Hatimae leo nimetua Toronto Canada

Hatimae leo nimetua Toronto Canada

Myahudi Jr II

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2016
Posts
6,816
Reaction score
8,809
Habari Watanzania Wenzangu, Naamini zoezi la Sensa linaendelea hapo nyumbani....

Walisema Wahenga Mungu hamtupi Mja wake, mimi ni mmoja wa watu wanaoamini mafanikio ya mbali na nyumbani, si kwasababu nyumbani hapafai, hapana bali ni imani ambayo ukiwa mbali na nyumbani akili inafanya kazi mara 100 zaidi kwasababu hakuna wa kukusaidia.

Baada ya miaka 6 Tangu kumaliza chuo kikuu nilianza harakati za kutafuta chimbo (CANADA or The US) kazi haikua nyepesi hadi mwaka 2021 ndipo Mwenyezi MUNGU muweza wa yote alipofungua milango yake nikafanikiwa kupata Visa ya CANADA (Study Permit) ya miaka 2

kwanini CANADA na si US

1. Canada wanatoa miaka 3 ya kufanya kazi baada ya kumaliza masomo (PGWP) baada ya miaka 2 ya PGWP unaweza kuomba PR kwakua tayari utakua na kitu wanayotaka inaitwa (Canadian Experience)

2. Kwasasa Canada ndi kimbilio la wahamiaji wengi (China, Wahind, Japanese,Nigerians) woote hawa kila siku wanatua toronto.

Kwanza Mh AGREY MWANRI unatakiwa uende Ukafanye kitubio kwa Mungu wako kufananisha TORONTO na vitu vya ajabu.

Ndugu zangu, Wazungu wameendelea, hawa jamaa ni balaa lingine sio wenzetu asee.

Baada ya kutua hapa nimethibitisha WATANGANYIKA HATUONGE KINGEREZA, TUNATAMKA MANENO YA KINGEREZA, kingine hawa jamaa wanakula uchafu asee, yaani hapa natamani nipate Ugali nyama choma eti unakutana na piza*/baga yaa shida tupu.

20220822_070315.jpg
20220822_185019.jpg
20220822_185042.jpg
20220823_012102.jpg



CC; Daby harakati za kitambo sana
 
Back
Top Bottom