Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 324
- 649
SERIKALI HAINA UWEZO WA KUPUNGUZA HIZI BEI ZA MAFUTA?
Na Elius Ndabila
0768239284
Nimesoma bei mpya ambazo zinaongeza maumivu mara dufu kwa mtu wa chini. Nimesema zinaongeza maumivu kwa mwananchi wa Chini kwa kuwa natambua wengine wanaotumia sawa sawa kodi za wavuja jasho maumivu hayawafikii kisawasawa.
Bei ya mafuta iliyotangazwa leo lita Moja kwa Ileje itanunuliwa 3,381/=. Yaani ukiwa na 10,000/= ambayo ulikuwa unanunua Lita 5 , sasa utanunua lita 2.
Tafsiri yake ni kuwa asilimia kubwa ya vitu tunavyotumia ndani navyo vitapanda bei. Kwa mfano Chumvi, sukari, Sabuni, Saruji, Mafuta n.k vyote vitapanda bei. Hapa namba tutaisoma zaidi sisi tunaokula Kwa jasho letu, wanaokula Kwa jasho letu maumivi siyo makubwa.
Mwezi January niliwahi kuandika ili kuweza kukabiliana na changamoto ya hizi za bei serikali ingeweza kustisha baadhi ya miradi mipya mikubwa Kwa muda ili kumsaidia mwananchi wa chini. Lakini bahati mbaya machozi ya samaki yanaishia majini. Lakini ukweli hili lingefanyika bei hii isingefika huku kwa kuwa kuna tozo serikali ingeziondoka kwenye mafuta ili kupunguza mfumuko huu.
Vita hii ya uchumi, kila Taifa linapaswa kukabiliana nayo kwa namna linavyoona inafaa. Hatuna sababu ya kukopi mbinu za kivita kuwasaidia wananchi wetu.
Swali lingine ninalojiuliza ni kuwa tuliambiwa nchi ina stock ya mafuta. Sasa haya mafuta yanafanya nini kwenye stoku, Kwa nini yastolewe kuja kupunguza gharama hizi? Au nayo yanauzwa Kwa Tshs3,381/=?
Wabunge nyie ndio silaha pekee iliyobaki kuwatetea Wananchi na kuishauri serikali namna nzuri ya kukabiliana na changamoto hii. Kuna faida gani kujivunia kijenga miradi mikubwa inayotumia fedha nyingi kama unaowajengea hawanafuraha moyoni? Kuna faida gani kujivuna kujenga miradi mikubwa kama unaowajengea hawajui mchana wanakula nini? Tuanze kuwatengenezea kwanza furaha watu ndipo tuingie kwenye uwekezaji.
Furaha ya Wananchi ni kuona wanamudu bei ya vitu sokoni, wanamudu nauli za usafiri hapo ndipo wataongeza amani ya moyo. Mfumko huu usipodhibitiwa, tunaenda kuongeza wagonjwa wa vidonda vya tumbo, presha na magonjwa ya akili yanayosababishwa na msongo wa mawazo.
Na Elius Ndabila
0768239284
Nimesoma bei mpya ambazo zinaongeza maumivu mara dufu kwa mtu wa chini. Nimesema zinaongeza maumivu kwa mwananchi wa Chini kwa kuwa natambua wengine wanaotumia sawa sawa kodi za wavuja jasho maumivu hayawafikii kisawasawa.
Bei ya mafuta iliyotangazwa leo lita Moja kwa Ileje itanunuliwa 3,381/=. Yaani ukiwa na 10,000/= ambayo ulikuwa unanunua Lita 5 , sasa utanunua lita 2.
Tafsiri yake ni kuwa asilimia kubwa ya vitu tunavyotumia ndani navyo vitapanda bei. Kwa mfano Chumvi, sukari, Sabuni, Saruji, Mafuta n.k vyote vitapanda bei. Hapa namba tutaisoma zaidi sisi tunaokula Kwa jasho letu, wanaokula Kwa jasho letu maumivi siyo makubwa.
Mwezi January niliwahi kuandika ili kuweza kukabiliana na changamoto ya hizi za bei serikali ingeweza kustisha baadhi ya miradi mipya mikubwa Kwa muda ili kumsaidia mwananchi wa chini. Lakini bahati mbaya machozi ya samaki yanaishia majini. Lakini ukweli hili lingefanyika bei hii isingefika huku kwa kuwa kuna tozo serikali ingeziondoka kwenye mafuta ili kupunguza mfumuko huu.
Vita hii ya uchumi, kila Taifa linapaswa kukabiliana nayo kwa namna linavyoona inafaa. Hatuna sababu ya kukopi mbinu za kivita kuwasaidia wananchi wetu.
Swali lingine ninalojiuliza ni kuwa tuliambiwa nchi ina stock ya mafuta. Sasa haya mafuta yanafanya nini kwenye stoku, Kwa nini yastolewe kuja kupunguza gharama hizi? Au nayo yanauzwa Kwa Tshs3,381/=?
Wabunge nyie ndio silaha pekee iliyobaki kuwatetea Wananchi na kuishauri serikali namna nzuri ya kukabiliana na changamoto hii. Kuna faida gani kujivunia kijenga miradi mikubwa inayotumia fedha nyingi kama unaowajengea hawanafuraha moyoni? Kuna faida gani kujivuna kujenga miradi mikubwa kama unaowajengea hawajui mchana wanakula nini? Tuanze kuwatengenezea kwanza furaha watu ndipo tuingie kwenye uwekezaji.
Furaha ya Wananchi ni kuona wanamudu bei ya vitu sokoni, wanamudu nauli za usafiri hapo ndipo wataongeza amani ya moyo. Mfumko huu usipodhibitiwa, tunaenda kuongeza wagonjwa wa vidonda vya tumbo, presha na magonjwa ya akili yanayosababishwa na msongo wa mawazo.