Hatimaye wachezaji wa soka,Cannavaro,Mgosi nk wasema Mwigulu chaguo lao

Hatimaye wachezaji wa soka,Cannavaro,Mgosi nk wasema Mwigulu chaguo lao

ukwelinauwazi

Member
Joined
Nov 24, 2014
Posts
71
Reaction score
91
CANNAVARO WA YANGA,JABU NA WACHEZAJI WENGI WAKUBWA WAMESEMA MWIGULU NCHEMBA NDIO CHAGUO LAO.

Source:Mwanaspoti
Toleo la leo Ukurasa wa 6.


WACHEZAJI mbalimbali wa soka wametoa maoni na mtazamo wao kuhusiana na wanachama wa vyama mbalimbali waliojitokeza na kutangaza nia kuwania urais wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa nchi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25.

Mpaka sasa ni zaidi ya wagombea kumi wametangaza nia za kugombea nafasi hiyo nyeti ambapo baadhi yao ni Edward Lowassa, Samuel Sitta, Steven Wasira, Mwigulu Nchemba, Mark Mwandosya, Sospeter Muhongo, Fredrick Sumaye, Dk. Khamis Kigwangala, Makongoro Nyerere, Lazaro Nyarandu, William Ngeleja na Titus Kamani wakati Bernard Membe anatarajia kutangaza nia kesho Jumamosi. Wote hao ni makada wa chama tawala cha CCM.

Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ yeye anamuunga mkono Mwigulu na kuwaomba Watanzania kumuunga mkono mgombea huyo ili aweze kuleta maendeleo nchini hasa kwenye sekta ya michezo.

Cannavaro alisema: “Mwigulu ni mmoja wa viongozi makini niliopata kuwaona nchini, ni kijana na tumekuwa tukiona uzalendo wake kwa kuwa na tabia ya kupenda nchi.

“Sina shaka na elimu yake, sina shaka na utendaji kazi wake. Naamini akipewa nafasi anaweza kufanya mabadiliko makubwa kwenye nchi na ndani ya miaka mitano na umasikini utapungua.”

Beki wa kulia wa Yanga, Juma Abdul alisema: “Nisingependa kuzungumza kwa niaba ya mtu yeyote, mimi binafsi nampa nafasi Mwigulu, ni mtu makini, anajua nini Tanzania inahitaji miaka inayokuja. Pia binafsi ninamuona kama kijana anayejua vijana wenzake wanapitia nini.”

Beki wa kushoto wa timu hiyo, Oscar Joshua alisema: “Tumekuwa na wakati mgumu kwenye nchi yetu. Wengi wetu ni masikini, hivyo muda huu ni muda wa kutafuta mabadiliko. Mheshimiwa Mwigulu anaweza kuwa mkombozi wetu kwenya hili janga la umasikini.

“Kama wachezaji wa soka tutaacha kulaumiwa na hiyo inatokana na mipango ya kuwekeza kwenye soka la vijana ambayo tumekuwa tukimsikia akilizungumzia.”

Kwa upande wa kipa wa Simba, Ivo Mapunda alisema: “Siwezi kusema nani anafaa kati ya wote waliotangaza nia zao ingawa nimebahatika kusikiliza hotuba zao kwa umakini mkubwa, kikubwa ambacho nakiona ni Kamati Kuu ya CCM kuchagua mtu watakayemsimamisha ambaye hana kashfa za ufisadi.

“Kwa asilimia kubwa wote waliotangaza nia wana kashfa za ufisadi, nchi yetu sasa inatakiwa iongozwe na rais ambaye ana sifa nzuri, ni msafi na hapo ndipo ninapoweza kusema ni rais gani anayeweza kutusaidia hata kwenye michezo, nimemsikiliza Profesa Muhongo kazungumzia michezo kwa asilimia ndogo sana wakati kwa nchi za wenzetu michezo ndiyo inayowaunganisha watu wa aina zote.”

Mussa Hassan ‘Mgosi’ alisema: “Rais Kikwete ni mpenda michezo ndio maana aliweza kubadilisha kwa kiasi fulani ila hawa wajao na kutangaza nia kwa kweli siwezi kuzungumzia lolote, tusubiri tuone na kuchagua tu atakayetufaa.Kufaa siyo kwenye michezo peke yake bali ni katika nyanja zote za maendeleo ya jamii nchini.”

Naye kiungo wa Simba, Jonas Mkude, alisema: “Mimi ninachosubiri ni kiongozi bora, yeyote atakayepitishwa naamini atakuwa na sifa. Kikubwa si jina, ila ni uwezo wa kufanya kazi.”
 
Kutokana maelezo ya wachezaji waliohojiwa, maoni ya ivo mapunda, Jonas mkude na Mgosi ni ya Ki-utuUzima sana!

Wale wengine hovyo kabsa, mbumbumbu wakubwa!
 
....haya wamwambie Malinzi ampishe mwigulu maana ndo wanayemtaka...
 
Back
Top Bottom