Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
MBUNGE ULAYA: Mheshimiwa Spika napenda kujua ni lini serikali itakarabati barabara ya Adam's court?
WAZIRI: Mheshimiwa Spika napenda kumhakikishia mbunge kuwa barabara hiyo itajengwa katika kipindi cha mwaka ujao wa fedha na kufikia October 1 mwakani itakua imekamilika?
MBUNGE BONGO: Mheshimiwa Spika ni lini serikali itajenga barabara ya Tabora Mbeya kupitia Chunya?
WAZIRI: Mheshimiwa Spika awali ya yote nimpongeze mheshimiwa mbunge aliyeuliza swali. Serikali inatambua umuhimu wa barabara hii hasa kuunganisha watu wa mikoa ya magharibi na
nyanda za juu kusini. Barabara hii itachochea kasi ya maendeleo hasa usafirishaji wa mazao ya chakula na biashara katika maeneo haya mawili. Pia itaongeza wigo wa ajira kwa vijana na
kuwezesha usafirishaji wa vipuri kwa ajili ya uanzishaji wa viwanda. Barabara hii ilibuniwa mwaka 1922 na serikali ya wajerumani kwa ajili ya kusafirisha vibarua wa mashamba ya tumbaku Tabora
kutoka Mbeya. Mwaka 2015 serikali ilikarabati barabara hiyo kwa kiwango cha Changarawe, na hivyo basi kwa kutambua umuhimu wa barabara hiyo serikali itaendelea kuikarabati mara kwa mara na ikiwezekana kuijenga kwa kiwango cha lami. Asante. (makofi pwapwapwa)!
WAZIRI: Mheshimiwa Spika napenda kumhakikishia mbunge kuwa barabara hiyo itajengwa katika kipindi cha mwaka ujao wa fedha na kufikia October 1 mwakani itakua imekamilika?
MBUNGE BONGO: Mheshimiwa Spika ni lini serikali itajenga barabara ya Tabora Mbeya kupitia Chunya?
WAZIRI: Mheshimiwa Spika awali ya yote nimpongeze mheshimiwa mbunge aliyeuliza swali. Serikali inatambua umuhimu wa barabara hii hasa kuunganisha watu wa mikoa ya magharibi na
nyanda za juu kusini. Barabara hii itachochea kasi ya maendeleo hasa usafirishaji wa mazao ya chakula na biashara katika maeneo haya mawili. Pia itaongeza wigo wa ajira kwa vijana na
kuwezesha usafirishaji wa vipuri kwa ajili ya uanzishaji wa viwanda. Barabara hii ilibuniwa mwaka 1922 na serikali ya wajerumani kwa ajili ya kusafirisha vibarua wa mashamba ya tumbaku Tabora
kutoka Mbeya. Mwaka 2015 serikali ilikarabati barabara hiyo kwa kiwango cha Changarawe, na hivyo basi kwa kutambua umuhimu wa barabara hiyo serikali itaendelea kuikarabati mara kwa mara na ikiwezekana kuijenga kwa kiwango cha lami. Asante. (makofi pwapwapwa)!