Hata mimi nashangaa

Asprin, Msanii, Teamo hebu nisaidieni hapo penye maneno mekundu :confused2:

The Finest, kama nimekuelewa hiyo ndo confession yenyewe. sasa anataka nini tena? si ameshasema ukweli wake? Inabidi asome between the lines
 

Hapo mwanamke alitakiwa agangamale haswa ili ajue kushoto wapi na kulia wapi kuliko yeye kutoka nduki au naona kasahau yale maneno "Nitakuvumilia kwa shida na Raha siku zote za maisha yangu" well najua inauma lakini lazima uwe na moyo wa ujasiri to face the facts
 

heheheheh........
 
Alipoingia kwenye ndoa ilibidi ajue hayo yooooooooooooote na kuamua kuwa atasamehe.

FP kuna haya maneno inabidi mwanamke ayakumbuke wakati alipokuwa akiyatamka "Nachukua............uwe mume wangu wa ndoa naahaidi kukuheshimu,kukuvumilia katika shida na raha siku zote za maisha yangu
 

Mpwa mambo yetu yale natumaini unakumbuka:becky::becky::becky: usije sema ukuniambia
 
Jamaa aliiba mke wa mtu na katika harakati za kukwepa fumanizi, akajikuta amepaki chupi ya kike. Katika hali ya kawaida ukimaliza tendo la ndoa unatupa kondom, inakuwaje uirudishie kwenye begi? Lazma kulikuwapo na purukushani huko alipokuwa huyo Jamaa.
 
huyu mwanaume nae alitakiwa awe na aibu kidogo maana just 4months? anagalau wengine tuliyajua baada ya miaka. Huyu binti arudi tu, sa hizi huyo kimada anashangilia ushindi!



wanawake cc tuna roho za ajabu sana, hivi unaona raha gani mwenzio akiteseka kwa maumivu?...kama kweli ni kamada wake anatakiwa amwage haraka iwezekanavyo, hamfai kabisa, ataendelea kumuharibia na kumuharibia....mie kwasasa labda kimada atambikie kwao au waamue waondoke wakaanzishe maisha yao mapya na kimada wake....kimada hajanitoa ndani bado labda enzi zile kwasasa....puuuu.
 
Nyamayao?Muhudumu wa hotel alipaki nguo zake kwa kuwa alipata ugonjwa wa ghafla sana akiwa hotelini hadi kushindwa kupark nguo zake?!uongo aliotumia ni wa level ndogo sana hauitaji tena maswali ya zaidi kupata majibu,,lkn mshauri mdogo wako ajipe moyo arudi kwa mumewe na umpe uhalisia na experience ya maisha ya ndoa,hata kama imetokea mapema or late kosa ni kosa awe mvumilivu ajipange namna ya kuhandle ndoa yake there is no Mr perfect neither Ms.Hata barabara huwa zina kona,atulie aombe Mungu kwani kila aliyeko kwenye ndoa anapita kny mapito kwa style yake ila kuta zinaficha siri.
 


ndugu yangu weee na mie jana ckuweza kuongelea sana hili jambo, ndoa yangu jana ilikuwa honeymoon nikautumia muda vilivyo, c unajua ni wa mcmu....lol, nikitulia jioni nitamcal niongee nae kirefu zaidi.
 
Alipoingia kwenye ndoa ilibidi ajue hayo yooooooooooooote na kuamua kuwa atasamehe.


wakati mwingine namuelewa huyu mdogo wangu, akili zake bado zinamtuma kubembelezwa tu, c ndoa bado changa so ana mapenzi ya wakati ule akibembelezwa kama mchumba? ngoja tumpe muda kwenye hili game atakuja kuwa sterling tu...hili game mchezo?
 
FP kuna haya maneno inabidi mwanamke ayakumbuke wakati alipokuwa akiyatamka "Nachukua............uwe mume wangu wa ndoa naahaidi kukuheshimu,kukuvumilia katika shida na raha siku zote za maisha yangu

ha haaaaaaaaaaaaaaa, I still remember those words. na ndo yananifanya nimwombe sana Mungu anisaidie isije ikafikia siku nisiyakumbuke na kuamua kujitwisha kilicho changu
 

:confused2::tape:
 

Hamna wanachokosa, hata uwape mgongo bado atatoka tu nje ya ndoa. cha msingi ni wanawake kutambua kwamba hao waume zetu ndivyo walivyo toka enzi hizo za mababu so cha msingi mdada ukiolewa uwe mvumilivu na kusali kwa sana ili mungu aingilie kati ndoa yako la sivyo mhhhhhhh!!!
 
wakati mwingine namuelewa huyu mdogo wangu, akili zake bado zinamtuma kubembelezwa tu, c ndoa bado changa so ana mapenzi ya wakati ule akibembelezwa kama mchumba? ngoja tumpe muda kwenye hili game atakuja kuwa sterling tu...hili game mchezo?

ha haaaaaaaaaa, Nyamayao, atuulize sisi tuliokomaa huko. Mambo ya kubembelezwa yaliisha aliposema "I do". sasa inatakiwa awe ngangari kulinda hiyo ndoa......................
Ni kweli hili game siyo mchezo!
 

unachosema ni kweli kabisa,
kumuomba Mungu ndio sahihi zaidi...
na baada ya hapo...focus! obviously kuna watoto na kama hawapo watakuja sometime in future,
let focus be on takin care of those angels and hayo mengine Mungu atasaidia....
 
ha haaaaaaaaaa, Nyamayao, atuulize sisi tuliokomaa huko. Mambo ya kubembelezwa yaliisha aliposema "I do". sasa inatakiwa awe ngangari kulinda hiyo ndoa......................
Ni kweli hili game siyo mchezo!

haaa huyu bado yupo kule kwenye sms za i mic u, i love soo much, gnite my sweetheart...haaaa asubirie atakapoambiwa wewe mama kachala....haaa
 
unachosema ni kweli kabisa,
kumuomba Mungu ndio sahihi zaidi...
na baada ya hapo...focus! obviously kuna watoto na kama hawapo watakuja sometime in future,
let focus be on takin care of those angels and hayo mengine Mungu atasaidia....

kuna wakati nilipokuwa na kasheshe zangu kwenye ndoa, nilikuwa nikiwaangalia watoto wangu wazuri nasema wacha nikae kae kanipa watoto watamu, yani yeye hayupo tena akilini mwangu ila wanangu....sasa na huyu cku moja atafikia huku tu.
 
ndugu yangu weee na mie jana ckuweza kuongelea sana hili jambo, ndoa yangu jana ilikuwa honeymoon nikautumia muda vilivyo, c unajua ni wa mcmu....lol, nikitulia jioni nitamcal niongee nae kirefu zaidi.

Utakuwa umefanya la maana, kwa sababu ndoa bado changa hana alijualo na umwambie kuna mengi zaidi ajifunze jinsi ya kuyavumulia na si kukurupuka na kuondoka. Inavyoonyesha huyo mumewe kweli alikuwa na nyumba ndogo ila hiyo nyumba ndogo ilikuwa inalengo baya ilikuwa inataka kuharibu kama huyo mwanaume anasoma koment hapa hiyo nyumba ndogo haifai kabisa aachane nayo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…