Haya matukio yalinifanya niamini uchawi upo

Haya matukio yalinifanya niamini uchawi upo

wakunyonya

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2024
Posts
520
Reaction score
1,414
Huwa nashangaa sana mtu kusema Hamna uchawi ila kusema kweli uchawi upo tena bila chenga.

Haya ni baadhi ya matukio ambayo yaliweza kuniaminisha kuwa uchawi upo.

TUKIO LA 1#
Miaka ya 2000s wakati huo nipo mkoa wa Iringa, kulikuwa na Mzee mmoja yeye shughuli yake ilikuwa ni kuchukua ulazi(bamboo juice)vijijini Kwa wagemaji na kupeleka kuuza mjini.

Sasa huyu Mzee alikuwa akimiliki gari Moja bovuu mno Yani bovu haswaa ambalo alikuwa akilitumia ktk shughuli za biashara yake. Sasa wakati anapeleka ulanzi alikuwa akikumbana na police ambao walikuwa wakishikilia gari lake kutokana na ubovu halina vigezo vya kutumika barabarani.

Sasa police walipeleka gari kituoni ili kumpiga Mzee faini, Mzee yule aliomba masaa kadhaa ajichange ili alipe faini, baada ya kama nusu saa Mzee aliludi kituoni ili kuwalipa faini police, Sasa Mzee kabla ya kulipa aliwaomba police achunguze gari lake kama lipo salama kama alivoliacha, Mzee baada ya kulicheki gari akawaambia police mbona gari langu engine haipo? Police kuangalia kweli engine Hamna na haijapita hata lisaa tangu Mzee awaachie gari, na police walikuwa hapohapo kituoni ikabidi police waanze kuangalia utaratibu wa kumlipa Mzee engine ya gari lake.

So baada ya police kumlipa yule Mzee alichukua gari na kuondaka wakati lilikuwa halina engine police walibaki midomo wazi,.

So huyu Mzee kila akishikiliwa na police walikuwa lazima wakutane na vibwenga vyovyote yaani lazima Mzee alipwe, ilifika muda Mzee akawa anaogopwa hakuna police wa kumshika labda wale police wageni ambao walikuwa hawamjui yule Mzee.

TUKIO LA 2#
Hiyohiyo Miaka ya 2000s ktk Kijiji ambacho nilikuwa nikiishi kulikuwa na Mzee mmoja ambaye alikuwa akijulikana na kijiji kizima kutokana na ushirikina,.

Sasa huyu Mzee alikuwa akisadikika kwamba anaua watoto wake kutokana na vifo vya kufa ovyo watoto wake tena ktk mazingira tatanishi, Sasa ndugu zake walikuwa wakimuuliza kwaniin unaua wanae ovyo, yeye anajibu kwan Kkna ubaya kuku kula mayai yake.

Baada ya hali kuwa mbaya misiba ya watoto wake imekuwa mingi, ikabidi wanandugu wakae pamoja kumtishia Mzee atolewe hayo madude yanayosadikika kuwa ndiyo chazo cha hivo vifo vya watoto wke.

Kweli Mzee bila hiyana akakubali kutolewa hayo madude yake ila akawaambia sijamwona mganga wa kutoa hivi vitu mpaka hapa vilipofikia. Wanandugu wakatangaza tenda mganga akajitokeza, nakumbuka zilitakiwa kutolewa ng'ombe sita Kwa mganga atakayetoa.

So mganga alikuja na team yake tayari kwa kazi, yule Mzee(anayetolewa uchawi)nakumbuka aliwaambia umati kuwa huyu mganga aliyekuja hatoshi kutoa hayo madude yake kwani Bado ni mtoto mdogo, watu wakajua ni dhihaka.

Bwana weee! mganga aliingia ndani ya nyumba ya yule mzee na wasaidizi wake wawili, umati wa watu tukiwa nje tunasubiri anayojiri.

Baada ya kama dakika Tano mlango ulijifunga mganga na wasaidizi wake wakiwa ndani, mara tukaaza kusikia vilio vya kuomba msaada, ikabidi tulio kuwa nje tuanze kubomoa mlango, jamaa watoke kweli zoezi la kubomoa mlango lilifanikiwa ila yule mganga na wasaidizi wake waliugua ukichaa, wakawa vichaa kabisa kabisa, wakati hayo yote yanatokea Mzee alikuwa akicheka vibaya mno mbavu Hana😂

Nakumbuka waliletwa waganga wengine kutoka mikoa ya mbali lakini still walishindwa so, solutions yule Mzee alikuja kuuliwa na tena Kwa timing mno maana hata zoezi la kuuliwa nalo lilikuwa limeshindikana.
 
Back
Top Bottom