Haya ndiyo maoni yangu:Kabla hujao boresha kwanza sehemu unayolala

Haya ndiyo maoni yangu:Kabla hujao boresha kwanza sehemu unayolala

Nikifa MkeWangu Asiolewe

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2024
Posts
6,944
Reaction score
14,351
Ni maoni yangu yanastahili kupingwa,kuungwa mkono au kukosolewa ama kuboresha zaidi.

Kwa mwanaume jambo ambalo unapaswa kulipa kipaumbele zaidi unapoanza maisha Yako ya kujitegemea boresha kwanza sehemu ya kulala.

Kwanini napendekeza sehemu ya kulala iwe nzuri.

Baada ya michakato,kazi ngumu na harakati za hapa na pale za kutwa nzima sehemu pekee ya kutuliza akili na uchovu ni kitandani unapolala uwe umeoa au hujaoa.

•Ni sehemu pekee ambayo mwili na akili hupumzika na kuchakata vilivyo ukiwa umetulia.
Kitandani ni sehemu pekee ambayo binadamu hunitumia kupumzika Kwa muda mrefu zaidi kuliko sehemu yoyote Ile.

Unapolala sehemu nzuri hata mwili wako utaamka ukiwa na nguvu tele.

•Ni sehemu pekee ya kuiwaza kesho Yako.
Ukweli usiopingika ukiwa kitandani baada ya kupigika na kazi za hapa na pale ni muda Sasa wa kupumzika na kutafakari zaidi maisha Yako ya badae.

Siyo rahisi sana kupata muda wa kutafakari kama hata sehemu ya kulala unaiwaza yaani wewe mwenyewe huipendi mara nyingi utakuwa unachelewa hata kurudi kwako Ili masaa yaende ukija kujitupia kitandani baasi ni kulala Moja Kwa Moja Kwa sababu umekuja Kwa kuchelewa.

•Hata Girlfriend wako atakuthamini zaidi kama wewe mwenyewe umejipa thamani kupitia kitanda chako.
Kataa ukubali wanawake wengi wanapenda usafi na unadhifu hasa sehemu unayolala haijarishi unalala chini ama juu lakini ukweli ni kwamba unapaswa upaboreshe zaidi pawe pazuri.

Hii haijarishi uwezo wako hata kama una godoro la Inchi4 ninachosema ni usafi na umaridadi wako.

Sisi tuliozaliwa kwenye familia za kifugaji tunajua maana halisi ya kulala pazuri

Nimelala kwenye ngozi ya ng'ombe Hadi natumiza miaka 13.

Nikaanza kulalia godoro la pamba Kwa Sasa wanaita msabato na wanaweka vitambaa hasa mabaki ya kwenye cherehani.

Siku nilipo anza kulala pazuri niliona utofauti mkubwa sana.

Ukweli ni kwamba hata wewe akija mgeni/wageni jambo la kwanza utakalo waza ni sehemu ya kuwalaza pazuri na kula vizuri pia.

Sehemu ya kulala ikiwa mbaya hata wewe mwenyew utapachukia tu.

Kuna dogo yeye kipaumbele chake ni simu anapolala Net imetoboka mashuka hayaeleweki hata Rangi Kwa kifupi ni mchafu sana na ukweli Huwa halali kwakwe mara Kwa mara.

Lakini kubadirisha simu Kali Hadi unajiuliza Hela za kununua simu Kali namna hii Huwa anatoa wapi?

Basi jitahidi sehemu ya kulala pawe na hewa safi na yakutosha pia
FB_IMG_1734795943031.jpg
 
Hiyo ndiyo ilikuwa philosophy yangu wakati naanza maisha, nilikuwa na geto lililotimja kila nilichokipenda, shida ikianza marafiki walipoanza kuniazima geto kwa shughuli za kindoa, baadaye nikavuta mamsapu ndo nikasalimika.
 
Hiyo ndiyo ilikuwa philosophy yangu wakati naanza maisha, nilikuwa na geto lililotimja kila nilichokipenda, shida ikianza marafiki walipoanza kuniazima geto kwa shughuli za kindoa, baadaye nikavuta mamsapu ndo nikasalimika.
Mimi niliwahio azimisha siku moja tu tangu hapo nikaghaili mazima kabisa nikawa sitaki kabisa kumpa mshikaji tena
 
Ni maoni yangu yanastahili kupingwa,kuungwa mkono au kukosolewa ama kuboresha zaidi.

Kwa mwanaume jambo ambalo unapaswa kulipa kipaumbele zaidi unapoanza maisha Yako ya kujitegemea boresha kwanza sehemu ya kulala.

