Haya Maridhiano ni ya CCM kujipendekeza kwa CHADEMA? Mbona Lissu anaisimanga sana CCM kwamba mambo ni yale yale?

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Nilitegemea baada ya kuingia kwenye Maridhiano viongozi wakuu wa CCM na Chadema wangekuwa wanatoa kauli za kujenga siyo kubomoa.

Lakini ni viongozi wa CCM Ndio wamekuwa watulivu pamoja na Mbowe pekee kwa upande wa Chadema.

Kauli za Tundu Lisu na Mnyika zimekuwa za Utata sana.

Juzi Mnyika kazungumzia Muswada wa Katiba Mpya unaoepelekwa bungeni huku akitoa tahadhari kadhaa kana kwamba hakuna Maridhiano.

Tundu Lissu naye kashuka tu kwenye Ndege na Kuanza kuishambulia CCM kwamba ina Watu walewale wanaofanya mambo yaleyale na kwamba CCM imefeli.

Niwape tu angalizo viongozi wa Chadema wasisahau kuwa CCM ni Chama kikubwa sana.

Nawatakia Juma Takatifu Lenye Baraka tele!
 
Yaani ni Ccm na Mbowe tu ndio wamekuwa watulivu. Mwisho wa kunukuu. It smells fishy isn’t?
 
Uje na wazo lako ,Toka umeaza kusikia taarifa za CAG kunamabadiliko , usishangae unavoambiwa yaleyale ,wale wale
 
Muulize Jiwe akusimulie .

 
Maridhiano yamempaisha mwenyekiti wa CCM na rais kimataifa, rejea kauli za Kamala Harris na jumuia na mashirika ya kimataifa.
Maridhiano haya yameleta misaada na mikopo ambayo serikali ya CCM inatamba nayo kwenye miradi inayo endelea nchini.
Kwa manufaa hayo hawajali kauli za Lissu na Mnyika wanajua miradi hiyo itawabeba uchaguzi ujao.
 
Wizi wa sasa hata mama keshaukataa ndiyo maana kasema wote waliotuhumiwa na CAG wapishe uchunguzi
 
Anajibaraguza tu kwa kuwa anataka chupa kubwa la asali, we subiri akatiwe mshiko wake uone kama atasema neno kama siyo kuimba mapambio tu.
Cheza na asali wewe!
 
Wapigie simu 0652627771 Athumani na Selemani 0715132277 ndiyo wenye kujua mambo yote yanayoendelea Nchini kwani wapo karibu na chadema na pia wapo karibu sana na CCM, watakufafanulia vizuri kwa uwazi
 
Anajibaraguza tu kwa kuwa anataka chupa kubwa la asali, we subiri akatiwe mshiko wake uone kama atasema neno kama siyo kuimba mapambio tu.
Cheza na asali wewe!
Kwani ipo Asali?hakuwa amepata Asali yake?
 
Hajakosea hata kidogo,Mwamba nae asikae kimya wakati majizi yanaliangamiza Taifa.
Ukitaka Habari zote za viongozi wa Nchi hii watafute Athumani na selemani watakupa file la kila mmoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…