Hawezi kunioa kwasababu hana "MSIMAMO WA MAISHA"

Aaaaahaaaaaaa! Na ndo maana stori yako iko biased na umekimbilia kutoa conclusion ya kublame! Hapo sasa nimekupata!

sija blame, nimesema kile kilicho ukweli mkuu, wasichana wamekuwa wakitafuta wanaume wenye hali ya juu kifedha, ili wapate maisha mazuri. Na kisingizio chao ni nataka mume awe na msimamo wa maisha.
Yani sio anipende? Ni awe na mali! Upuuzi mtupu.
 
muelekeo wa maisha ndo unatakiwa
mnashindwa kuwaelewa wasichana
unaweza ukawa una kazi nzuri halafu usiwe na muelekeo wa maisha
muelekeo wa maisha ina maanisha malengo ya baadaye au uliyonayo.

Hamna ukweli wowote hapo, wanakimbilia ambapo atakuta nyumba ishajengwa, mwanaume ana kazi ya kipato cha juu kuliko wewe!
Hakuna mtu ambaye hana malengo ya maisha bana. Ila kufanikiwa kwetu, kuna anayewahi kufanikiwa kuliko mwenzako. Sasa huwezi sema yule aliyewahi kufanikiwa mapema, ndio mwenye malengo katika maisha.
 
sija blame, nimesema kile kilicho ukweli mkuu, wasichana wamekuwa wakitafuta wanaume wenye hali ya juu kifedha, ili wapate maisha mazuri. Na kisingizio chao ni nataka mume awe na msimamo wa maisha.
Yani sio anipende? Ni awe na mali! Upuuzi mtupu.

Hahahahaaaa! Inaweza kuwa ni upuuzi mtupu lakini pia inaezakuwa sio......upo!! Kama alivosema shantel inategemea na mtu uliyekutana nae pamoja na we mwenyewe! Hivi kweli unaambiwa uwe na msimamo wa maisha kama ulivosema gari, nyumba, pesa, sasa unapompatia anakuwa amekupenda ama unakuwa umemvuta?? Haya kwa wale wa hali ya chini ama ya kawaida wanaolalamika, kipato chenyewe kidogo lakini utakuta na ye anajilazimisha kumgea gal mavitu makuubwa akiamini atapewa upendo siku huduma ikikata ghafla na upendo kwishneh ndo man anaanza kulalamika 'nikufanyie nini' wakati huo amesahau kwamba ile hali ameicreate yeye, jamani kama upendo haupo haupo tu! Tumeshuhudia watu wengi wanapenda lakini wanalipwa mabaya na kuachwa chakari, sasa akupende ili iweje? (sitetei ila jua kuna makwazo sana)!! Halafu unasema "yaani msichana anapenda vitu na sio anipende", why usiweke neno KUPENDANA au kwa sababu wewe una vitu basi kazi yako ni kusupply tu ivo vitu??
 
Inabidi na sisi wanaume tuanze kuwauliza wale wanaotuteka kama wana msimamo.
 
kwa hiyo wewe pretty huna cha upendo wala nini, msimamo mbele, mapenzi nyuma?
Pole!

.........Sasa kama mtu hana msimamo atawezaje kuwa kichwa cha familia? Au mimi sijakuelewa labda!!! Mimi kwangu mwanaume kuwa na nyumba, gari sijui pesa huo si msimamo wa maisha. Maana kama nyumba au gari hata mimi naweza kuvipata kwa pesa yangu.

Msimamo wa maisha ni mwanaume anayejua wajibu wake kama kichwa cha familia, mwanaume anayejua kutafuta, mchapa kazi.............hata kama hana pesa inabidi kichwa kifanye kazi ajue afanye nini ili aweze kumudu maisha.
 
Mim bado nipo sana 2! Msimamo ninao mwelekeo ninao.. Ila m2 akileta maigizo nami namletea usanii vile vile... Mtu unatakiwa kuwa mguu ndani na nje pia.
 
hebu kua mtu mzima sometimes ,pliiz naomba usinitafutie ban ka ulivomfanyia Mwita25
 
Kaka kweli umeongea vya point ila hebu tuangalie na upande wa pili wa shilingi aisee, hivi ingekuwa wewe ni dada alafu kwa ugumu huu wa maisha unapata nafasi ya kuchagua uolewe na masikini kama mimi hapa au mtoto wa Chenge ungechagua nini hasa? Tusilaumu tu, haya ya kusema mapenzi kwanza mengine baadae yameshapitwa na wakati bana, kama mapenzi yatakuja tu ukiyalazimisha hata kwa huyo mtoto wa Chenge au Lowassa....
 
wengi hukimbilia vitu vya mpita kama pesa na magari lakini wanashindwa kupata heshima na mapenzi
 
Mimi ningekuchagua wewe...
 
Tatizo lake ni kwamba wako sahihi kwa wanachozungumza lakini
hawako sahihi kwa wanachomaanisha. Anaposema msimamo ilibidi
amuangalie mwanaume ana malengo gani anaweza kwenda kwa
mwanaume mwenye gari na nyumba kumbe huyo ndo hana msimamo
cause inaweza kuwa kavikuta tu kwa baba akarithi n.k
 
Wahasibu mnawaonea jamani! Hivi kuwa mhasibu ni ishara ya kuwa na fedha? Kuhusu hilo la kina dada msiwaonee, hata wanaume siku hizi hawaoi wanawake bali wanaoa kilicho ndani ya wanawake. Mtazamo wa kimapenzi umebadilika sana tofauti na zamani. Wanawake nao hawataki wanaume wenye kipato cha chini na wanaume nao hawataki wanawake wasio na kipato hivyo mimi naon hapo pana conflict of interest.
 
Mimi ningekuchagua wewe...
Kweli? Hebu jaribu uone, njoo ufue nguo na majani ya mpapai kama ndio sabuni huku unapiga mswaki na mkaa kama ndio toothpaste. Asubuhi unawahi kuamka saa 11 kasoro kwenda kisimani kilomita 3 toka home, kusafisha nyumba na kusafisha watoto 4 tulionao ambao wote wako primary mkubwa darasa la 5 na mdogo la 3, kisha unawahi shamba fasta, saa ya kurudi shamba unakuja na mzigo wa kuni na kisamvu unakitwanga unapika ugali ndio tunakula na tukienda kulala haki yangu kama kawaida......., hamna maswali wala umechoka sijui nini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…