Hati ya Muungano ilichomwa moto mwaka 1970-ilibaki majivu tu yaliyotunzwa kama kumbukumbu

Hati ya Muungano ilichomwa moto mwaka 1970-ilibaki majivu tu yaliyotunzwa kama kumbukumbu

MdogoWenu

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2009
Posts
554
Reaction score
916
Ilitokea hivi.

Mwaka 1970, Nyerere aliittoa askari waende kupigana kuikomboa Msumbiji. Baadhi ya wanajeshi wakachukuliwa kutoka Zanzibar.

Wakati meli ilioywahukua imekaribia kisiwa cha Chumbe ndio Karume akataarifiwa kwamba wanaenda Msumbiji. Kumbe taarifa ile Karume ndiyo kwanza anaambiwa na hakujua kuwa kuna askari wazanzibar wanachukuliwa kwenda Msumbiji. Nyerere alifanya vile akijua kwamba yeye ni Amiri Jeshi Mkuu na ulinzi ni suala la Muungano.

Karume alipohabarishwa dakika ileile akaamuru meli irudi na wanajeshi wale wasiende.

Nyerere akasikia kwamba wamerudishwa na hivyo akamuita Karume ikulu ya Dar. Jibu la Karume likawa kwamba wale ni wazanzibar na wakiuawa vitani ni lazima ataulizwa yeye na si Nyerere na hivyo alipaswwa ajue kabla ya yote.

Kwa jibu Nyerere akapoa. Lakini mzozo haukupoa. Ndipo Karume akaitisha Baraza la Mapinduzi kueleza hali ile. Mzee Nassor Moyo hupenda sana kuisimulia hadithi hii na hata mimi hadi hapa sijasem kitu kipya.

Baraza likaamua kwamba Mambo kadhaa yasiwe ya muungano kama vile ulinzi, sarafu na kadhaa ambayo Moyo hupenda kuyakumbusha na hakuna aliywahi kuyakanusha.

Hivyo, Baraza likaona kwamba waende wote na Karume kumvaa Nyerere na kumueleza hayo.


Walipofika Ikulu ya Dar, hakika siku hiyo wapo waliodhani Muungano utavunjika. Kabla kikao hakijaanza, Karume akamuomba Mwalimu faili lenye Hati ya Muungano. Nyerere akiamini hakuna kitakachotokea akampa mara moja Karume, huku wengne wote wakisubiri mkutano na hawajui kinatokea nini kati ya Nyerere na Karume.

Karume alippokea faili lile akaenda nje ya ofsi ya Rais, akachagua chumba ambacho atakuwa peke yake hakuna mwingine, na huko aakafanya kitu hiki ambacho wengi hawajui lakini wachache wameanza kukijua.

Karume alichofanya huko peke yake, akachukua ile hati ya Muungano, akachukua kiberiti na akaichoma moto akahakikisha imebaki majivu.

Kisha akachukua majivu yale akayaweka vizuri kwenye mkoba akamrusishia Mwalimu akimueleza hivi "Mwalimu, nakuletea haya majivu kwa sababu nimeamua kuichoma hii Hati ya Muungano kwa sababu hawa watu sasa wameanza kutuhoji haya mambo".

Mwalimu akawa hana la kufanya, bali akaamua kuyatuza majivu yale kwenye plastic bag na juu yake kukawa na bendera ya Tanzania.

Hiki ndicho kinachojulikana na wachache inabidi wengi wakijue pia.

Hivyo, piga ua, Hati ya Muungano haiwezi kupatikana kwani ilichomwa moto kwa namna ile. Ndiyo sababu ulikuwa ukileta hoja ya Muungano enzi za Mwalimu basi ni afadhali ukutane na jehenamu.

Hivyo, ni kweli kwamba jua liwake lisiwake, Hati ya Muungano haitapatakina milele, labda yale majivu yake na kama waliendelea kuytaunza.
 
Ni ajabu sana nyerere hakujua kuwa alikuwa ana deal na lumpeni. Hata hivyo alitakiwa awasiliane na makamu wake wa kwanza mwenye dhamana visiwa.alijua angekumbana na upinzani. Inasikitisha alitegemea gentle treatment! Unategemea nini zaidiya mavisasi.
 
mnaojifanya mnajua mnatusumbua mara abdul jumbe alikuwa na hati na alitafuta wanasheria wauvunje muungano huko UN mara 1970 umechomwa moto,nn tunatafuta!?
 
hivi kwanini Jumbe asiulizwe,si yupo hapa mjimwema njia ya kuelekea kimbiji?hapa hapa Dar.Tena angetupa mwanga wa kutosha juu ya huu muungano
 
aiseeeeee!! duuh! hata hivyo mimi binafsi sio umuhim saaaana wa hyo hati kwani ni dhahili hata CCM wanajua kabisa kuwa inabidi kuwepo na muungano wakishirikisho ndio tutaenda sawa! kwani kwa hali ya sasa Zanzibar haiwezi kukubali kutokuwa na rais eti awe makamu wa kwanza wa muungano kama Karume alivyokubali! ugumu wa shirikisho unatoka wapii!? ukifuatilia mambo haya sana unaweza kutoa matusi kwa watu wazima na hasa wanao jiita wasomi! YAANI WANAJIDHALILISHA HADI WATOTO WANAGUNDUA!!
 
Kwa karume anaweza jamaa zilikua zinamtosha mwenyewe yule
 
Hati ya Muungano 'ilipotea' Ikulu ya Zanzibar na kupelekwa Ughaibuni..
 
Sasa ile aliyoonyesha katibu mkuu kiongozi bwana Ombeni Sefue kwa wanahabari ni ipi?
 
Hadithi nzuri hiyo…kwani kulikuwa na nakala moja tu…mbona tuliambiwa nyingine ilipelekwa UN…..hapa ufahamu wangu walao zingekuwa 3..moja huenda ilikuwa Tanganyika..moja Zanzibar na nyingine UN New York
Sasa kusema ilikuwa hiyo moja tu basi upande wa Zanzibar hawakupewa haki..na je UN hawakupeleka kitu chochote nafiiri lazima wapeleke kuthibitisha huo Muungano
 
Back
Top Bottom