Hazina na Serikali Mtandao chunguzeni ufanisi wa malipo ya serikali kupitia control number, huenda tunapigwa kama Rais Samia alivyowahi kutahadharisha

Hazina na Serikali Mtandao chunguzeni ufanisi wa malipo ya serikali kupitia control number, huenda tunapigwa kama Rais Samia alivyowahi kutahadharisha

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Wakati Mhe. Rais anaingia Madarakani aliwataka watendaji wa serikali kufanya tathimini kuhusu aina ya mifumo inayohitajika serikalini na kuboresha ufanisi.

Juzi Kati Tanesco walipata matatizo kwenye mfumo wa LUKU nakupelekea kukosekana kwa huduma hii.

Niliwaza sana kuhusu udukuzi wa kimtandao unaofanyika Duniani kwa sasa, nikajiuliza hatukudukuliwa? Je, malipo yetu ya mtandao yapo salama?

Hi nadhani ndiyo iliyonipelekea niwaze hatupigwi? Na Kama tunapigwa tunapigwa kiasi gani? Nani mwenye uhakika kwamba control number zinazotolewa mara mbili mbili siyo tobo la maafisa tehama na wakandarasi kuibia serikali? Nchi nyingi Duniani zinapigwa mabilioni kupitia mifumo, najiuliza sisi hapa kwetu usalama tumeutoa wapi wa mifumo yetu?

Je, watendaji wa serikali mtandao wanaelewa upo umuhimu wakupitia mifumo ya taasisi zote na benki kujiridhisha kuhusu malipo?

Enzi zetu wahasibu walikuwa wanatengeneza vitabu vyao vya risiti, je watengenezaji wa mfumo hawawwezi kujitengenezea control number au wadukuzi awawezi kuchepusha malipo kwenda kwenye akaunti?

Hebu serikali mtandao fanyeni tathimini bila kuwashirikisha Wataalamu wa ICT wa taasisi mbalimbali ambao naamini wanaficha ukweli wa mifumo kuonyesha inafanya vyema, watafuteni watu randomly na tengenezeni ukaguzi maalumu mtuakikishie fedha zetu zipo salama.

Maana yapo magazeti na vyombo vya habari vinaripoti wizi wa huduma zinazolipiwa kwa control number, huo wizi unafanyika kwa njia gani au wanajiandikia bila kujua huduma zinatolewa vipi?

Hazina mitandao si ya kulala ni kukekesha mnachunguza mianya na kuoziba
 
Kwa kauli za ^Nafungulia Nchi^ ^Mwacheni Kuwashurutisha Wafanyabiashara Kutoa Kodi^ ^Tunasafisha Majiji,^ ni dhahiri kwamba tumepigwa hatari since Day One. Wazalendo sasa tafuteni beacon iliyosalia, rudini Ground Zero, anzeni mapambano ya dhati -- day in & day out -- hadi kirusi gubu kilichorejea Tanzania kiondolewe --- kitake kisitake.
 
Pambaneni msiibiwe enyi wazalendo wa nchi.
 
Tunapigwa sana. Luku ilikuwa welcome call
 
Hakuna kitu cha hovyo cha kuchezea kama mitandao.
 
Acha zako wewe mleta mada!

Hapo hatupigwi ila mataga, sukuma gang na marehemu wanakomolewa.

Na kubwa zaidi bavicha wanasubiri hela zirudi mtaani ili wawe wanaziokota, na wakuzirudisha wanaamini ni hao unaosema wanatupiga.
 
Watz upigaji kama umehalilishwa KILA apatae nafasi uwaza kupiga,baba anapiga ofisini,akampa mama mama nae anapiga za matumizi anatuma kwao, housegirl nae upiga chenji za dukani anatuma kwao.Thus ni vigumu sana kuendelea.
 
Una hoja.

Ila wabongo bado tupo nyuma kwenye udukuzi.

Ingekuwa Nigeria au Sauzi tungekuta bakuli tupu
 
Yaani utengeneze control number ziwe zinaingia kwako serious? control no siyo hela cash labda tukusaidie kama hujui ile ni no ya utambulisho tu ya muamala, unaweza pewa control no na usilipe na maisha yakaenda, ndiyo maana kuna bank reconciliation.
 
Kulipa kwa control namba kunahusisha mitandao ya simu, mabenki na wakala wa serikali nafikiri anaitwa GPSA......sasa transaction ikikamilika unapata risiti yako. Sijui ni wapi kati ya hawa kuna uwezekano wa kupigwa..
 
Shosti Fanya tena research maana naona wizi hapo ni mgumu sana maana kuna reconciliation nyingi zinafanyika hapo. Pamoja na "upuuzi" wake wote, electronic payment ni successful initiative ya JPM.

Hapa alikuwa scientific sana. Ninamkubali sana kwenye scientific ways of controlling finance. He was good licha ya madhaifu kwenye system zetu.
 
Back
Top Bottom