Hatimaye zee la propaganda @gentemycine aipigia salute yanga

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
Naaam, natoa kongole kwa huyo mwana Simba lialia mzee wa propaganda wakuitwa GENTAMYCINE.

Nimepitia baadhi ya nyuzi zake zilikua ni kuichokonoa yanga na maneno ya kejeri kwa kweli Kama una hasira unaweza kutukana kwenye kila nyuzi zake.

Huyu mwamba alisahau kabisa Kama Simba wamesajili saidoo ntibazonkiza aka Babu wa bujumbura na hakuona kabisa Kama Simba wamemuongezea inonga mkataba.

Sikuona uzi wowote au pongezi zozote kutoka kwake zikiisifia Simba namna gani wamesajiri usajili mpya lakini mwamba kapiga kimya tu na alikua bize na feitoto pamoja na kusambaza propaganda za uongo utadhani analipwa ili apush agenda

Siyo huyo tu Kuna makolo wengine toka Juzi walikua wanaandika Mambo ya feitoto na yanga wakiamini kuwa feisali anaibeba yanga

Kilichotokea Jana pale uwanja wa mkapa hawaamini macho yao kuwa feisal siyo kitu Bali yanga ni dubwasha kubwa lenye professional players Ina maana kuwa no feisali no problem.

Mwamba GENTAMYCINE Leo kwa maandishi kakiri kuwa yanga ni Bora, ndyooooooo yanga ni bora japo WAKULUNGWA wanambeza wakiamini Kuna mtu kashika simu yake nakumuandikia mazuri kuhusu yanga bila yeye kujua.

NB. This is football Jambo zuri sifia acha kufanya Mambo yakihisia, au kuleta Yale Mambo yale huipendi yanga lakini unaibetia unapata hela.
 
Hivi Genta una ID ngapi?
 
Huyo ni Saidoo alipokuwa kwetu walimwita Mzee. Kwao kawa kijana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…