Dodoma moja
JF-Expert Member
- Jan 3, 2014
- 307
- 182
Victoria fm ya mjini Mwanza jana asubuhi kipindi cha matukio wameripoti kuwa wamefanya mahojiano na naibu waziri wa elimu Bw.Philip Mulugo kuhusu tuhuma zinazomkabili ambapo amesema hawezi kujiuzulu kwa kuogopa majungu ya vyama vya upinzani wanaopika uongo juu yake ili kuwika kisiasa.
]Mulugo amekanusha madai yote yaliyoandikwa na gazeti la Mwananchi na kudai kuwa kama kuna mwenye wasiwasi na elimu yake aende akamuoneshe vyeti vyake vya elimu ya sekondari hadi vya taaluma na chuo alichosoma.
SIJIUZULU KWA MAJUNGU YA WAPINZANI NI NAIBU WAZIRI WA ELIMU TANZANIA | MFUATILIAJI
Huyu alisema hajiuzulu, sasa yamemkuta...amefukuzwa!
Wakuu mzee wa division five(mulugo) hatimaye kang'oka rasmi kwenye baraza jipya la mawazir lililotangazwa na katibu mkuu kiongoz ikulu muda mfup uliopita. Pongezi kwake mkuu wa nchi kwa usikivu!!!
Ntazimiss sana pumba zake..
Huyu hakustahili kabisa kiutwa Waziri mdogo wa wizara ya elimu.
[video=youtube_share;e3BNegmIUKM]http://youtu.be/e3BNegmIUKM[/video]
Pamoja na kukubali ya kuwa Baraza bado lina mapungufu (la zamani na jipya), huyu mtu anayeitwa Mulugo alikuwa kitovu cha aibu na chanzo cha watanzania ulimwenguni kote kuona aibu hata kutamka hadharani kuhusu uraia wetu. Hiyo hotuba yake ilikuwa kwenye youtube na huku nilipo ilikuwa inatumiwa kila wakati kuonyesha kwa mshangao kuwa 'eti kuna nchi hapa duniani ambayo naibu Waziri wake wa ELIMU anatoa hotuba kama iliyoandikwa na kusomwa na mtoto wa darasa la tano'.
Kama huyo ndiye Naibu Waziri, wanafunzi wanaotoka kwenye taasisi za Elimu mbalimbali nchini mwetu watakuwa na viwango gani? Nilishangaa sana miaka ya mwanzoni mwa 2000 nilipokutana na mwanafunzi kutoka Tanzania aliyekuja huku kwa dhamira ya kutafuta Chuo cha kusoma baada ya 'kufanya vizuri sana kwenye mtihani wa kidato cha 6' aliposisitiza ya kuwa kisiwa cha Mafia hakipo Tanzania, na pili alisisitiza kwa kunihakikishia ya kuwa yeye anajua sana Jiographia, na Spain ni sehemu ya Marekani...
Sikuelewa maskini, kumbe halikuwa kosa lake. Maskini Tanzania yangu!
Serikali ya CCM ina vichekesho vya aina yake....Ngoja tuone..