malema 1989
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 1,319
- 520
Aula??????????
Ni sisi wenyewe ambao tunaendeleza fikra za ufisadi humu nchini. Maneno tunayoyatumia husaidia kufanya hivyo. Kwa mfano neno 'aula'. Hili neno linaashiria kuwa huko anakokwenda kuna 'kula'. je kazi au nafasi aliyokuwa nayo kabla ilikuwa haikidhi haja zake? ni vizuri kutumia neno 'kuteuliwa' kwa sababu huko anakokwenda atakuwa anatumikia nchi na si 'kula nchi'. Tabia ya 'kula nchi' tunaiona waziwazi jinsi viongozi wetu wanavyoila Tanzania.
mkuu samahani sana kwa kukukera, nilikuwa namaanisha kapandishwa cheo! maana sua alikuwa mhadhiri wa kawaida.
kweli mkuu!Ni sisi wenyewe ambao tunaendeleza fikra za ufisadi humu nchini. Maneno tunayoyatumia husaidia kufanya hivyo. Kwa mfano neno 'aula'. Hili neno linaashiria kuwa huko anakokwenda kuna 'kula'. je kazi au nafasi aliyokuwa nayo kabla ilikuwa haikidhi haja zake? ni vizuri kutumia neno 'kuteuliwa' kwa sababu huko anakokwenda atakuwa anatumikia nchi na si 'kula nchi'. Tabia ya 'kula nchi' tunaiona waziwazi jinsi viongozi wetu wanavyoila Tanzania.
wabongo bwana!!Ni sisi wenyewe ambao tunaendeleza fikra za ufisadi humu nchini. Maneno tunayoyatumia husaidia kufanya hivyo. Kwa mfano neno 'aula'. Hili neno linaashiria kuwa huko anakokwenda kuna 'kula'. je kazi au nafasi aliyokuwa nayo kabla ilikuwa haikidhi haja zake? ni vizuri kutumia neno 'kuteuliwa' kwa sababu huko anakokwenda atakuwa anatumikia nchi na si 'kula nchi'. Tabia ya 'kula nchi' tunaiona waziwazi jinsi viongozi wetu wanavyoila Tanzania.
wabongo bwana!!
hivi hujui aliyeleta uzi ni mtu wa aina gani!
mkuu kuna kitu kinaitwa rejesta... nadhani ulisoma katika somo la kiswahili!
kuula ina maana kwamba amefanikiwa katika jambo fulani.. wala hata haina maana mbaya!
Asante sana kwa kunipa 'somo'. Ndio, nimesoma Kiswahili kuanzia darasa la kwanza mwaka 1962 mpaka High School, nimekuwa mwalimu wa Kiswahili shule za sekondari na vyuo vikuu.
Naelewa sana maana ya matumizi ya misemo kuwakilisha maana fulani katika lugha. Kila mtu vilevile anaweza kutafsiri lugha jinsi anavyoiona, licha ya kwamba amesoma au la.
Hata hivyo nilichokuwa nakisema ni jinsi maatumizi ya maneno fulani yanavyodumisha, kukuza na kuendeleza mitazamo na hali tofauti katika jamii. Kwangu mimi, neno 'kuula' japokuwa linamaanisha kupata kitu fulani, kwa mantiki hii, kazi, hata hivyo linabeba hisia ndani yake kuwa huyo aliyepata kazi 'atakula' huko kazini kwake. Hapo neno 'kula' lina uzito zaidi ya kufanya kazi.
ila nakumbuka mwaka 1954 wakati tunaanzsha TANU, haya mambo hayakuwepo kabisa!