Hawa waimbaji wa injili mbona wana mapozi tata sana?

Sauti ya Injili wanayo nyimbo nzuri za zamani huwa nazimiss nikiwa out of their coverage na kwenye tunein hawapo mara nyingi nasikiliza kile kipindi cha Safina radio Arusha kinapigwa jpili nyimbo za zamani.

 
Barabara ya 13

Naupenda Sana wimbo wa Samsoni , palikiwa na mtu pamoja na katikati viumbe vyote vilivyoubwa binadamu kaumbika kuliko vyote.
Kuna yule mbaba ana sauti ya kwanza ya kike nilikuwa napenda aisee!

Basi nakumbuka dogo alikuwa haelewi pale wanapoimba 'ajitwike msalaba wake,anifuate' akawa anaimba anjige njige msalaba wake.....
 
Mkuu hapo ushamba wako wa kiroho jamaa yangu. Hujawahi sikia boringo/mziki wa dance, rap na rage?? Labda taarabugospo mimi ndiyo sijasikia.
Taarabu gospel ipo niliisikia nikachoka mwili na maini!!!
 
Watu hawaishiwi maneno kwani kwa mungu hawatakiwi watanashati? Don't judge the book by the look of it's cover
 
Hapa umenikumbusha mama, halfu enzi hizo tuna kaseti bhana, anasikiliza huku ana pika hahaha!!

Lakini hawa waimbaj wa siku hizi wana tutania aki ya Mungu
Hahaaa!!! Eti wanatutania!!
Unasikiliza wimbo unawaza hiki kitu gani sasa, wimbo si wimbo kelele sio kelele basi tafrani tu.
 
Hao siyo waimbaji ni wanatoa Sauti nzuri tu.kuimba Hawajui
 
Hapo kwenye malezi umenigusa,my sister nilishangaa home kwake kuna aina fulani tu ya gospel zinazopigwa, ukijumlisha na hizo gospel za zamani kama Tumaini,Mama Jusi,Buliankulu(sijui ndio inavyoandikwa) and of the sort, anasema 'hizi bongo flavour zenu sizitaki humu ndani kwangu'. Now i get it.
 
Ndio maana napenda sana kwaya kuliko waimbaji binafs

Waimbaji binafs nawakubali hawa
Ambwene Mwasongwe
Joshua Mlerwa
Shusho


Wengine wapiga hela tu
Yaani gospel imevamiwa acha kabisa, kuna hiyo moja niliiona mabinti wamevaa skin jeans alafu wanakata viuno hatari, nilipigwa na butwaa!!! Rose
Muhando nae full kukata viuno sasa sijui ndio vitu gani hivi.
 
Kuna yule mbaba ana sauti ya kwanza ya kike nilikuwa napenda asisee!

Basi nakumbuka dogo alikuwa haelewi pale wanapoimba 'ajitwike msalaba wake,anifuate' akawa anaimba anjige njige msalaba wake.....
Hahaha...ni kweli Ulyankulu sauti ya kwanza inaimbwa na mwanaume, ya pili ni wanawake wote

Nilishangaa sana kusikia wale waimbaji ni wakimbizi...ila Mungu aliwabariki sauti hadi wakaipaisha Tanzania.
 
Hahaha...ni kweli Ulyankulu sauti ya kwanza inaimbwa na mwanaume, ya pili ni wanawake wote

Nilishangaa sana kusikia wale waimbaji ni wakimbizi...ila Mungu aliwabariki sauti hadi wakaipaisha Tanzania.
Kumbe ni wakimbizi, kwakweli walibarikiwa, nyimbo zao hazichuji,kila siku ukizisikiliza hazichoshi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…