Hata wanapokosea tunawasifu? Embu jiulize, ukoo wenu ni lini mtafaidi keki ya Taifa?

Hata wanapokosea tunawasifu? Embu jiulize, ukoo wenu ni lini mtafaidi keki ya Taifa?

Trable

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2023
Posts
1,781
Reaction score
3,288
Kuna mazingira wananchi wametengenezewa na CCM kuwalazimu wao kusifia tu kusifia tu hata kama yeye na ukoo wao wote ni masikini wa kutupwa na hawana mbele wala nyuma

CCM, yenyewe imejitengenezea ulaji wa keki ya Taifa kupitia familia chache sana ambazo ndizo zitaendelea kuneemeka na mema yote ya nchi mpaka kiama, kama tu wananchi wataendelea kuwa watumwa na wajinga wa kusifia hata pasipositahili

Mtindo huu unaanza kuuona hata kwenye vyama vya upinzani! Viongozi vyama vya upinzani nao wako bize kuandaa ukoloni uleule, hawataki kuachia madaraka na kuwapa aengine, wako bize kuandalia watoto wao kukava nafasi zao na ama watu wa Karibu nao!

Tangu nimekuwa na akili, nasikia majina yale yale ya ukoo uleule iliyowahi kuwa kwenye vitengo mhimu na mpaka leo iko vilevile familia zile zile ambazo mpaka leo ndio wanakula keki ya Taifa

Majina yale yale ndiyo yanayoteuliwa kurudi kwenye ulaji ule ule na wananchi wanasifia! Hivi watanzania mmelogwa?

Unajiuliza, kwani wao wamesoma shule zipi ambazo jamii nyingine haikusoma huko?

Mitoto mingine ya hao mabwanyenye, haina hata shule, na ndiyo hiyoinayosababishia hasara nchi yetu, usimamizi mbovu na haiguswi, wanaoguswa ni wale tu ambao kwa bahati mbaya waliingia hizo nafasi licha ya ukweli kwamba, wamefanya vizuri lakini kwa kuwa sio miongoni mwa hizo familia pendwa na viongozi wa ccm wanatemwa tu

kila ukifungua mitandao ya kijamii, unakutana na Habari za walioteuliwa kushika nyadhifa, unakutana na majina yale yale ya miaka na miaka na ama watoto wa walewale waliowahi kuwa viongozi

Namna hii, unajiuliza, kwani hakuna watu wengine nao wakapewa hizo nafasi ili nao kama watanzania waile keki?

kwenye ajira za malipo mazuri bado mambo ni yale yale, mtoto wa masikini ambaye hana mtu huko, ajira za namna hiyo atazisikia tu kwenye bomba, bila kujitambua na yeye anaanza kusifia! Huo ni upumbavu kabisa!

Unasifia wenzako wanavyoishi kukwapua utajiri wa nchi yako na wewe kuishi kama mtumwa kwenye nchi yako? Ujinga
 
Acha ujinga kijana. Sio CCM wenyewe waliojitengenezea ulaji, hata wapinzani nao wale wajanja wajanja wamo katika ulaji. Sema wewe na familia yako ndio hawapo huko unaposema kuna ulaji. Ila wengine ndugu zetu ni wapinzani wa mchongo na wapo kwenye ulaji kama kawa, wanalamba asali na kusaza bila kujali chawa wao huku mitaani.

Na bado sisi wapambe wao tuliobaki mtaani tunawasifu hao wapinzani na kuwaona ni wakombozi wetu wa baadae.

Ila hili au hao wewe haujawaona?
 

Attachments

  • images (6).jpeg
    images (6).jpeg
    34 KB · Views: 1
  • images (8).jpeg
    images (8).jpeg
    26.4 KB · Views: 1
Acha ujinga kijana. Sio CCM wenyewe waliojitengenezea ulaji, hata wapinzani nao wale wajanja wajanja wamo katika ulaji. Sema wewe na familia yako ndio hawapo huko unaposema kuna ulaji. Ila wengine ndugu zetu ni wapinzani wa mchongo na wapo kwenye ulaji kama kawa, japo sisi tuliobaki mtaani hao wapinzani tunawasifu na kuwaona ni wakombozi wetu wa baadae.

Ila hili au hao wewe haujawaona?
Mkuu!

Andiko hili linagusa wengi sana, nyie mlio kwenye huo ulaji endeleeni, kama siyo watoto wenu, basi wajukuu wenu watafurushwa tu
 
Mkuu!

Andiko hili linagusa wengi sana, nyie mlio kwenye huo ulaji endeleeni, kama siyo watoto wenu, basi wajukuu wenu watafurushwa tu
Mkuu ulichoandika kina uhalisia fulani, lkn ulichokosea ni pale ulipoitaja CCM pekee na wakati wapinzani wa vyama vyote vikuu wamo katika huo ulaji ila haukuwataja.

Wapinzani wametengeneza chawa kibao, mitaani na mitandaoni bila kuwasaidia chochote zaidi ya kuwatumia kwenye maandamano, na kuandika andika ujinga mitandaoni, ila linapokuja swala la masilahi wapinzani hao wanakula wao tu na familia zao huku wakijifanya kuwasahau chawa wao waliopo humu mitandaoni na mitaani. Hilo ndio tatizo.

Ila kwa namna fulani nakubaliana na ulichoandika, japo ulikwepesha kwepesha hapo kwa walamba asali wengine.
 
Kama ukoo wenyewe wanaishia f2 tu, .hao hata keki ya loan board wataiskia kwenye redio.
National cake mpaka upige shule haswa na uwe na distinction performance hapo unaweza ukaajiriwa hata BOT
 
Kama ukoo wenyewe wanaishia f2 tu, .hao hata keki ya loan board wataiskia kwenye redio.
National cake mpaka upige shule haswa na uwe na distinction performance hapo unaweza ukaajiriwa hata BOT
Sawa Mkuu, hao wanaoila keki yetu wamefika wapi? Mbona kuna vilaza kibao huko na ndio zinazosababishia hasara nchi yetu?
 
Sawa Mkuu, hao wanaoila keki yetu wamefika wapi? Mbona kuna vilaza kibao huko na ndio zinazosababishia hasara nchi yetu?
We endelea kupuuza Elimu huko tunakoenda hata walinzi wa minara watatakiwa wawe na Shahada ya kwanza
 
Acha ujinga kijana. Sio CCM wenyewe waliojitengenezea ulaji, hata wapinzani nao wale wajanja wajanja wamo katika ulaji. Sema wewe na familia yako ndio hawapo huko unaposema kuna ulaji. Ila wengine ndugu zetu ni wapinzani wa mchongo na wapo kwenye ulaji kama kawa, wanalamba asali na kusaza bila kujali chawa wao huku mitaani.

Na bado sisi wapambe wao tuliobaki mtaani tunawasifu hao wapinzani na kuwaona ni wakombozi wetu wa baadae.

Ila hili au hao wewe haujawaona?
Kama ulivyomsifu Sabaya, Makonda na yule tapeli wa Chato?
 
Wananchi wengi ni wajinga sana!

Nyie wajinga ndio mlikuwa mnamsifia dhalimu wakati kaleta lugha ya kupinga kila kitu. Leo hii hamko kwenye ulaji ndio mnaishia kuleta uchuro.
 
Back
Top Bottom