yaani mtu anakuja kuuliza tabia za mpenzio wake jf kwani sisi tunamjua jamani?watanzania kwa kupenda kudanganywa?
Japo kweli watanzania tunapenda sana kutambua makabila kwa tabia, kisaikolojia na hata kwa ushahidi wa sisi wenyewe katika mahusiano yetu ya kila siku KILA MWANADAMU ANA TABIA ZAKE!
Siyo kila mtoka kabila isadikiwayo kupenda ugomvi ni mgomvi; sio kila atokaye kwa kabila MALAYA (lidhaniwavyo) ni malaya, n.k.
Jamaa yako ajiangalie akitakacho kwa mpenzi wake; na mema vs mapungufu! Mizani ikakaa sawa aoe! Mie nimeoa toka kabila la wala watu na mwaka wa 20 ndaoni niko hai nachangia sasa katika JF! Ukisikiliza sana theory hutooa wewee!