Hawa wanafaa kusomea ualimu

Mzee Mwenzangu

Senior Member
Joined
Dec 23, 2013
Posts
190
Reaction score
168
Ili kuwa na waalimu wenye uwezo, serikali inatakiwa iwapange wale wote wenye DIV 1&2 vyuo vya ualimu daraja la tatu A. Wataokwenda Form 5 na kupata DIV 1&2 form 6 nao wapangwe ualimu diploma...
Amini usiamini waalimu waliopo Marian Girls, Feza, St Francis, Kifungilo......na shule kama hizo wengi ni wenye Bachelar Degree. Waliobaki ni watawa wasio na pressure hata chembe ya maisha.
Ni mtazamo tu ktk kuboresha Elimu TZ.
 
Sasa 5 na 6 aende nani? au wenye dv III ya pnt 30
 

wazo liko tenge mkuu.

tafadhali rejea miaka ya 70 mpaka 90, hawa walimu wa enzi hizo walichaguliwaje?

kwanini wao walikuwa na efficiency na effectiveness kubwa kuliko hawa wa sasa hivi?

there is a root problem i must say, waalimu wa sasa mbali na grade wanazochaguliwa nazo, kuna mambo mengi sana yanayowakinga kufikia lengo lao la ufanisi katika kazi..

endapo mazingira ya kazi yataboreshwa, mishahara itaongezwa, gharama za maisha zitapunguzwa kiasi kwa waalimu, hii angalau itapandisha morali ya waalimu kufaulisha na kufundisha watoto kwa moyo mmoja.
 
Me sidhani kama walimu wanahusika kwa wanafunzi kufeli,ila shida iko kwa wanafunzi wenyewe,kwa kweli inabidi tufike mahali tukubali kuwa,vijana wengi wa sasa hawana time na masomo,wengi wao wana time na mambo yasiyo ya msingi kama bongo flavour,watsupp,facebuk nk..wazazi nao wamekua bussy kiasi cha kushindwa hata kufuatilia maendeleo ya vijana wao huko mashuleni,kwa hiyo walimu wasitupiwe lawama za wanafunzi kufeli,ila lawama zote ziwaendee wanafunzi wenyewe kwa kutokuweka bidii katika elimu na wazazi wao kwa kutokua na ukaribu katika kufuatilia maendeleo ya vijana wao.over
 
Kwa maslahi gani mazuri waliyo nayo walimu?
Mimi nasema kama nikijaaliwa uzima, mwanangu ningependa asome shule zinazoitwa shule,ikiwezekana hata kwenye nchi za kikoloni...Haiwezekani hawa vijana waliokuwa hatched na kina Mulugo waje kumfundisha kijana wangu ujinga, wanaweza kumfundisha kufeli badala ya kufaulu maisha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…