Hatimae Serikali imekubali kwamba hakuna kitu kinaitwa kipaji maalumu

Hatimae Serikali imekubali kwamba hakuna kitu kinaitwa kipaji maalumu

The Assassin

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2018
Posts
4,942
Reaction score
20,077
Hatimae Serikali imeanza kutoka kwenye zama za ujinga za kutenga shule kadhaa na kuziita za vipaji maalumu.

Serikali kusitisha mfumo wa kutangaza mwanafunzi wa kwanza sijui wa mwisho ni mwanzo mwema wa kuhama kutoka kwenye ujinga/zama za giza na kwenda kwenye mwanga na kuleta mapinduzi kwenye mfumo wetu wa elimu.

Wewe mtoto mmoja anasoma Kitopeni secondary school ambako hakuna walimu wala miundombinu ya kutosha ya kujifunzia, mwingine anasoma Feza ambako kuna kila miundombinu ya kujifunza, halafu uwape mtihani sawa halafu useme wa Feza ana kipaji maalumu na yule wa kitopeni hana kipaji chochote, ni zero brain, hakuna kitu.

Kwa mfumo wetu hata ukiiba mitihani ukapata A masomo yote wewe una kipaji maalumu.

Nimefurahi kuona Serikali inaanza kufanya kazi, kuanza kubadilisha mfumo wetu wa elimu uliopitwa na wakati.
 
Serikali ilikuwa inakosea sana kuita wanaofauli kwa maksi nyingi kuwa ni vipaji maalumu wakati wote walisomea hicho hicho kitu, wakawa wanawatengea shule walizoziita vipaji maalumu. Vipaji maalumu huwa ni vichache na ni unique kwa mwanafunzi, na mara nyingi havifundishwi na havina shule speciffic
 
Hatimae serikali imeanza kutoka kwenye zama za ujinga za kutenge shule kadhaa na kuziita za vipaji maalumu.

Serikali kusitisha mfumo wa kutangaza mwanafunzi wa kwanza sijui wa mwisho ni mwanzo mwema w kuhama kutoka kwenye ujinga/zama za giza na kwenda kwenye mwanga na kuleta mapinduzi kwenye mfumo wetu wa elimu.

Wewe mtoto mmoja anasoma kitopeni secondary school ambako hakuna walimu wala miundombinu ya kutosha ya kujifunzia, mwingine anasoma Feza ambako kuna kila miundombinu ya kujifunza, halafu uwape mtihani sawa halafu useme wa Feza ana kipaji maalumu na yule wa kitopeni hana kipaji chochote, ni zero brain, hakuna kitu.

Kwa mfumo wetu hata ukiiba mitihani ukapata A masomo yote wewe una kipaji maalumu.

Nimefurahi kuona serikali inaanza kufanya kazi, kuanza kubadilisha mfumo wetu wa elimu uliopitwa na wakati.

Sasa tofauti kati ya hiyo kitopeni na feza kaileta nani? Kwanini serikali isikubali makosa yake yenyewe na kurekebisha miundombinu yake iwe bora kwa wanafunzi kusomea. Hiyo hoja imekaa dhahiri kwamba serikali haiko tayari kukubali makosa yake yenyewe na kutaka kujificha kwenye msingi wa kuficha matokeo. Ni aibu kwamba everytime shule za private ndo zinafanya vizuri
 
Wewe mtoto mmoja anasoma kitopeni secondary school ambako hakuna walimu wala miundombinu ya kutosha ya kujifunzia, mwingine anasoma Feza ambako kuna kila miundombinu ya kujifunza, halafu uwape mtihani sawa halafu useme wa Feza ana kipaji maalumu na yule wa kitopeni hana kipaji chochote, ni zero brain, hakuna kitu.
Kama walioko madarakani ndiyo thinking capacity yao imefikia hapo usitegemee nchi kupiga hatua
 
