Hawa jamaa ni waukweli au wapigaji..?

Hawa jamaa ni waukweli au wapigaji..?

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
14,747
Reaction score
24,250
Salaam kwako mkuu...
Katika pitapita zangu mtandaoni nimekutana na jamaa wanajiita KiKUU ni wauzaji wa bidhaa mtandaoni.

Nahitaji kununua bidhaa kwao, je, ni waaminifu au ndiyo wale wale, ukilipa umepigwa?
 
Sometimes yes sometimes no. Juzi kuna mfanyakazi mwenzangu kaagiza simu na ikamfikia.
 
Nilikuwa naagiza vitu vingi tu kwao mwaka jana na vyote vilifika salama, wana ofisi zao pale shoppers plaza mikocheni ndo nilikuwa naenda kupokelea pale though sijui kama wamehama or bado wapo. Kwa experience yangu nao ni waaminifu.
 
Wako real, ila wakati mwingi uwa wanachelewesha sana order za wateja na kosa kubwa walilonalo hawako makini kabisa ivo hujikuta wanachanganya mizigo.. unakuta mzigo A unakwenda B
 
Fernando Jr
Heading to work tomorrow
Lukanka
Wana free shipping hii imekaaje kwa kuletewa bidhaa yako, but naona bidhaa imeandikwa tshs 55,000/- ukiendelea kujaza details mwisho wanakupa bei nyingine labda tshs 78,500/-, nini maana yake hapo?
 
Fernando Jr
Heading to work tomorrow
Lukanka
Wana free shipping hii imekaaje kwa kuletewa bidhaa yako, but naona bidhaa imeandikwa tshs 55,000/- ukiendelea kujaza details mwisho wanakupa bei nyingine labda tshs 78,500/-, nini maana yake hapo?
Wanakuandikia mfano 1000 lakini kuanzia PCs 10, ukichukua chini ya hapo bei inakuwa zaidi ya 1000, na ukizidisha Pcs 10 bei inapungua pia yaani uwingi wako wakuchukua ndo unapunguziwa na ukichukua chini ya order walioandika bei inapanda
 
Salaam kwako mkuu...
Katika pitapita zangu mtandaoni nimekutana na jamaa wanajiita KiKUU ni wauzaji wa bidhaa mtandaoni.

Nahitaji kununua bidhaa kwao, je, ni waaminifu au ndiyo wale wale, ukilipa umepigwa?
Huduma zao kawaida tu kama ebay,amazon etc....agiza kitu ndani ya wiki unaletewa hadi nyumbani...Tatizo wabongo mnadhan kila kitu cha online ni Utapeli
 
Hiyo sometimes No tupe experience
Kuna mdau humu alileta uzi wake akiwa lalamikia 'hiyo ndiyo sometimes YES' (yaani ni matapeli)

Sometimes No, ni kama nilivyosema hapo kuwa kuna mfanyakazi mwenzangu aliagiza simu na kuipata.

Yes, muda mwingine ni matapeli. No, muda mwingine si matapeli, 50/50.
 
Kwa experiences zangu jamaa ni waaminifu sema wanachelewasha sana order zao, pili usidanganyike na picha
 
Unapokelea mikocheni plaza wakati kikuu wanakuletea mpaka ulipo au mikocheni ndio uliweka address yako
Nilikuwa naagiza vitu vingi tu kwao mwaka jana na vyote vilifika salama, wana ofisi zao pale shoppers plaza mikocheni ndo nilikuwa naenda kupokelea pale though sijui kama wamehama or bado wapo. Kwa experience yangu nao ni waaminifu.
 
Nilifanya nao niashara kama mara 4 hv, marabya mwisho walizingua na mpaka leo sijaupata mzigo wangu, kwenda pale kwa ofisi zao kisiwani masaki nlikutana na kidada kimoja kinamajibu kama choo, nikaachana nao, ingawa nilipanga kuwapeleka mahakamani badae nikapotezea
 
Kwa experiences zangu jamaa ni waaminifu sema wanachelewasha sana order zao, pili usidanganyike na picha
Kwenye huo mstari wa mwisho ndipo muhimu sana,sometime unaweza agiza mzigo kwa vile umevutiwa na picha but wanakuletea tofauti kabisa na ule wa kwenye picha.nadhan ni sababu ya out of stock
 
Unapokelea mikocheni plaza wakati kikuu wanakuletea mpaka ulipo au mikocheni ndio uliweka address yako
Ni maamuzi yako, ukitaka subiri uletewe ama ukiamua fuata ndo maana wakati unaweka order yako kuna mahala unachagua self pick ama home delivery. Self pick mzigo unafuata kwa office zao which was more convenient for me.
 
Kuna mdau humu alileta uzi wake akiwa lalamikia 'hiyo ndiyo sometimes YES' (yaani ni matapeli)

Sometimes No, ni kama nilivyosema hapo kuwa kuna mfanyakazi mwenzangu aliagiza simu na kuipata.

Yes, muda mwingine ni matapeli. No, muda mwingine si matapeli, 50/50.
Kikuu nimetumia alot of time SIO MATAPELI....Somestime its best kabla ya kutoa ushaur upate first hand experience kuliko kusikia ya watu
 
Kikuu nimetumia alot of time SIO MATAPELI....Somestime its best kabla ya kutoa ushaur upate first hand experience kuliko kusikia ya watu
Kuna mdau alileta hapa malalamiko juu ya kutapeliwa na Kikuu hiyo mosi, pili nimeshuhudia mfanyakazi mwenzangu akipokea mzigo wake kutoka Kikuu.

Unataka nitoe maelezo gani hapo?
 
Kuna mdau alileta hapa malalamiko juu ya kutapeliwa na Kikuu hiyo mosi, pili nimeshuhudia mfanyakazi mwenzangu akipokea mzigo wake kutoka Kikuu.

Unataka nitoe maelezo gani hapo?
Sasa huyo mdau una uhakika gan katapeliwa?? Na katapeliwa kwa njia gan? What is anataka kufanya Sabotage tu? Afu na wewe unasambaza eti sometimes Yes.
 
Sasa huyo mdau una uhakika gan katapeliwa?? Na katapeliwa kwa njia gan? What is anataka kufanya Sabotage tu? Afu na wewe unasambaza eti sometimes Yes.
Sasa nina uhakika gani kwamba wewe unachosema ni kweli?
 
Back
Top Bottom