Haya sasa, sarafu yetu ya MIA TANO hii hapa!

hapo mi naona ni mambo ya katiba mpya....wanzanzibar wanazugwa kwa kuwekwa picha ya karume katika hiyo sarafu ili wakubali serikali mbili kiuraini kwakudhani wanathaminiwa. Kalaghabaho!
 
Sababu walioitoa BOT ni kuwa 500 ya noti ambayo inatengenezwa na pamba huchakaa kwa haraka sana Ndio maana wanaleta sarafu sasa.

Dah ndio shida ya kuwa na watu wanaotumia makalio kufikiria, hivi katika zile sifa za money wao wameangalia durability tu? Huku ni kupeana mizigo isiyokuwa na msingi mifukoni
 
Sababu walioitoa BOT ni kuwa 500 ya noti ambayo inatengenezwa na pamba huchakaa kwa haraka sana Ndio maana wanaleta sarafu sasa.

hawapendi tu kuadmit kwamba imetengenezwa kwa kiwango hafifu, dola ya marekani imetengenezwa kwa cotton paper kama kawaida, noti zetu zote cotton paper, haya sasa watengeneze coin ya elf kumi tuachane na noti! kumbuka mlipolalamika elfu kumi zinachuja rangi mlijibiwa nini na yule kilaza "ukiona inachuja rangi ujue ndiyo original!!!"...lame.
 
Sababu walioitoa BOT ni kuwa 500 ya noti ambayo inatengenezwa na pamba huchakaa kwa haraka sana Ndio maana wanaleta sarafu sasa.

Kama sababu ya kuleta sarafu ya mia tano ni kwa vile noti za mia tano zinachakaa haraka basi suluhisho sio kuleta sarafu bali kutengenza noti zenye kiwango cha juu cha ubora; mbona zile noti zilizokuwa zinatumika kabla ya hizi hata zile za 5000 zilikuwa hazichakai kama hizi za sasa?

Unfortunately , hata hizi sarafu kama zikitengenezwa kwa kiwango cha chini cha ubora kama wanavyotengeneza sarafu za 200 basi tutakuwa tumejiongezea gharama bure bila kutatua tatizo; sarafu za 200 za sasa hivi zikikaa kwenye maji kwa muda zinayeyuka, kama huamini weka sarafu ya mia mbili kwenye kikombe cha maji jioni halafu kaiangalie asubuhi uone ilivyobadilika!!!!

Uongozi wa BOT wa huyo Ndullu ni majanga matupu.
 

value ya currency ndio tatizo kubwa kwenye uchumi, hususani inaposhuka kwa kasi kubwa ukilinganisha na fedha za wenzetu (ukiondoa mara chache wachumi wanaposhusha kuvutia soko).
 
huku tunapoelekea watatoa sarafu 50000 hawa jamaa wa ccm hawafai kabisa
 
Ni wasi wasi ccm wameanza maandalizi ya kusaka hela ya kampeni
 
Duu!! kila ikikaribia uchaguzi, watu wanatafuta vyazo vya kupiga hela.
 



Sarafu ya shilingi mia tano inatarajiwa kuzinduliwa na Benki Kuu ya Tanzania katika siku za usoni. Sarafu hiyo itatumika sambamba na noti za shilingi mia tano huku zikiwa zinaondolewa kwenye mzunguko taratibu taratibu. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Huduma za Kibenki na Sarafu wa Benki Kuu Baada ya noti ya shilingi mia tano kubainika kuwa kwenye mzunguko mkubwa sana na hivyo kuchakaa mapema,Benki Kuu ya Tanzania(BOT) imeamua kuleta sarafu ya shilingi mia tano mwaka huu wa fedha inayotegemewa kudumu kwa miaka zaidi ya ishirini.
 

Attachments

  • tanzania-2011-500.jpg
    28.5 KB · Views: 1,192
  • unnamed+(2).jpg
    38 KB · Views: 1,226
value ya currency ndio tatizo kubwa kwenye uchumi, hususani inaposhuka kwa kasi kubwa ukilinganisha na fedha za wenzetu (ukiondoa mara chache wachumi wanaposhusha kuvutia soko).

Kwa miez mitatu mfululizo bei ya mafuta imepanda kila Jumatano ya mwanzo wa mwezi, kiashirio kimojawapo kuwa shilling yetu iko taaban dhidi ya dolari.
 

Hii ndo maana ya Slogan za CCM:
1. Maisho bora kwa kila Mtanzania- tunaongeza upatikanaji wa vyuma Chakavu ili mateja wapate ajira
2.. Ari zaidi, Nguvu zaidi, na kasi zaidi katika kudhooficha uchumi wa nchi kwa usimamizi mbovu wa rasilimali fedha, watu,maliasili.
Tumethubutu, tumeweza na sasa tunasonga mbele kwa ongezeko la inlation rate, deni la taifa, ufisadi uliopindukia, mikataba mibovu na mwngineyo.
NOTE:
Hize fedha za noti ni zaidi ya feki na hazino ubora wowote. Kampuni inayochapisha hizi note inatumia material fake na fedha ikikaa kwenye mzunguko miezi sita imeshachakaa na zimekuwa rahisi sana kutengenezwa na mafisadi na zinatumika kwenye mzunguko. sasa sielewe kama wabunge wameweza kurealize hili tatizo la noti za nchi kuwa dhaifu mpaka zinapindukia.
Hiyo sarafu ni mradi wa kifisadi zaidi.
 
Aliyetoa wazo hili ni nani?

Kumbe inawezekana watu wanajadili uchumi wa nchi huku wakiwa bar wanavuta balimi na kunywa sigara!

Mkuu acha dharau kwa walipa kodi maarufu hapa nchini...eboo!!
 
uchumi umepanda kwa %5. Tz majanga hayatakwisha.
 
mifuko itakuwa mizito balaa, noti zinapungua kwenye wallet tunabebeshwa mavyuma kilazima.

Ukiwa na hizo 10 si sawa na muuza chenji??

Ulimwengu wa noti huu sio hayo mabati.

umenifanya nicheke maana hapa nina note 9 za mia tano natafakari ingekuwa coin
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…