Kwanini napendekeza sehemu ya kulala iwe nzuri.

Baada ya michakato,kazi ngumu na harakati za hapa na pale za kutwa nzima sehemu pekee ya kutuliza akili na uchovu ni kitandani unapolala uwe umeoa au hujaoa.

•Ni sehemu pekee ambayo mwili na akili hupumzika na kuchakata vilivyo ukiwa umetulia.
Kitandani ni sehemu pekee ambayo binadamu hunitumia kupumzika Kwa muda mrefu zaidi kuliko sehemu yoyote Ile.

Unapolala sehemu nzuri hata mwili wako utaamka ukiwa na nguvu tele.

•Ni sehemu pekee ya kuiwaza kesho Yako.
Ukweli usiopingika ukiwa kitandani baada ya kupigika na kazi za hapa na pale ni muda Sasa wa kupumzika na kutafakari zaidi maisha Yako ya badae.

Siyo rahisi sana kupata muda wa kutafakari kama hata sehemu ya kulala unaiwaza yaani wewe mwenyewe huipendi mara nyingi utakuwa unachelewa hata kurudi kwako Ili masaa yaende ukija kujitupia kitandani baasi ni kulala Moja Kwa Moja Kwa sababu umekuja Kwa kuchelewa.

•Hata Girlfriend wako atakuthamini zaidi kama wewe mwenyewe umejipa thamani kupitia kitanda chako.
Kataa ukubali wanawake wengi wanapenda usafi na unadhifu hasa sehemu unayolala haijarishi unalala chini ama juu lakini ukweli ni kwamba unapaswa upaboreshe zaidi pawe pazuri.

Hii haijarishi uwezo wako hata kama una godoro la Inchi4 ninachosema ni usafi na umaridadi wako.

Sisi tuliozaliwa kwenye familia za kifugaji tunajua maana halisi ya kulala pazuri

Nimelala kwenye ngozi ya ng'ombe Hadi natumiza miaka 13.

Nikaanza kulalia godoro la pamba Kwa Sasa wanaita msabato na wanaweka vitambaa hasa mabaki ya kwenye cherehani.

Siku nilipo anza kulala pazuri niliona utofauti mkubwa sana.

Ukweli ni kwamba hata wewe akija mgeni/wageni jambo la kwanza utakalo waza ni sehemu ya kuwalaza pazuri na kula vizuri pia.

Sehemu ya kulala ikiwa mbaya hata wewe mwenyew utapachukia tu.

Kuna dogo yeye kipaumbele chake ni simu anapolala Net imetoboka mashuka hayaeleweki hata Rangi Kwa kifupi ni mchafu sana na ukweli Huwa halali kwakwe mara Kwa mara.

Lakini kubadirisha simu Kali Hadi unajiuliza Hela za kununua simu Kali namna hii Huwa anatoa wapi?

Basi jitahidi sehemu ya kulala pawe na hewa safi na yakutosha pia
View attachment 3181810
Haya mandhari nimeyapenda
 
Ulale chini au kwa godolo mlima ndoto tutakazoota ni zile zile.tena wewe unaelalia godoro mlima unaweza ota mandoto ya kutisha mpaka ukakimbia ndani kwako mm nae lalia mkeka nkawa naota napata dinner na elon musk
Mkuu sikupingi hata lakini unapolala kwenye mkeka ni kwamba umependa au imekulazimu ulale tu kwa sababu uwezo huna?

Mimi nimepitia maisha ya kulala kwenye ngozi ya ng'ombe na pengine wewe hujawahi, nimelia msabato hivyo najua kila kitu. kuota ndoto na kupumzika ni jambo jingine maana kuna watu wana majumba ya kifahari na hawalali kwa raha. lakini kwa hali ya kawaida kabisa kitandani lazima papewe kipaumbele zaidi.

ukilala kwenye mkeka hata mwili utaamka umechoka yaani viungo vya mwili havitakuwa na ushirikiano mzuri
 
Inategemea na ukubwa wa ndoto zako. Kwa mtu anayewaza makubwa lazima mwanzoni awekeze hela yake karibu yote kwenye chanzo chake cha mapato. Ukiwa na chanzo cha kueleweka cha mapato mambo mengine huwa marahisi mno.
Hii inaingia akilini kweli mkuu mfano kwa siku unaingiza 50kila una malengo makubwa sana huko mbele je utaendelea kulala kwenye mkeka hadi utimize malengo yako?

Unajua wazi kabisa magodoro yapo hadi ya 70k nk
 
Back
Top Bottom