Hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwa kijana wa Buguruni

BM X6
Hapo unapimwa reasoning capacity yako. Rudi uwaambie Hakuna kumpangishia dogo nyumba ya gharama kubwa ilihali Hana uzoefu na kazi, means baada ya miezi 6 atashindwa kujilipia Kodi. Mtafutie dogo chumba Cha elfu 50, then umfungulie biashara ya kuuza nguo za mitumba especially ya kike huku ukimfanyia close monitoring.

Baada ya mwaka mmoja mfungulie kwa matakwa yake biashara ya pili ambayo yeye binafsi atamuajiri kijana lakini wewe utaendelea kuwa mshauri na msimazi Mkuu.
 
Sorry my chief iam a man.
Yap ile kugeuza na kuchanganya hao wanawake kidogo mantiki imepotea, hata ule uzito wa hoja ya kuomba ushauri kuhusu huyo kijana imekua nyepesi sana.
Ooh, Jina lako limenichanganya,..kuhusu Story yeah kweli hilo nimeliona, coz watu hawajikiti tena kwenye hoja ilivyonifanya nianzishe Uzi wao wanataka tu niendelee na simulizi
 
Ooh, Jina lako limenichanganya,..kuhusu Story yeah kweli hilo nimeliona, coz watu hawajikiti tena kwenye hoja ilivyonifanya nianzishe Uzi wao wanataka tu niendelee na simulizi
Lakini tuongee tu ukweli ndugu yangu kweli hatma ya maisha yako ipo kwa huyo kijana kweli kama ulivyosema kwenye kichwa cha mada na vile ulivyo malizia kweli?

Bora hata ungesema kule ofisini pale ndio kuna changamoto haswa kama ni kweli lakini.
 
[mention]BM 6X [/mention] please be serious, hii story naomba kwa niaba ya wanaforum uimalizie, hapo sio mwisho tushakuwa walevi tayari
Acha tuone likizo yangu ya job ikiisha mambo yatakuaje huko Ofisini maana hadi Sasa hivi nipo njia panda sijajua niamue lipi

Halafu na Mzee nae Hata hajamaliza mwezi tangu ameondoka, so wacha tuone itakuaje akirudi Bongo kwasababu hapa ndio nipo mikakati ya kufanya zoezi lake, So let us wait and [emoji102]
 
Jamani njooni
 
Lakini tuongee tu ukweli ndugu yangu kweli hatma ya maisha yako ipo kwa huyo kijana kweli kama ulivyosema kwenye kichwa cha mada na vile ulivyo malizia kweli?
Bora hata ungesema kule ofisini pale ndio kuna changamoto haswa kama ni kweli lakini.
Yeah, kwasababu ndoto yangu ni kufanya Biashara so nikifeli kwenye huu mtihani wa Mzee ni kama ndoto zangu zimeishia hapo japokuwa sijajua Maamuzi yake atakayochukua baada ya kufeli

Kuhusu kazi ni kweli Lakini huko hata nikiacha kazi haitaniuma sana kama kufeli mtihani wa Mzee, Japokuwa naombea vyote nivi handle vizuri
 
Sawa lakini sidhani.na hiyo....nguo za mitumba ya especially ya kike....ndio gani hizo. Au unamaanisha mtumba na special?
 
Mtihani namba moja

Muite mama mueleze ukweli wote kuhusu wewe na binti yake akiamua uendelee na Kazi sawa na akisema Kazi Basi sawa.

Kuingia kwenye ndoa na mtu ambae hujamridhia na yupo unaempenda ndoa itakuwa ndoano, pesa au Mali ni vitu vyakupita kamwe usidanganyike navyo.

Baki na mpenzi wako aliyesimama na wewe pale ambapo ulishindwa
 
yeap sahihi kabisaa asiwe na tamaa ya kfnya ivo ilimradi nae apewe mtaji no apange chmba kikbwa biashara ya mtumba
 
vipi mama akimwambia mzee khs yanayoendelea na mzee ajw kma waish na mwanamkee
 
Very nice story! If truly the story based on really life here is my advice kutokana na nilivyoelewa.

