Haya magazeti yanamuonea Magufuli au ndivyo ilivyo

Mkuu Kwa mtu ambaye hajazisoma hukumu hizo anaweza hisi walionewa lakini ukizisoma hukumu hizo kama una roho nyepesi unatokwa machozi jinsi watoto walivyofanyiwa
 
Mahakama zote ziliwaona wana hati, huu msamaha au waondolei kosa. Ushahidi pasina shaka ndiyo unaoweza kumtia hatiani mtu. Gazeti halina kosa wale ni wabakaji asilimia mia, na kwani wamwambie watakuwa watu wema?
 
Akhsante kwa masahihisho, kweli ni kulawiti sio kubaka kama nilivyoandika hapo awali.

Lakini kuhusu eti tunalizungusha ili ionekane ni kubaka badala ya kulawiti, sijui unamaanisha akina nani tunaolizungusha. Maana kama nilivyokwambia hili suala lilifikia kuwa la kisiasa hadi wagombea kulipigia kampeni za uchaguzi kwa kujua kuwa wapiga kura wengi walikuwa wanaamini kuwa hao jamaa walisingiziwa (maneno ya chini chini)

Lakini naweza kukuelewa, nadhani unamaanisha tunaomuunga mkono JPM ndo tunalizungusha suala hili. Binafsi sioni haja ya kufanya hivyo, maana haitabadilisha chochote!
 
Mtoa mada mbona hueleweki? Huamini kama walibaka? Au huziamini mahakama zetu? Au ulitaka gazeti liandikeje?

Kwanza kabisa huwa sina imani na mahakama za Kiafrika, maana zinategemea uchunguzi wa mapolis wa Kiafrika wasiokua na vitendea kazi ipasavyo na huishia kukurupuka.
Hivyo naomba iwe kwamba uchunguzi ulifanywa kindani na kugundua jamaa hawakua na makosa, lakini hayo ya kudai eti wasamehewe maana hakuna mtu asiyekua na makosa dunia hii, aisei kulawiti watoto haisameheki.
 
Mkuu Rais ni taasisi wala si mtu mmoja!! Ukisikia wanasema Rais elewa ni taasisi wala si mtu mmoja!!
Mkuu rais ni mtu mmoja tu, ndiye anayepigiwa kura na ndiye anayeapishwa, na akipatikana na kosa ndiye anayepigiwa kura na kutokuwa na imani naye, hata katika katiba ukiisoma utaona inamataja rais kama mtu mmoja, kiingereza wanatumia he/she.
 
Naomba tupate maana ya maneno haya matatu
1)Kubaka
2)Kulawiti
3)Kunajisi
Nadhani tunayachanganya, mimi kwa jinsi ninavyofahamu, kubaka ni kufanya ngono na mwanamke bila ridhaa yake, na inachukuliwa mtoto chini ya miaka 18 hawezi kutoa ridhaa, hivyo ukifanya mapenzi na mtoto wa kike inachukuliwa ni kubaka.

Mapenzi kinyume na maumbile ni kulawiti, lakini ukimfanyie mtoto mdogo kinyume na maumbile ni kumnajisi..

Kama kuna anayejua tofauti na hili ninaomba msaada.
 
Kwa uamuzi wa Rais Magufuli kuwasamehe hiyo ilikuwa haki yake kikatiba lakini kwa kuwakaribisha hawa jamaa ikulu ni big mistake kwani Mwalimu Nyerere alisema Ikulu ni pahala takatifu kwa kwa wahalifu wa aina hii pamoja na kusamehewa hawakutakiwa kukaribia ikulu hiyo.
 
MK254,
Umeuliza swali muhimu sana ambalo lingetakiwa maelezo ya kina sababu ya mhimili wa serikali/dola/ executive kuamua kuwafungulia hawa jamaa wa familia ya Nguza.

Ikiwa kama Mh. Rais na bodi ya parole n.k walipitia kesi na kuona kuna mapungufu au jambo jipya wakaona hakuna haja ya kulipeleka mahakamani kupoteza muda haki ipatikane kwa wafungwa basi wangetolea maelezo maelezo ya sababu ya kuamua kutumia ''uwezo'' wa kikatiba ambao ni sheria mama rejea.

Kwa taasisi ya Urais kuamua kuwapa 'msamaha', kunazua maswali mengi mengine ''chanya'' kuwa ''wafungwa'' hawa wa familia ya Nguza walionewa na kuna maswali mengine ''hasi'' kuwa inakuwaje ''wabakaji'' wameachiwa.

Mhimili wa Mahakama au Bunge au Serikali ina la kujifunza kuhusu uamuzi wa msamaha huu ikiwa tu sababu zitawekwa wazi na kusaidia huko mbeleni kama kuna maamuzi ya ''shindikizo/pressure'' basi mihimili hiyo itajitahii kuiepuka na kutenda haki kwa wote na muda wote.
 
Na wanaishi kama wako peponi kwa sasa!
 
Always two sides to the story...then there is the truth...Hii kesi ilinichanganya sijui niamini nini...
 
Mwenyezi Mungu ndie mjuzi wa kila kitu. Tuache kulalamika.
 
Watz bana, wabakaji ikulu? Hiyo ikulu baadaye mtakuja ifanyia maombi, hadi na mafuta ya upako humo ndani mtayamaga sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…