Joshydama upo sahihi kabisa lakini kwa scenario ya huyu ndugu, Kuna technicalities za vipengele vitakavyozungumzia makato ya gharama zitakazotumika kufanya ukarabati.
Kwanza kwa asili ya makubaliano Kama haya, ningependa kukushauri kuwa Ni vyema mngekubaliana Na mpangaji wako kuwa akukate asilimia kadhaa katika kodi mpaka hiyo m3 itakapoisha, Mfano Kama kodi Ni 500000, basi awe anakulipa angalau 200000 kila mwezi.
Lakini pia, embu angalia huo ukarabati Ni kwa manufaa ya nani, Na siku yeye akihama je, unaweza nufaika Na huo ukarabati?, Na hata kwa kipindi hiki cha mkataba wewe mwenye nyumba unanufaika vipi Na huo ukarabati?, hii itasaidia kukufanya uwe Na maamuzi sahihi maana wengine hutumia ujanja huo Ili kulipa gharama kidogo.
Kingine, angalia kodi ya mwezi, itaweza kulipa gharama za pesa iliyotumika kufanya ukarabati kwa miezi mingapi?, Mfano gharama za ukarabati Ni M3, alafu kodi Ni laki 1, Ina maana hapo utaanza kupokea kodi baada ya miaka miwili Na miezi sita, ambayo Ni muda mrefu Sana kitu ambacho mpangaji anaweza kuwa amemaliza mkataba wake Na usiambulie chochote.
Lakini cha zaidi kwenye mkataba wenu kuwepo Na kipengele cha kumbana mpangaji kuwa Na upangaji wa muda mrefu, angalau kuanzia miaka miwili.
Haya niliyoyasema nimekisia kulingana na maelezo yako kuwa finyu, lakini naamini yanaweza kukupa mwanga.
Note: Mkataba Ni jambo la kisheria,Na Ni jambo la kitaaluma, Ni vizuri ukamlipa wakili angalau hata Kati ya 30000-50000 Ili mkataba wako uwe salama kwa pande zote mbili, maana atakupa na ushauri zaidi.
Tafuta wakili aliye jirani yako.