saidoo25
JF-Expert Member
- Jul 4, 2022
- 624
- 1,456
MBUNGE wa Jimbo la Nyasa, Injinia Stella Martin Manyanya ameweka wazi kutoridhishwa na utekelezaji wa Mradi wa Bwawa la Kufua Umeme la Mwalimu Nyerere na kuweza wazi msimamo wake kuwa Tanzania lazima tujitambue na hatutaangalia sura ya mtu bali umeme upatikane Bwawa la Mwalimu Nyerere.
"Na hapa nauzungumzia Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, Tanzania lazima tujitambue kuna wakati tunaweza tukawa tuna malengo makubwa mazuri ambayo yametupa heshima katika nchi yetu halafu baadae kwa sababu moja ama nyingine kwa sababu labda uongozi mmoja haupo umekuja uongozi mwingine watu wengine wanaweza kufikia kujaribu tukuchezea kwa kutushauri tofauti ili tushindwe kwenda kule tulikotaka kwenda"
"Kwa sababu Mheshimiwa Rais amedhamiria na ametangaza hadharani nawaomba Wizara ya Nishati tafadhalini tusimuangushe Mh Rais wetu tuhakikishe mradi huu wote kwa pamoja tunashirikiana timu iliyoko sasa na hata ile iliyokuwa mwanzo kama kuna jambo ambalo wao wanalifahamu mshirikiane kuhakikisha kwamba tunaenda vizuri sisi hatuangalii sura mtu tunaangalia umeme upatikane katika Bwawa la Mwalimu Nyerere" amesema Stella Manyanya alipozungumza bungeni.
"Na hapa nauzungumzia Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, Tanzania lazima tujitambue kuna wakati tunaweza tukawa tuna malengo makubwa mazuri ambayo yametupa heshima katika nchi yetu halafu baadae kwa sababu moja ama nyingine kwa sababu labda uongozi mmoja haupo umekuja uongozi mwingine watu wengine wanaweza kufikia kujaribu tukuchezea kwa kutushauri tofauti ili tushindwe kwenda kule tulikotaka kwenda"
"Kwa sababu Mheshimiwa Rais amedhamiria na ametangaza hadharani nawaomba Wizara ya Nishati tafadhalini tusimuangushe Mh Rais wetu tuhakikishe mradi huu wote kwa pamoja tunashirikiana timu iliyoko sasa na hata ile iliyokuwa mwanzo kama kuna jambo ambalo wao wanalifahamu mshirikiane kuhakikisha kwamba tunaenda vizuri sisi hatuangalii sura mtu tunaangalia umeme upatikane katika Bwawa la Mwalimu Nyerere" amesema Stella Manyanya alipozungumza bungeni.