Hebu lete "top 3" ya mechi bora za fainali UCL kuanzia mwaka 2000 na kuendelea

1998 UEFA Champion final btn Man untd na Bayern Munich, Ole Gunner super sub anawarejesha Man Untd kwenye reli dk za lala salama, binge la game timu zote zimetimia hakuna mdhaifu hapo.
 

Mkuu umenikumbusha huyo Walter pandiani, mechi ya marudiano na Milan alimpiga kanzu MTU mzima maldini halafu akafunga..huyo deportivo ilikuwa weka mbali na children!
 
Hii ya john Terry ilivuma Sana hasa alipo mnyandua mke wa mchezaji wenzake I hope ni mke WA J.Cole

UCL 2005 ya Liverpool na AC Milan is the best Kwangu
J.Cole huyu anyanduliwe mke nayy kitambi mbna
 
Dado prso Dah huyu jamaa simsahau alikuwaga Ac Monaco
 
Aisee bhana mm kwa upande wangu fainali bomba nlizowah kushuhudia na nikazikubali ni mbili,moja ni ila ya Bayern munich vs chelsea chini ya kocha msaidizi roberto de Mateo,chelsea tunachukua ubingwa kwa penalty naikumbuka sana ile penalty ya David Luiz bonge ya penalty

Na ya pili ni ile kati ya real Madrid vs Atletico Madrid

LIle goal la Ramos dk za mwisho anaisawazishia real alaf dk za nyongeza tunashinda 4:1 ilkua shangwe sana kwa kweli nahisi Diego simeone anaifikiria sana ile fainal haswa lile goal la ramos.
 
1998 UEFA Champion final btn Man untd na Bayern Munich, Ole Gunner super sub anawarejesha Man Untd kwenye reli dk za lala salama, binge la game timu zote zimetimia hakuna mdhaifu hapo.
Na hisi ilikuwa mwaka 1999.
 

Deportivo 4-0 Ac Milan

Hii mechi mpaka kesho ntaendelea kuikumbuka, Ilikuwa mechi ya robo fainali sikosei, Mechi ya kwanza San Siro, Deportivo alikula 4-1.

Marudiano pale Riazor Stadium, Super Depo ikaishangaza Dunia kwa kupindua matokeo dhidi ya Ac Milan ya akina Dida, Pirlo, Gattuso, Sheva, Rui Costa tena bingwa mtetezi wa Uefa ikaaga mashindano. Milan
 
Pia mechi ya Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya 2012, Bayern Munich Vs Chelsea.

Bayern wakicheza katika uwanja wai wa nyumbani, waliongoza mechi muda mwingi wa mchezo mpaka pale dakika za lala salama, Didier Drogba aliposawazisha kwa goli maridhawa la kichwa na kufanya ubao usomeke 1-1.

Mechi ikaenda extra time kisha kwenye mikwaju ya penati, ambapo Didier Drogba (The Ivorian Giroud) akapiga penati ya ushindi na kuwapa taji Chelsea.

Pamoja na sifa kubwa alizopewa Didier kwenye fainali, bado wachambuzi wengi wa soka kwa makususdi walifumbia macho kazi kubwa iliyofanywa na Petr Cech, pengine fainali ile ingeisha kwa Bayern kushinda dk 90 tena kwa goli kama 3 kama si mchango mkubwa uliofanywa na Cech.
 
Usiku mmoja wa siku ya jumanne mwaka 2010 pale jijini Barcelona, dunia ikisubiri ione jinsi gani Barcelona ya Guardiola ikipindua matokeo dhidi ya Inter Milan ya Mourinho, baada ya mchezo wa kuanza kuisha Inter 3-1 Barcelona kule jijini Milan nchini Italy.

Mechi ikawadia, Mourinho katika ubora wake alipaki treni, dhidi ya Barcelona ya Xavi, Iniesta, Messi, Ibrahimovic na Thiery Henry.

Dakika ya 14 Thiago Motta wa Inter anakula red card na kufanya Inter wawe pungufu kwa muda mwingi wa mchezo. Xavi alipiga sana pasi, Iniesta akafanya sana penetration ila Ukuta wa Inter muda wote ulikuwa imara chini ya majemedari Zanetti, Maicon, Chrstian Chivu, Walter Samuel, Lucio. Bila kumsahau golikipa Julio Cesar golini.

Dakika 90 mechi inaisha Barcelona 1-0 Inter tena goli alifunga Pique.

Inter Milan akaingia fainali baada ya aggregate ya 3-2 dhidi ya Mabingwa watetezi wa Ulaya.
 
Alicheza penalties ya babu kipara
Na akaokoa kichwa cha kudundisha cha Thomas Muller ..
Na mengine kibao ...

Makipa hawanaga nyota mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…