Leo baada ya kutoka church nikaamua kupita kwa wadogo zangu wawili kuwasalimia na kuwatakia amani ya bwana. Katika kupiga piga stori tukafikia kuulizana hivi maziko yetu yatakiwa wapi tukifa leo?
Wadogo zangu hawa wakadai ikitokea wamefariki basi niwazike hapa hapa mjini na nisije thubutu kupeleka maiti zao mkoa/kijijini kwa Maziko. Nilipofika home nikaamua kumuuliza waifu, nae kang'aka eti ikitokea nije nimzike hapa hapa mjini, kijijini hataki kupasikia.
Nimepigwa na butwaa, hata maiti hazitaki kurudi mkoa!