Sasa tofauti kati ya hiyo kitopeni na feza kaileta nani? Kwanini serikali isikubali makosa yake yenyewe na kurekebisha miundombinu yake iwe bora kwa wanafunzi kusomea. Hiyo hoja imekaa dhahiri kwamba serikali haiko tayari kukubali makosa yake yenyewe na kutaka kujificha kwenye msingi wa kuficha matokeo. Ni aibu kwamba everytime shule za private ndo zinafanya vizuri
Mkuu hoja yako inafikirisha sana.
Zamani, shule binafsi zilikuwa zinaonekana duni kuliko za serikali.
Wazazi wengi walipenda watoto wao wasome katika shule za serikali maana zilikuwa na miundombinu bora, na walimu bora na wakutosha.

Kutokana na uzembe katika kusimamia shule za serikali, hali imebadilika. Wazazi wenye uwezo wanaona ni afadhali kupeleka watoto wao katika shule binafsi.
 
.
Umetoa hoja nyepesi kwa ishu nzito.
.
Kama wanafunzi wako mazingira tofauti kwanini wanafanya mtihani mmoja?? Kwanini wasingetungiwa mitihani tofauti?
.
Tuache double standards na kujifurahisha kisiasa.
 
Kwa hoja yako serikali inajificha kwenye shamba la karanga.

Kitopeni Sec kukosa walimu na miundombinu ya Feza Sec ni uzembe wa serikali yenyewe!

Serikali yako ilishaweka kigezo cha ufaulu ili mtoto ajiunge na shule za bweni za serikali kwa kidato cha kwanza.

Matokeo wanafunzi 50,475 wamekidhi na nafasi ni 4,224 pekee kwa kuwa shule hizo ni 38 tu.

article-1264092-081D0A9F000005DC-144_468x3392.jpg
Bahati mbaya Ostrich Effect haijawahi kuwa suluhisho.
 
Sasa tofauti kati ya hiyo kitopeni na feza kaileta nani? Kwanini serikali isikubali makosa yake yenyewe na kurekebisha miundombinu yake iwe bora kwa wanafunzi kusomea. Hiyo hoja imekaa dhahiri kwamba serikali haiko tayari kukubali makosa yake yenyewe na kutaka kujificha kwenye msingi wa kuficha matokeo. Ni aibu kwamba everytime shule za private ndo zinafanya vizuri
Mkuu shule za private zisikie tuu....hamna kitu mule sema watanzania wengi ni mbumbumbu kwa kudhani shule zinafaulisha kwa kutozwa mahela mengi. Mwisho wa siku mahela hayohayo yananunua mitihani kuwafurahisha.
In short wanajitekenya na kujicheka wenyewe.
Fuatilieni maendeleo ya hao wanafunzi hadi vyuoni then mtapata majibu.
 
Mkuu shule za private zisikie tuu....hamna kitu mule sema watanzania wengi ni mbumbumbu kwa kudhani shule zinafaulisha kwa kutozwa mahela mengi. Mwisho wa siku mahela hayohayo yananunua mitihani kuwafurahisha.
In short wanajitekenya na kujicheka wenyewe.
Fuatilieni maendeleo ya hao wanafunzi hadi vyuoni then mtapata majibu.

acha uwongo bwana, mtihani wa form 4 au six kama hujafundishwa vizuri utafeli tu hata upewe maswali yanayotoka kwenye mtihani.
 
Kama hauko kwenye sector ya elimu utanibishia AU ukikua utaelewa.

niwafanyishe interview wanafunzi zaidi ya 2000 wajitokeze, nichukue wanafunzi 100 bora kati yao, niwafundishe vizuri kwa walimu wanaolipwa vizuri,mahitaji yote muhimu wapate kwa wakati halafu waje wafanye vizuri kwenye mitihani yao unasema wameiba mtihani, ukiamini hivyo utakuwa ni tahira na elimu yako uliyonayo.

wewe na akiliy
 
Back
Top Bottom