikusudia kuchimba shimo la choo.sasa wakati anajipanga kukamilisha choo majirani wanatumia Kwa matumizi ya nyumbani. Rangi ya maji hayo ni njano.
Kabla ya kufungia visima ningeomba tatueni changamoto hii ya maji najua Kipindupindu kitaishia hapo. Naomba kuwasilisha.
Suala la Kipindupindu Mbeya halihitaji utafiti. Jibu liko wazi Mbeya wanakunywa na kutumia maji ya vyooni. Ni kawaida maji kutotoka kwenye mabomba zaidi hata ya mwezi. Maji yanayotumika ni maji ya visima katika nyumba zilizosongamana.
Hayo ndiyo wananchi wanakunywa, kuoshea vyombo, nk. Jiji Zima la Mbeya. Mtu alikusudia kuchimba shimo la choo.sasa wakati anajipanga kukamilisha choo majirani wanatumia Kwa matumizi ya nyumbani. Rangi ya maji hayo ni njano.
Kabla ya kufungia visima ningeomba tatueni changamoto hii ya maji najua Kipindupindu kitaishia hapo. Naomba kuwasilisha.