Awali mzee alikwambia sio kila mtu anaeingia kwenye biashara anafanikiwa, wengi na wanafelishwa na kupuuza baadhi ya vitu.
Ni wazi kabisa BM unawasiwasi na vigezo vya kumfungulia kijana biashara livyokupa mzee moja wapo ni; aweze kujilipia kodi baada ya miezi sita isiyopungua 100,000 kwa mwezi.
Kwa maisha ya kawaida kodi hio ni kubwa kwa mtu ambae hana kipato cha kueleweka Hususani kwa kijana ambae umepewa task ya kumfungulia biashara na kumsimamia isimame


Unashauriwa Kodi ya nyumba isizidi 20% ya kipato chako per month. Hivyo, kama kodi ni 100,000 basi kijana umpatie business inayoweza kuingiza faida isiyopungua 500,000 kwa mwezi.

Hivyo, usipuuze swala la hilo. Kama unaona gharama hio ya kodi ni kubwa na itakusababishia kurisk mtaji mkubwa mwanzoni basi mtafutie kijana nyumba ya gharama ya chini ukiwa na malengo kumuamishia kwenye nyumba ya gharama 100,000 na kuendelea endapo biashara itaenda vizuri baada ya miezi 6. Lkn pia mzee afahamishwe hilo baadae ikiwa tayari biashara imesimama.



USISAHAU KUNITUMIA NAMBA YA CARYN PM NIKAFOSI KING MWANANGU BM [emoji846][emoji846]
 
Story ina mafundisho ila imenifikirisha sana baadhi ya mambo, mfano unawezaje kukumbuka kila neno katika sentensi wakati wa mazungumzo yenu na mzee, caryn, annie, accountant, mama?

Inanifanya nihoji uhalisia (ukweli) wake.
 
Ni true story mkuu, labda Mashaka yako yapo sehemu gani ya story?
Sio true story mkuu, kuna loopholes nyingi kwenye hii story yako lakini si busara kuyaweka hapa..

Ila hongera sana, unajua kuandika na kuunganisha matukio..
 
PStory ina mafundisho ila imenifikirisha sana baadhi ya mambo, mfano unawezaje kukumbuka kila neno katika sentensi wakati wa mazungumzo yenu na mzee, caryn, annie, accountant, mama?

Inanifanya nihoji uhalisia (ukweli) wake.
Haina uhalisia wowote. Kuna mambo mengi ya kuhoji na yapo wazi ila sijui kwanini wengi hawajayaona.

Mfano mdogo tu; jamaa anasema kaileta story humu kwasababu anajua mzee aliyetoa mtihani hataweza kuiona sababu yeye si mtumiaji wa JamiiForums, lakini vipi kuhusu huyo mwanae Caryn? Vipi kubuzu Mama na mwanae Accountant? Je nao hakuwafikiria kwamba wanaweza kuona na kujua kinachoendelea?

Caryn ni teenager, kwa umri wake nadhani anapaswa kuwa shule na sio boss wa kampuni eti ndiye anashikilia nafasi ya baba aliyesafiri. Kwa mazingira tunayoyajua kwa watanzania hapa napo kuna walakini, lakini pia ujengaji hoja wa Caryn sio wa hawa teenager tunaowajua.

Story itakavyoendelea ni jamaa atakubali kuacha kazi kule kwenye kampuni anayofanya kazi then abaki na Annie lakini atajikuta kwenye mtihani mwingine wa kupendwa na Caryn.

Zingatia hapo aliposema amesisitizwa atembelee mara kwa mara kwa mzee..
 
Mzee mbona hakuna mtihani hapo, hilo suala ulilopewa ni jepesi tu, biashara zipo kibao,

Wasiwasi wangu mimi ni ukifanikiwa mzee akakuona uko smart akaamua ili akukabidhi biashara umuoe binti yake hapo ndio kwenye NTITI,
Huyo annie wako usimuache karma itakutafuna.

Pambania biashara, dogo atoboe, upate biashara yako uepukane na mitihani ya ofisini, madhari akili yako inasema ACCOUNTANT sio mwanamke wa kuoa, shikilia hapo hapo, ndoa ni zaidi ya UTAMU WA KITANDANI

ukikwama sehemu usisite kunicheki.
Stori yako kama ya fix hivi halafu kuna kaukweli kwa mbali.

Karibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…