Hatimaye wanafunzi wote wa UDOM kitivo cha sayansi na jamii wamerudishwa nyumbani

Hatimaye wanafunzi wote wa UDOM kitivo cha sayansi na jamii wamerudishwa nyumbani

samirnasri

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
1,388
Reaction score
213
Kuna taarifa kuwa uongozi wa chuo kikuu cha dodoma umewafukuza wale ambao unawaita vinara wa mgomo ambao ulianza juzi chuoni hapo na kuwataka waondoke chuoni hapo kabla ya sa kumi na moja jioni jana. Uongozi wa UDOM mara nyingi umekuwa na roho nyepesi kufanya maamuzi ya kufukuza wanafunzi mapema mara tu unapotokea mgomo lengo likiwa ni kuwafurahisha viongozi wa chama na serikali. Ukweli ni kwamba madai ya wanafunzi ni ya msingi na ndio maana jana waziri wa elimu shukuru kawambwa aliridhia serikali kuwa na mpango wa mpito kuwawezesha wanafunzi hao kufanya mafunzo kwa vitendo. Naushauri uongozi wa udom kuacha tabia ya kufukuza fukuza wanafunzi wakidhani kwamba watamaliza migomo kwa namna hiyo.
 
Kuna taarifa kuwa uongozi wa chuo kikuu cha dodoma umewafukuza wale ambao unawaita vinara wa mgomo ambao ulianza juzi chuoni hapo na kuwataka waondoke chuoni hapo kabla ya sa kumi na moja jioni jana. Uongozi wa UDOM mara nyingi umekuwa na roho nyepesi kufanya maamuzi ya kufukuza wanafunzi mapema mara tu unapotokea mgomo lengo likiwa ni kuwafurahisha viongozi wa chama na serikali. Ukweli ni kwamba madai ya wanafunzi ni ya msingi na ndio maana jana waziri wa elimu shukuru kawambwa aliridhia serikali kuwa na mpango wa mpito kuwawezesha wanafunzi hao kufanya mafunzo kwa vitendo. Naushauri uongozi wa udom kuacha tabia ya kufukuza fukuza wanafunzi wakidhani kwamba watamaliza migomo kwa namna hiyo.
 
wanafunzi wote wametakiwa waondoke na wasionekane ifikapo saa nane mchana
 
Baada ya mgomo wa kudai field na kupelekea wanafunzi wapatao mia kusimamishwa masomo,leo chuo kikuu cha dodoma college ya social sciences imefungwa rasmi till further notice.
 
Uongozi wa chuo kikuu cha dodoma umekifunga chuo cha sayansi za jamii kuanzia leo na kuwataka wanafunzi wote wa college hiyo kuondoka chuoni hapo ndani ya masaa mawili kufuatia mgomo uliodumu kwa siku tatu.
 
VYUO VIMEKUWA VIPOLE MNO......! mtu asomeshwe kwa kukopeshwa, aandamane kwa kualazimisha aongezewe kiwango cha kukopeshwa,alete fujo kwa wale wanoendelea na masomo wasipojiunga na migomo yao.......!
AENDELEE KUVUMILIWA KISA UDHR (HAKI ZA BINADAMU) JE TUTAFIKA?
 
Mapambano ya kudai haki huwa yanaambatana na costs nyingi kama kifo,kufungwa jela,kupewa adhabu kali,kutengwa na jamii au kundi fulani la watu; lkn hayo yote huleta ukombozi wa haki kwa faida ya jamii nzima, hivyo nawapongeza vijana wa UDOM kwa mapambano na hakuna haja ya kujutia uamuzi mliochukua ktk kudai haki yenu na kufungwa kwa chuo ni sehemu ya harakati mfu za watawala kutaka kuwanyamazisha wanaodai haki zao!!!
Jiulize: kuna sababu zipi za msing zinajustify kuwa mgomo ukidum 3days chuo kifungwe?
 
Kuwafukuza wanafunzi na kufunga chuo sio suluhisho la matatizo lazima uongozi wa udom ifike mahali watumie busara sio kilg mgomo wao wanakimbilia kufukuza watu na kufunga chuo. Sasa wameshafunga vyuo viwili kile cha informatics na sasa cha social science. Kazi ipo.
 
Mabadiliko ya hayaji kwa kubembeleza bali kwa kudai. Unafikiri aliyeanzisha Peoples' power hakuwa na akili? Marekani unayoiona leo ni matokeo ya harakati za akina Malcom, Martin, Douglas na wengineo. Vijana tuamuke turudishe nchi pale Nyerere alipoiachia ili mtoto wa mkulima naye afaidike.
 
Kutokana na hali kua tete, taarifa niliyoipata hiv punde toka mdau wa UDOM, college ya social science na college ya humanities zimefungwa na wanachuo wamepewa masaa manne wawe wameondoka eneo la chuo
 
Back
Top Bottom