Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,421
Watu wengi sana ambao hawajaoa au kuolewa huwa wanafikiria zaidi kuhusu kumpata mtu anayefaa. Wanawake ndio wako kwenye kifungo hiki zaidi. Jamii imewaambia kwamba, umri unavyoongezeka na nafasi yao ya kuolewa na pia kuzaa watoto inakuwa finyu zaidi. Kwa bahati mbaya wameamini hivyo.
Lakini nijuavyo mimi, maumbile hayana kuoana, wala hayana kitu kinachoitwa watoto wa nje ya ndoa. Najua kauli yangu hii itawakera wale wanaoamini katika dini zao hizi za mapokeo, lakini huo ndio ukweli wenyewe.
Lakini naamini watakubaliana na mimi kwamba, hata waanzilishi wa hizi kubwa, sio wote ambao walioa. Ingekuwa kuoa ni suala la maumbile, basi nao wangeoa pia. Ukweli ni kwamba kuoa au kuolewa ni suala la binadamu zaidi. Hivyo uoe au usiolewe ukweli kwamba utabaki kuwa binadamu na kutimiza kile kilichokuleta duniani, hauwezi kuondoka.
Lakini nijuavyo mimi, maumbile hayana kuoana, wala hayana kitu kinachoitwa watoto wa nje ya ndoa. Najua kauli yangu hii itawakera wale wanaoamini katika dini zao hizi za mapokeo, lakini huo ndio ukweli wenyewe.
Lakini naamini watakubaliana na mimi kwamba, hata waanzilishi wa hizi kubwa, sio wote ambao walioa. Ingekuwa kuoa ni suala la maumbile, basi nao wangeoa pia. Ukweli ni kwamba kuoa au kuolewa ni suala la binadamu zaidi. Hivyo uoe au usiolewe ukweli kwamba utabaki kuwa binadamu na kutimiza kile kilichokuleta duniani, hauwezi kuondoka.