Hatua za awali Injini Automatic Transmission ikikataa kuwaka!

Hatua za awali Injini Automatic Transmission ikikataa kuwaka!

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Juzi kuna mteja alituita kuwa gari yake aliipaki na kuingia kwenye supermarket kupata mahitaji yake. Ila baada ya kurudi kwenye gari haikuwaka kabisa, ingawa taa zilikuwa zinawaka, radio inafanya kazi wiper zinafanya kazi ila stator motor ilikuwa haigoti kabisa.

Tukatuma fundi wetu kwenda kuangalia na kweli naye akasema diagnostics inahitajiwa ambayo asingeweza kuifanya pale kwenye parking lot, hivyo tukapeleka tow truck (breakdown kinyumbani) yetu kulivuta gari lile. Huwa tunachaji dola 100 kwa towing services. Baada ya kuvuta gari lile na kulifikisha kwenye karakana yetu, likafanya kazi kama kawaida bila matengezeo yoyote!

Tukagundua kuwa inawezekana ile switch ya parking ilikuwa haikushika sawasawa kwa vile magari yaenye automatic transmission huwa hayastart iwapo transmission haiko kwenye P au N. Ili gari lile liwekwe sawa kabla ya kubebwa na tow truck, ilibidi liwekwe kwenye neutral halafu lisukumwe hadi kwenye jaw za tow truck, na process hiyo ndiyo iliyotatua tatizo lote.

Ushauri wangu sasa: Ukipata kadhia ya namna hiyo na gari yako, jaribu kuhamishahamisha stick ya auto-transmission kati ya P-R-N-R-P kabla ya kujaribu kustart tena. Inaweza kukusaidia sana kuondoa kero na vile vile kukupunguzia gharama za kutafuta mafundi.

Kich: Certified ASE Consultant
 
Kwa uzoefu wangu hapo alitakiwa ajaribu kuipush ikiwa ipo kwenye gear ili self-starter ijarbu kushtuka ikiwa labda imekwama baadhi ya gar tatzo Hilo hujitokeza na pili Kuna gari zikichemka ukizima ukitaka kuwasha Tena ni mtihani hvyo tumia maji kumwagia sehemu ya selfu then ipush kidogo ikiwa kwenye gear alafu jarbu kuwasha
 
Kwa uzoefu wangu hapo alitakiwa ajaribu kuipush ikiwa ipo kwenye gear ili self-starter ijarbu kushtuka ikiwa labda imekwama baadhi ya gar tatzo Hilo hujitokeza na pili Kuna gari zikichemka ukizima ukitaka kuwasha Tena ni mtihani hvyo tumia maji kumwagia sehemu ya selfu then ipush kidogo ikiwa kwenye gear alafu jarbu kuwasha
Hapana; utaharibu gearbox yako haraka sana ukifanya mambo ya namna hiyo. Autotransmission zina kiburi sana, ukizichezea zinakunyoosha.
 
Niliwahi kuoata tatizo hili, gari lilikuwa linasumbua kuwaka kwenye P lakini nikishusha kwenye N linawaka, nilitengeneza baada ya siku 2.
 
Back
Top Bottom