Hatimae mh. Jenista Mhagama anena kuhusu ajira za walimu wapya

Hatimae mh. Jenista Mhagama anena kuhusu ajira za walimu wapya

CALMAN

Senior Member
Joined
May 23, 2013
Posts
190
Reaction score
54
Kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia kutoka kwa wakuu wa shule waliokuwa na kikao na Naibu waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi hapo juzi Mkoani Iringa, mhe. Jennista Muhagama naibu wa wizara hiyo alionekana kuwasihi sana wakuu hao wa shule kuwa wavumilivu na moyo wa subira kwa upungufu wa walimu uliopo na kuahidi ahadi iliyokuwa na mashaka ndani yake kuwa, nanukuu "labda ajira mpya za walimu zitatoka April mosi" kutokana na ukosefu wa fedha za malipo kwaajiri ya walimu hao wa ajira mpya kwa kuwa serikali imeelekeza fedha nyingi kwenye malipo ya utekelezaji wa programu ya BRN na fedha nyingine zitatumika kwa malipo wa wajumbe wa bunge la katiba.


Kwa mtazamo huu naitafakari serikali nakuiona ni yakusadikika kwa kushindwa kutumia kila fungu la fedha kulingana na wizara husika, lakini pia mhe Majaliwa TAMISEMI kama kiongozi aliuhadaa umma kwa kutosema ukweli na kudanganya kuwa ajira zitatoka mapema january kwa kuajiri walimu 26,000 wa shule za msingi na sekondari hii ni taarifa yake akiwa Morogoro na Maafisa Elimu. Wahanga wa ajira mpya tunapaswa kuchukua hatua kuelekea Ofisi za wizara ya Elimu Dsm nipo tayari kuongoza maandamano hayo tuwasiliane kupitia namba +255 682 893 290

------------------------


Hatimae Mh. Jenista Mhagama anena kuhusu ajira za walimu wapya.



Kutokana na mengi kuongelewa kuhusu ajira mpya za walimu,ambapo awali waheshimiwa mbalimbali wa wizara husika walikwisha kutoa matamko tofauti ambayo mpaka sasa hayajatimia,naye naibu waziri wa elimu mafunzo na ufundi mh.Jenista Muhagama aamua kunena.



Awali mwaka jana mwishoni, Naibu waziri anayeshughulikia Elimu (TAMISEMI),Kassim Majaliwa,alinukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari na kusema ajira hizo zinategemewa kutoka mwezi wa kwanza 2014,ambapo kauli hiyo haikutimia mpaka sasa mwezi wa pili na hakutoa tena tamko lolote juu ya hilo.




Mwishoni wa mwezi wa kwanza katibu wa Elimu Mafunzo na Ufundi, Prof. Sifuni Mchome,naye alitoa taarifa kupitia kituo kimoja cha TV,yaani EATV,akisema kila kitu tayari na wanasubiri kutangaza tu hizo ajira mpya za walimu,ambapo mpaka sasa pia kauli hiyo bado haijatimia maana ni kama wiki tatu zimeshapita.




Tarehe 11/02/2014,kulikuwa na kikao ambacho kilihusisha wadau mbalimbali wa elimu yaani walimu na wadau wengine wa sekta hiyo.Kikao hicho kiliendeshwa ndani ya ukumbi wa shule ya sekondari ya Lugalo iliyopo manispaa ya Iringa.




Kikao hicho ambacho mgeni rasmi alikuwa mh. Jenista Mhagama kama naibu waziri Elimu,aliweza kusikiliza mengi yanayoikumba sekta ya elimu.Pamoja na mambo mengi yaliyozungumziwa,wadau walitaka kufahamu ajira mpya za walimu zitatoka lini.




Kwa mujibu wa naibu waziri huyo alisema kuwa wale wote wanaosubiri ajira hizo,majina yatatoka tarehe 1/04/2014 kwasababu kwa sasa serikali haina fedha na nyingi zimetumika kwenye maswala mbalimbali ya kitaifa lakini kubwa ni maswala ya katiba mpya.






Kwa maelezo zaidi unaweza ukawasiliana na mdau yeyote wa elimu aliyehudhuria kikao hicho cha tarehe 11/02/2014,shule ya sekondari Lugalo iliyopo manispaa ya Iringa mjini.

Regional-Administration-and-Local-Government-Deputy-Minister-Education-Kassim-Majaliwa.jpg



Naibu waziri anayeshughulikia Elimu (TAMISEMI),Kassim Majaliwa.


Prof.-Mchome.jpg



Profesa Sifuni Mchome,Katibu Mkuu Wizara ya Elimu



11.jpg

Naibu Waziri wa Elimu Mafunzo na Ufundi,Jenista Mhagama

source; Save Societies


 
Inakera msomi kukaa unasubiria ajira serikalini baadala ya kujipanga kwa kujiajiri.
 
inakera sana lakini wazo la kusema wahanga wa ajira mpya waandamane kwenda wizarani siliungi mkono
 
vuteni subira mtaajiriwa tu maandamano si suluhu ya tatizo hilo.sina uhakika kama kuna haki ya mhitimu kuajiriwa na serikali vinginevyo migomo ingekuwa kila siku!¡!!!!!!!!!!
 
Acha uongo Mr,wakuu wa shule ndio wapewe taarifa embu toa nonsense zko
 
serikali mbona mnashinswa kutoa ajira kwa walimu toka mwaka jana hadi leo........................ ? Wengi walimu walijua leo nd' siku nzuri kwao kumbe sivyo jamani mwenye fununu yoyote tujuze baxi
 
Taarifa nlizozipata kutoka kwenye chanzo mwaka huu walimu wa sayansi na hesabu ndo watakao ajiriwa tu wamasomo ya arts mpaka budget ipite yaani mwezi wa 7
 
Muandamane kwani kuna mkataba mliingia na serikali kuwa mkimaliza mnaajiriwa.
 
jamb mbona unakatisha watu tamb ya kuajiriwa!
 
Inakera msomi kukaa unasubiria ajira serikalini baadala ya kujipanga kwa kujiajiri.

Kwa taaluma aliyoisomea(ualimu) we unafkr angejiajirije labda? afungue tuition center? apige tempo? "tumejenga tabia kisha tabia zikatujenga"
 
Back
Top Bottom