Hawa wachezaji bora wa tff, ni umbumbu mwingine.

DREAMBOY

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
2,117
Reaction score
1,369
Salute!
Pamoja na Mimi kuwa mshabiki wa yanga sioni huo uchezaji bora wa msuva ,labda ufungaji. Pia hata huyo kichuya ni hovyo kabisa. Nakwambia hawa wachezaji wawili ni wabahatishaji tu, kubwa ni mbio. Mimi nilitarajia nimuone ndani:
Ibrahim Ajibu(Simba sc)
Haruna Niyonzima(Young Africans)
Yakub Mohammed(azam fc)
Jafari Mohammed(Toto Africans)
Abdulrahman Musa (Ruvu Shooting)
Mbaraka Yusuph(kagera sugar)
Aishi Manula(Azam fc)
Salum Abubakari( Azam fc)
Ikumbukwe huo ni mtazamo wangu ,mnisamehe kwa kweli, ila kwa kuwa majina yameshatoka ni ukweli usiopingika kuwa Haruna Niyonzima ndo bora.
Samahani naomba msnitukane maana kuna watu humu ni waja wa laana.
 
amesahaulika Yusuph Ndikumana(mbao fc)
 
Mchezaji bora ni Fakhi wa kagera Sugar tuu sababu uwepo wake uwanjani ulisababisha Mikia kufungwa Na kukata rufaa mpaka FiFa.
hawa ndo yanga nao wajua hawatukani, naskia alpanda bombardier kuja kujitetea mbele ya kamati
 
TFF wana vigezo vyao, ukizungumzia wachezaji wa timu zingine nje na Azam, Yanga na Simba
Hao wachezaji ni bora ndio lakini wamefikisha wapi timu zao??
Unataka kumpa uchezaji bora timu yake inashuka daraja

Wache wakapige kura tuone nani atakua bora
Lakini kwa upande wangu hawa watatu wamesaidia sana timu zao "Aishi Manula", " Niyonzima" na "Kichuya"
 
Zimbwe Jr,mchezaji pekee aliyecheza mechi zote za Simba ligi hii dk 90, ndiye mchezaji anayeongoza kwa kucheza dakika nyingi ligi hii kwa kiwango cha juu
 
Zimbe Jr,mchezaji pekee aliyecheza mechi zote za Simba ligi hii dk 90, ndiye mchezaji anayeongoza kwa kucheza dakika nyingi ligi hii kwa kiwango cha juu

Tshabalala = yes, kiwango cha juu mno
Kichuya = ver talented but not good enough this season
Niyonzima = yes, fantastic season
Msuva = Yes, consistently improving
Manula = Yes, ngumu kutokuwa mchezaji bora msimu huu
 
Zimbe Jr,mchezaji pekee aliyecheza mechi zote za Simba ligi hii dk 90, ndiye mchezaji anayeongoza kwa kucheza dakika nyingi ligi hii kwa kiwango cha juu
Huyo zimbe Jr kacheza mechi hizo zote sabab hapo mkiani, aka wowowo fc hakuna mbadala wake yaan wote ni kiwango kibovu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…