Haya mabomu tunayoambiwa Hayati Magufuli aliyatega. Je hakujua kama ataongoza Nchi kwa miaka mingine mitano?

Haya mabomu tunayoambiwa Hayati Magufuli aliyatega. Je hakujua kama ataongoza Nchi kwa miaka mingine mitano?

Error 404

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2022
Posts
2,151
Reaction score
3,493
Kulitokea suala la Umeme tukaambiwa na wajuzi wa Mambo kwa ilikuwa ni matter of time bomu hilo kulipuka kwa hiyo shida kutokea ni matatizo ya Awamu ya Tano.

Kukatokea suala la ugumu wa Maisha na vitu kupanda Bei tukambiwa hivyo hivyo na kuongeza kwamba bwana Yule hakuacha pesa Hazina ila baadae ikasingiziwa vita ya Ukraine.

Suala la Ajira ni sababu zile zile.
Na mambo mengine mengi

Mikopo ya masharti Magumu majibu ni Yale yale.

Hivi Huyu Shujaa hakujua kuwa ataendelea kutawala miaka mitano mingine ?
 
Ktk point za kihayawani kuwahi kuskia ni hili la kutoacha pesa Hazina.

1. Kwani alipokufa serikali iliacha kukusanya kodi?

From 800b to 1.6T ya makusanyo per month bado mnasema hakuacha pesa? Ht km hakuacha pesa then aliiwaachia mfumo wa kuikusanya. Amefariki 17th..means, atleast they got a half ya makusanyo.

2. Hizi $5B equvalent to 11T km akiba ya fedha za kigeni zilizopo BOT ni kwamba zilikusanywa Overnight baada ya mama kuingia?

Hii inchi ina vichwa maji wengi sana...we need to overhaul our education systems.
 
Ktk point za kihayawani kuwahi kuskia ni hili la kutoacha pesa Hazina...
1. Kwani alipokufa serikali iliacha kukusanya kodi...
Hii Nchi ina mambo ya Ajabu sana
 
Kwenye ajira umeandikia utumbo, aliajiri yule?
 
Kwenye ajira umeandikia utumbo, aliajiri yule?
Mkuu Ajira ni Bomu la muda Mrefu sio awamu ya Tano tu ,Nchi kama nchi lazima iJenge Viwanda na vyanzo vya ajira vingi sio kuajiriwa serikali .
 
Back
Top Bottom