Hatimaye Kaseja atemwa timu ya Tanzania kwenda CECAFA

Olmost

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2014
Posts
337
Reaction score
441
KIKOSI CHA MWISHO CHA KILIMANJARO STARS

Benchi la ufundi la timu ya taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ limetaja orodha ya mwisho ya wachezaji 22 wanaoondoka kuelekea nchini Uganda kwaajili ya michuano ya CECAFA Challenge inayotarajiwa kuanza Desemba 7, 2019.

Kwenye orodha hiyo, majina 11 yamekatwa kutoka kwenye kikosi cha awali ili kukidhi idadi inayohitajika ambapo miongoni mwa waliokatwa ni golikipa Juma Kaseja, ambaye taarifa zinaeleza anasumbuliwa na majeraha.

Pia mshambuliaji wa Ik Frej Taby ya nchini Sweden Rashid Chambo ameongezwa kwenye kikosi licha ya kuwa hakutajwa katika kikosi cha awali.

Wachezaji wanaokwenda Uganda ni.

1. Metacha Mnata – Yanga SC
2. Aishi Manula – Simba SC.
3. David Kisu – Gor Mahia.
4. Juma Abdul – Yanga SC
5. Nickson Kibabage – Difaa El Jadid, Morocco.
6. Gadiel Michael – Simba SC.
7. Mwaita Gereza – Kagera Sugar.
8. Mohamed Hussein – Simba SC.
9. Bakari Mwamnyeto – Coastal Union.
10. Kelvin Yondan – Yanga SC
11. Baraka Majogoro – Polisi Tanzania.
12. Jonas Mkude – Simba SC.
13. Zawadi Mauya – Kagera Sugar.
14. Mzamiru Yassin – Simba SC
15. Hassan Dilunga – Simba SC.
16. Ditram Nchimbi – Polisi Tanzania
17. Cleoface Mkandala – Tanzania Prisons.
18. Paul Nonga – Lipuli FC
19. Miraji Athuman – Simba SC.
20. Eliuter Mpepo – Buldcon, Zambia.
21. Lucas Kikoti – Namungo FC.
22. Rashid Chambo – Ik Frej Taby, Sweden.

WALIOKATWA:
Wachezaji 11 waliokuwa wametajwa katika kikosi cha awali na sasa hawamo ni pamoja na

1. Juma Kaseja - KMC
2. Salum Kimenya – Tanzania Prisons.
3. Abdulmajid Mangalo – Biashara United.
4. Fred Tangalu – Lipuli FC
5. Idd Seleman – Azam FC.
6. Kelvin John – Football House.
7. Jaffary Kibaya – Mtibwa Sugar.
8. Salum Abubakar – Azam FC.
9. Eliud Ambokile – TP Mazembe, DR Congo.
10. Yusuph Mhilu – Kagera Sugar.
11. Shaban Chilunda – Azam FC
 
Kila lakher ila mshambuliaji shaban chilunda na Eliud ambukile
 
Hii timu haitafika mbali. Imechaguliwa kubalansi makundi tu. Metacha mfano anamiwekaje benchi kaseja kwa performance ya kaseja timu ya taifa? Yange yenyewe metacha ni namba mbili.
 
Sasa huyu rashid anahusika vipi hapa?
 
Kwa kikosi hicho,hatufiki popote mtu aweke jiwe mi naweka 50 cash na demu wangu.
 
Hii timu haitafika mbali. Imechaguliwa kubalansi makundi tu. Metacha mfano anamiwekaje benchi kaseja kwa performance ya kaseja timu ya taifa? Yange yenyewe metacha ni namba mbili.
Hata KMC pale Kaseja ni namba mbili. Hii inamaliza ubishi kwamba baada ya Kaseja wa enzi za Simba, golikipa bora aliyefuatia ni Aishi Manila, kuanzia wa Azam hadi sasa wa Simba. Hakuna cha Kaseja wa KMC, Kakolanya wala Metacha, hajatokea mwingine zaidi ya Aishi, hata akiumia akapumzika bado ni Tanzania One
 
Salum Kimenya,sure boy, ambokile, chilunda duuuh
 
Kakolanya ana uwezo mkubwa kuliko Aishi, sema ndio hivyo tena misumari ina nafasi yake katika soka letu!
 
Ila
Ila Kakolanya ni namba nyingine muda unaenda kasi
 
Hii timu haitafika mbali. Imechaguliwa kubalansi makundi tu. Metacha mfano anamiwekaje benchi kaseja kwa performance ya kaseja timu ya taifa? Yange yenyewe metacha ni namba mbili.
Huu ushabiki maandazi
 
Hii timu haitafika mbali. Imechaguliwa kubalansi makundi tu. Metacha mfano anamiwekaje benchi kaseja kwa performance ya kaseja timu ya taifa? Yange yenyewe metacha ni namba mbili.
Jumapili tunapigwa na ZNZ kama kawaida...wachezaji wa Yanga na Simba hawajitumi kwenye haya mashindano bora wangechukuliwa wachezaji wa timu ndogo wakaonekane
Kwa kikosi hicho,hatufiki popote mtu aweke jiwe mi naweka 50 cash na demu wangu.
Hahahaha, naomba niungane nanyi ktk mtazamo huu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…