Haya ndio wanayoyataka ndugu zetu wa ki-zanzibara muungano uwe hivi

Haya ndio wanayoyataka ndugu zetu wa ki-zanzibara muungano uwe hivi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363


Kamati ya Maridhiano Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake, Mhe. Hassan Nassor Moyo, imefafanua

MAMLAKA KAMILI inayotaka Zanzibar iyasimamie yenyewe ambayo yanajumuisha mambo

yafuatayo:

1. Mipaka ya Zanzibar kama ilivyokuwa kabla ya tarehe 26 Aprili, 1964.

2. Uraia.

3. Uhamiaji.

4. Mambo ya Nje.

5. Polisi.

6. Sarafu, Mabenki na Usimamizi wa Fedha za Kigeni.

7. Mikopo na Biashara ya Nchi za Nje.

8. Kodi ya Mapato, Ushuru wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa.

9. Bandari, Usafiri wa Anga, Posta na Simu.

10. Leseni ya Viwanda na Takwimu.

11. Elimu ya Juu.

12. Maliasili ya mafuta na gesi asilia na maliasili nyengine zote zilizomo ardhini na baharini.

13. Baraza la Taifa la Mitihani.

14. Usafiri na Usafirishaji wa Anga.

15. Utafiti.

16. Takwimu.

17. Vyama vya Siasa.


Ukiondoa hayo yale maeneo mengine yaliyopendekezwa kubaki katika Muungano basi Kamati

imetaka utaratibu wa uendeshaji na usimamizi wake uwe wa wazi na uhusishe na ushirikishe

pande zote mbili kwa usawa kama nchi washirika - Zanzibar na Tanganyika.

CHANZO.
http://zanzibarniitakayo.blogspot.com/2013/05/mapendekezo-ya-kamati-ya-maridhiano.html

 
Huyo aliyependekeza hayo ni kichaa, tena hana maana hata kusikilizwa, maana hataki muungano ila anaanzia mbele anarudi nyuma.
Mfungo umeisha karibu kwenye Chair fire.
 
hivi ni kweli wazanzibari wanataka muungano tucje tukatumia garama nying alafu baadae wakazingua kama hawautaki waseme 2
 
hivi ni kweli wazanzibari wanataka muungano tucje tukatumia garama nying alafu baadae wakazingua kama hawautaki waseme 2

Sio Wazanzibari tu, hata mimi ninayetoka kijiji cha Nyibhoko, Kata ya Kisaka, Tarafa ya Ngoreme, Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara SITAKI HUU MUUNGANO wa kuwafaidisha Wapemba huku sisi tukipokea matusi na Tindikali.

Kwa mfano, katabia kalikooneshwa juzi na Wajahidina ka kuwamwagia tindikali wale watoto wa watu kataathiri utalii kwa Tanzania as a whole.

Hili jambo Mwalimu alilifanya wakati ule kwa manufaa, sasa tukumbuke kuwa chakula cha leo kesho ni kinyesi. Huu Muungano ni dhambi
 
hivi ni kweli wazanzibari wanataka muungano tucje tukatumia garama nying alafu baadae wakazingua kama hawautaki waseme 2
Mkuu chibwilu chibwade Wa-Zanzibar wanautaka Muungano lakini kwa Masharti hayo 17 yalipo kwenye Thread hii yangu yakikamilika ndio kwao wao Wa-Zanzibar huuu Muungano utakuwa ni wa ukweli. Pasipo na hayo Masharti 17 utakuwa Muungano usiokuwa wa ukweli ndani yake kwa Mawazo yao hao ndugu zetu wa Ki-Zanzibar.
 
Elimu ni ktu muhimu sana sasa wat wakiwa wanaamshwa na huo uamsho wao pasipokuwa na elimu (sio ilimu) ya kuwawzesha kupambnua mambo kwa kna madhara yake ndo hayo sasa.hlo ni shinkizo kwa maslahi ya wachache.kifup ni kwamba wanaukataa muungano kwa njia ya ama masharti magumu au kwa kujizungusha (indirect refusal) lakini wanasahau kuwa kwa muungano watu wameoana,wamezaa na kujenga familia kubwa tu sasa sijui wanataka baada ya kuvunjwa muungano wat waombe uraia? Ningekuwa ndo mtoa maamuzi ningesema "vunja tu"
 
Hivi wadanganyika hakuna nchi nyengine ya kuungana lazima iwe zanzibr?ndio maana mnaporwa rasilimali kwa kuwa nchi yenu danganyika hamuitaki.
 
Elimu ni ktu muhimu sana sasa wat wakiwa wanaamshwa na huo uamsho wao pasipokuwa na elimu (sio ilimu) ya kuwawzesha kupambnua mambo kwa kna madhara yake ndo hayo sasa.hlo ni shinkizllo kwa maslahi ya wachache.kifup ni kwamba wanaukataa muungano kwa njia ya ama masharti magumu au kwa kujizungusha (indirect refusal) lakini wanasahau kuwa kwa muungano watu wameoana,wamezaa na kujenga familia kubwa tu sasa sijui wanataka baada ya kuvunjwa muungano wat waombe uraia? Ningekuwa ndo mtoa maamuzi ningesema "vunja tu"
Yaani wewe unayejiona kuwa una elimu ndiye ambaye hoja yako yote ya muungano umeijengea kwenye kuoana na kujenga familia kubwa!

Masikini hujui kuwa kabla ya muungano Wtg na Waznz walikuwa wameoana na kuwa na familia kubwa tu...waliishi vipi?

Nenda sehemu za mipakani uone jinsi Watanganyika walivyooana na raia wa nchi nyingine na kuwa na familia kubwa tu...wanaishi vipi?
 
hivi ni kweli wazanzibari wanataka muungano tucje tukatumia garama nying alafu baadae wakazingua kama hawautaki waseme 2

Majority ya wa Zanzibar hawautaki muungano. Wanaoutaka muungano ni wanzanzibar wachache waliopo kwenye serikali ya muungano na wabunge ambao wanapata tonge kupitia serikali ya muungano, na bahati mbaya hawa ndio wanaowawakilisha wanzanzibar kwenye bunge la muungano ambalo ndio kama linatoa maamuzi ya mwisho.
Labda wanzanzibar wasusie kupiga kura kwa wabunge wa muungano, wapige kura kwa wajumbe wa baraza la wawakilishi tu.
 
Back
Top Bottom